Pages

Ads 468x60px

Thursday, October 29, 2015

Kuanzia wa kwanza mpaka wa mwisho… asilimia mpaka idadi ya kura za matokeo yote ya Urais 2015 Tanzania



Dr. John Pombe Magufuli wa (CCM) ametangazwa mshindi wa kiti cha urais kutoka kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 ambapo ameongoza kwa zaidi ya asilimia 50, matokeo kamili ndio haya hapa chini.

BREAKING: Dr. Magufuli ametangazwa mshindi kiti cha Urais Tanzania, list yote na asilimia viko hapa



October 29 2015 ndio siku yenyewe matokeo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 yametangazwa ambapo Dr. John Pombe Magufuli (CCM) ndio ametangazwa mshindi akiongoza kwa asilimia 58, anaemfatia ni Edward Lowassa akiwa na asilimia 39.
Aliyeshika nafasi ya tatu ni mama Anna wa ACT aliyepata 0.65%, huku Chief Yemba wa ADC akipata 0.43%, wa tano ni Hashim Rungwe wa CHAUMMA 0.32%, huku NRA, TLP na UPDP wakipata wote asilimia 0.05.

Maneno ya kwanza ya Profesa Jay baada ya kushinda kiti cha Ubunge





Bado tupo kwenye headlines za uchaguzi 2015 ambapo msanii mkongwe wa HipHop Tanzania Joseph Haule (Profesa Jay) ni mmoja wa wawashindi wa kiti cha ubunge kwenye uchaguzi huu akiwa amechukua jimbo la Mikumi Morogoro na anachosubiri kwa sasa ni kuingia bungeni.
Prof. ameongea na millardayo.com >>>‘Nawashukuru sana wananchi wa Mikumi kwa kuniamini na kunipa dhamana hii kubwa, watanzania wameniamini kwa sababu ya upeo mkubwa ambao Mungu amenipa, naamini sana katika umoja na mshikamano….! na ndiomaana nimekuwa nasisitiza hata katika kampeni zangu, lazima tushikamane watu wote wa vyama vyote na hata wasio na vyama ili kuikomboa Mikumi yetu ‘ –
.
.
‘Changamoto kubwa ni maji, elimu, miundo mbinu pamoja na ajira, nitaendelea kuwatumikia wananchi wangu kwasababu wao ndio wamenituma Dodoma, mimi kuwa mwanamuziki halitonizuia kuwawakilisha wananchi…. nitaendelea kuwa mwanamuziki na huwenda nikafanya muziki ule wa juu zaidi kwasababu nategemea kukutana na watu wa juu zaidi’– PROFESSOR J
prof
Unaweza ukabonyeza play hapa chini kumsikiliza Professor Jay akizungumza kuhusu ushindi wake wa kiti cha Ubunge

DUNI AZUIWA KUWASILISHA HATI YA PINGAMIZI YA MATOKEO JIJINI DAR LEO.

Mgombea mwenza wa CHADEMA Juma Duni Haji amezuiwa kuingia katika chumba cha kutangazia matokeo ya urais katika ukumbi wa Julius Nyerere wakati zoezi hilo likiendelea baada ya kueleza kuwa ameleta hati ya pingamizi ya matokeo.

Hata hivyo walinzi wa eneo la kutangazia matokeo walimkatalia kuingia katika chumba hicho na kumtaka aende Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchguzi (NEC) kuwasilisha hati yake hiyo na kisha kusindikizwa kwenye gari alilokuja nalo lenye namba T754 DDY aina ya Toyota.
 
Blogger Templates