Dr. John Pombe Magufuli wa (CCM) ametangazwa mshindi wa kiti cha urais kutoka kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 ambapo ameongoza kwa zaidi ya asilimia 50, matokeo kamili ndio haya hapa chini.
Thursday, October 29, 2015
BREAKING: Dr. Magufuli ametangazwa mshindi kiti cha Urais Tanzania, list yote na asilimia viko hapa
October 29 2015 ndio siku yenyewe matokeo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 yametangazwa ambapo Dr. John Pombe Magufuli (CCM) ndio ametangazwa mshindi akiongoza kwa asilimia 58, anaemfatia ni Edward Lowassa akiwa na asilimia 39.
Aliyeshika nafasi ya tatu ni mama Anna wa ACT aliyepata 0.65%, huku Chief Yemba wa ADC akipata 0.43%, wa tano ni Hashim Rungwe wa CHAUMMA 0.32%, huku NRA, TLP na UPDP wakipata wote asilimia 0.05.
Aliyeshika nafasi ya tatu ni mama Anna wa ACT aliyepata 0.65%, huku Chief Yemba wa ADC akipata 0.43%, wa tano ni Hashim Rungwe wa CHAUMMA 0.32%, huku NRA, TLP na UPDP wakipata wote asilimia 0.05.
Maneno ya kwanza ya Profesa Jay baada ya kushinda kiti cha Ubunge
Bado tupo kwenye headlines za uchaguzi 2015 ambapo msanii mkongwe wa HipHop Tanzania Joseph Haule (Profesa Jay) ni mmoja wa wawashindi wa kiti cha ubunge kwenye uchaguzi huu akiwa amechukua jimbo la Mikumi Morogoro na anachosubiri kwa sasa ni kuingia bungeni.
Prof. ameongea na millardayo.com >>>‘Nawashukuru
sana wananchi wa Mikumi kwa kuniamini na kunipa dhamana hii kubwa,
watanzania wameniamini kwa sababu ya upeo mkubwa ambao Mungu
amenipa, naamini sana katika umoja na mshikamano….! na ndiomaana
nimekuwa nasisitiza hata katika kampeni zangu, lazima tushikamane watu
wote wa vyama vyote na hata wasio na vyama ili kuikomboa Mikumi yetu ‘ –
‘Changamoto
kubwa ni maji, elimu, miundo mbinu pamoja na ajira, nitaendelea
kuwatumikia wananchi wangu kwasababu wao ndio wamenituma Dodoma, mimi
kuwa mwanamuziki halitonizuia kuwawakilisha wananchi…. nitaendelea kuwa
mwanamuziki na huwenda nikafanya muziki ule wa juu zaidi kwasababu
nategemea kukutana na watu wa juu zaidi’– PROFESSOR J
Unaweza ukabonyeza play hapa chini kumsikiliza Professor Jay akizungumza kuhusu ushindi wake wa kiti cha Ubunge
DUNI AZUIWA KUWASILISHA HATI YA PINGAMIZI YA MATOKEO JIJINI DAR LEO.
Mgombea
mwenza wa CHADEMA Juma Duni Haji amezuiwa kuingia katika chumba cha
kutangazia matokeo ya urais katika ukumbi wa Julius Nyerere wakati zoezi
hilo likiendelea baada ya kueleza kuwa ameleta hati ya pingamizi ya
matokeo.
Hata hivyo walinzi wa eneo la kutangazia matokeo walimkatalia kuingia katika chumba hicho na kumtaka aende Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchguzi (NEC) kuwasilisha hati yake hiyo na kisha kusindikizwa kwenye gari alilokuja nalo lenye namba T754 DDY aina ya Toyota.
Hata hivyo walinzi wa eneo la kutangazia matokeo walimkatalia kuingia katika chumba hicho na kumtaka aende Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchguzi (NEC) kuwasilisha hati yake hiyo na kisha kusindikizwa kwenye gari alilokuja nalo lenye namba T754 DDY aina ya Toyota.
Subscribe to:
Posts (Atom)