Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 15, 2015

SIMBACHAWENE AAGIZA TAKA ZILIZOKUSANYWA WAKATI WA UHURU ZIZOLEWE


wafanyakazi wa wizara ya ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora wakimsikiliza waziri wao George Simbachawene.
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo mjini Dodoma.
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Jumanne Sagini alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma.
Naibu waziri nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora, Selemani Jaffo akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Jumanne Sagini alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akisaini kitabu mara baada ya alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma.
 
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurungenzi wote wa halmashari nchini kuhakikisha wanazoa taka zote zilizokusanywa wakati wa siku ya uhuru kabla ya tarehe 20 mwezi huu.Kauli hiyo aliitoa wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa kikao cha kumkaribisha katika ofisi ya Tamisemi mjini Dodoma.

Alisema kuwa hataki kuona hadi ifikapo tarehe 20 ya mwezi huu kuwa uchafu wa siku ya uhuru bado unaendelea kulalamikiwa na watu kuwa bado haijaondolewa katika maeneo uliokusanywa.“Hadi ifikapo tarehe hiyo sitaki kusikia uchafu bado haujaondolewa katika maeneo ulipokusanywa toka siku ya uhuru lakini pia unapoondolewa huo kuna uchafu mwingine unakuja hivyo basi watendaji wanaohusika wa hakikishe kuwa wanaanda maeneo ya kuupeleka”alisema Simbachawene.

Aidha aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wa kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani awamu ya tano ya haitaendelea kuwalea watendaji wavivu.Kwa upande wake,Naibu Waziri wa wizara hiyo Suleiman Jaffo, aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wao wa zamani ili waweze kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuweza kuboresha maisha ya wananchi.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates