Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia),
akimkabidhi cheti cha Urais Rais Mteule wa Tanzania Dk.John Magufuli
katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam leo.
Kushoto ni Makamu wa Rais Mteule, Samia Hassan Suluhu.
Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia),
akimkabidhi cheti cha Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu katika hafla
hiyo.
Rais
Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli (kulia), akiwapungia mkono
wananchi wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa cheti cha urais. Kutoka
kushoto ni mgombea urais kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira
na mgombea nafasi hiyo kupitia Chama cha ADC, Chief Lutalosa Yemba.
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi (kushoto), akimpongeza Rais Mteule wa Tanzania Dk. John Magufuli baada ya kuchaguliwa kuwa rais.
Makada
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakishangilia wakati Rais Mteule wa
Tanzania Dk.John Magufuli alipokuwa akitoka Ukumbi wa Diamond Jubilee
kukabidhiwa cheti cha urais.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo.
Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Magufuli akimuonesha Rais Jakaya Kikwete cheti cha ushindi.
Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Makufuli akiwa katika picha ya pamoja na wagombea urais wenzake wa vyama vingine.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akimpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva kwa kusimamia vizuri uchaguzi mkuu wa
2015.
Rais Jakaya Kikwete na Rais Mteule Dk.John Pombe Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na wake zao kwenye hafla hiyo.