Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 15, 2015

Duu!! sio Bongo tu hata Ulaya usaliti upo, baada ya kipigo Mourinho kataja wasaliti wake

December 14 ni siku ambayo Ligi Kuu ya Uingereza iliendelea tena ambapo moja kati ya mechi zilizochezwa ni ile ya Leicester City dhidi ya Chelsea. Mchezo huo uliyochezwa kwenye uwanja wa King Power ulimalizika kwa Chelsea kufungwa goli 2-1, matokeo yaliyoifanya Chelsea kufikisha jumla ya mechi 9 ilizofungwa katika mechi 16 walizocheza msimu huu.
Matokeo hayo yamemfanya Kocha Jose Mourinho kuwa na wasiwasi na wachezaji wake kuwa wanamsaliti tofauti na jinsi wanavyojipanga kwenye mazoezi lakini mwisho wa siku wanakuja kupoteza pointi tatu. Mourinho aliongea huku akifoka wakati akifanya mahojiano na vyombo vya habari.
article-0-1CC63E7100000578-287_634x370
“Inachosha sana kutizama kazi ambayo tumefanya ikisalitiwa, wakati mwingine nahisi kama vile nilijitahidi kuimarisha uwezo wa wachezaji wetu msimu uliopita na sasa inaonekana wameshindwa kustahimili ushindani katika kiwango hicho. Hatuwezi maliza katika nafasi 4 za kwanza ila tukijitahidi huenda tukacheza katika ligi ya Europa. Naona haya bila shaka”>>>> Mourinho

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates