Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 5, 2015

Rais JPM kaanza kazi !! Maalim Seif Z’bar? ‘Mashangingi’ je? Polisi jela?.


November 6 2015 tayari ninazo zote zilizozinasa kwenye Uchambuzi wa Magazeti Redioni, hizi hapa kwenye nukuu yake pamoja na audio nilizorekodi.
Rais Dk. Magufuli amesema yeye ndiye Rais, akiri uchaguzi ulikuwa mgumu na amejifunza mengi… Changamoto za uongozi wa Dk. Magufuli zatajwa.
Rais JPM ameanza kazi kwa kumteua George Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu Tanzania, Mawaziri Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye hawakuhudhuria sherehe za kuapishwa Dk. Magufuli, wapingana na matokeo ya Urais.
Mawaziri na Manaibu waliomaliza muda wao warudisha ‘MASHANGINGI’ Ikulu ili yatolewe namba na kufanyiwa matumizi mengine… Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad bado hajarudisha magari ya Serikali japo alisema hadi Novemba 2  2015 Z’bar itakuwa haina Serikali.
JK atoa msamaha kwa wafungwa 4,100  muda mfupi kabla ya kukabidhi madaraka kwa Rais JPM… Majambazi yateka magari Tabora na kupora watu huku wakiimba ‘hapa kazi tu’!!
Aliyekuwa Askari Polisi Oysterbay amehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha…

SIKU YA KWANZA YA DK. MAGUFULI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na wanausalama alipowasili Ikulu mara baada ya Kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli (Katikati) Akiongozana na Mkewe Mama Janet Magufuli walipowasili Ikulu mara baada ya Kuapishwa kwenye sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Uhuru leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na wafanyakazi wa Ikulu mara baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ngoma kama ishara ya kumkaribisha Ikulu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kuapishwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwaongoza baadhi ya marais wa Afrika Kuimba wimbo wa Taifa, Kushoto kwake ni Rais wa Tanzania aliyemaliza muda wake Dk. Jakaya Mrisho Kikwete
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janet Magufuli na Mke wa Rais aliyemaliza muda wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika hafla iliyofanyika mapema leo Ikulu Dar es Salaam
Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ally Mohamed Shein akimueleza jambo Rais wa Kenya Uhuru Kenyata wakati wa hafla iliyofanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiteta jambo na Rais wa Uganda Yoweri Museveni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya Pamoja na baadhi ya viongozi wa nchi za afrika na wawakilishi wa mataifa mengine duniani katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, Kulia ni Rais aliyemaliza muda wake Dk. Jakaya Kikwete na Kulia ni Mke wa Rais Mteule Mama Janet Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyata, Raila Odinga na wake zao
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyata leo Ikilu Jijini Dar es Salaam
Raila Odinga akimkumbatia Rais wa Kenya Uhuru Kenyata katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Raila Odinga, na Mama Janet Magufuli akisalimiana na Raila Odinga wakati wa Hafla iliyofanyika Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwaeleza Jambo Rais wa Kenya Uhuru Kenyata na Rais aliyemaliza Muda wake Dk. Jakaya Mrisho Kikwete leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa awamu ya Pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi na Rais wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu leo Jijini Dar es Salaam

DK. MAGUFULI RASMI URAIS, AAPISHWA LEO JIJINI DAR ES ASALAAM, NI PAMOJA NA MAKAMU WAKE, MAMA SAMIA




Wananchi wenye shauku ya kuona tukio la kuapishwa kwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, wakiwa wamepanga foleni kuingia katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, leo asubuhi
Wananchi wakiwa wamejikinga mvua kwa mwavuli wakati mvua ilipokuwa ikinyesha kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Mwananchi akijikinga muavuli na mwaae wakati mvua ilipokuwa ikinyesha kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Hali ya eneo la kuapishia lilivyokuwa kabla ya tukio la  tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Baadhi ya viongozi wa dini na watu mashuhuri, wakiwa kwenye hema maalum wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Baadhi ya viongozi na wageni waalikwa wakiwsili katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Viongozi wa dini wakienda jukwaa la kuapishia wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan leo
Maadamano kuelekea eneo la kuapisha, yalianza kwa kuongozwa na jaji Mkuu wa Tanzania, katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Jaji Mkuu wa Tanzania na Spika wa Bunge wakipanda jukwaani
Makamu wa Rais Mstaafu, Dk. Mohammed Gharib Bilal na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein wakienda kwenye eneo la kuapisha wakati wa tukio la kuapsihwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Magufuli na Makamu wa Rais Mama samia Suluhu Hassan leo
Rais wa awamu ya tano Dk. John Magufuli akienda eneo la kuapishiwa huku akiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick
Rais Dk. Magufuli akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mohammed Othman Chande kabla ya kuapishwa
Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete akiwasili Uwanjani
Rais mstaafu Dk. Jakaya Kikwete akiwasili Uwanjani
Rais staafu Jakaya Kikwete akienda kukagua gwaride rasmi la kumuaga
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete baada ya kukagua gwaride rasmi
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete baada ya kukagua gwaride la Omega
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akipigiwa mizinga na wimbo wa Taifa
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete baada ya kupigiwa mizinga na wimbo wa taifa
Rais mstaafu Jakaya Kikwete akienda eneo la kuapishiwa Rais mpya Dk. Magufuli
Rais wa awamu ya Tao Dk. John Magufuli akiapishwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo
Rais wa awamu ya tano John Magufuli akitia saini kiapo chake
Rais wa awamu ya tano Dk. John Magufuli akikabidhiwa kiapo chake baada ya kusaini na Jaji Mkuu
Jaji Mkuu akimpongeza Rais John Magufuli baada ya kumuapisha
Rais Dk. John Magufuli akikabidhiwa mkuki ikiwa ni ishara ya kupokea ukumbwa
Dk. Magufuli akionyesha mkuki na ngao baada ya kukabidhiwa
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiapa mbele ya Jaji Mkuu
Mama Samia akisaini kiapo
Jaji Mkuu akimkabidhi Mama Samia kiapo chake baada ya kusaini
Kisha akampongeza
Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Maguli  na Makamu wake wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan wakiwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na makamu wa Rais Mstaafu Dk. Bilal, baada ya kuapishwa.
Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Dk. John Maguli  na Makamu wake wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan wakiwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na makamu wa Rais Mstaafu Dk. Bilal, baada ya kuapishwa.
Sheik Mkuu Mufti wa Tanzania Abubakary Zuberi akisoma dua baada ya Dk. Magufuli na mama Samia kuapishwa
Kardinali Polycarp Pengo akiomba dua baada ya Dk. Magufuli na Mama Samia kuapishwa


Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete na makamu wake Mstaafu Dk. Mohammed Gharib Bilal wakitoka eneo la kuapishia na kwenda jukwaa la juu, baada ya Dk. Magufuli na Mama Samia kuapishwa
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Dk. Bilal wakiwa kwenye gari maalum wakati wakienda jukwaa juu, huku wakionekana wenye furaha
Mama Samia akitoka jukwaani
Vongozi wa dini wakitoka jukwaa la kuapishia
Rais wa awamu ya tano Dk. Magufuli akiwa amebaki na Mkuu wa JJeshi la Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange kwenye jukwaa la kuapishiwa
Rais wa awamu ya tano Dk. John Magufuli akipigiwa mizinga na wimbo wa taifa baada ya kuapishwa


Dk. Magufuli akikagua gwaride la Alfa la Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania kuashiria kuanza utawala wa Urais awamu ya tano
Baadhi ya waliohudhuria hafla hiyo
Baadhi ya waalikwa
Rais Magfuli akienda jukwaa kuu kuungana na viongozi mbalimbali
Viongozi mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na wale wa kutoka nchi za nje wakisimama kumlaki Rais Magufuli jukwaa kuu
Rais Dk. Magufuli akiwasalimia wageni wakati akipanda kwenda jukwaa kuu
Rais Dk. Magufuli akisalimiana na Mkewe Mama Janet
Rais John Magufuli akikumbatiwa kwa Rahaaa, na Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete
"Kiti chako hicho hapo Mzee", Ni kama Rais mstaafu Kikwete alikuwa akisema hivyo kumwambia Rais Magufuli alipowasili jukwaa kuu
Rais Magufuli na Rais Mstaafu Kikwete wakiteta jambo
Rais Magufuli akipokea salam za heshima kutoka kwenye gwari
"HIMA HIMAAAA.. TANZANIAAAA", Wanajeshi wa JWTZ wakipaza sauti wakati wakitoa salam ya Rais kwa Dk. Magufuli


Ndege Vita zikipita Uwanja wa Uhuru kutoa salamu kwa Rais mpya, Dk. agufuli
Licha ya Uwanja wa Uhuru kufuria wananchi lakini mamia wengine walilazimika kubaki nje, baada ya uwanja huo kujaa.
 
Blogger Templates