Meneja
wa Kanda ya Dar es Salaam wa kampuni ya GAPCO Tanzania, Jane Mwita
(kati) akibonyeza kitufe kwenye kompyuta kuwatafuta washindi wa droo ya
tatu ya promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" inayoendeshwa na Kampuni
hiyo kwa Wateja wake wa jijini Dar es Salaam,ambapo zaidi ya wateja 20
huibuka kidedea kila wiki. Kulia anaeshuhudia ni Mkaguzi wa michezo ya
kubahatisha nchini, Chiku Saleh na Kushoto ni Meneja Masoko wa GAPCO
Tanzania, Caroline Kakwezi.
Thursday, December 17, 2015
KAMATI YA URATIBU YA SHIRIKISHO LA VYUO ELIMU YA JUU YAANZA VIKAO VYA SIKU MBILI

Mwenyekiti wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Zainab Abdallah (MNEC) akiongoza kikao cha Kamati ya Uratibu Taifa ya la Vyuo vya Elimu ya juu kilichofanyika kwenye ukumbi wa Sekretarieti, Makao Makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Zainab Abdallah (MNEC) akiongoza kikao cha Kamati ya Uratibu Taifa ya la Vyuo vya Elimu ya juu, kulia ni Katibu Mtendaji Ally S. Hapi

Mwenyekiti wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Zainab Abdallah (MNEC) akijadiliana jambo pamoja na Daniel Zenda (katikati) na Ally S. Hapi wakati wa kikao cha Kamati ya Uratibu Taifa ya la Vyuo vya Elimu ya juu.

Wajumbe wa kikao wakichambua mambo mbali mbali.
Kamati ya Uratibu taifa ya Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya Juu leo imeanza kikao cha siku mbili kinachofanyika makao makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba jijini Dar es salaamchini ya Mwenyekiti wake bi Zainab Abdallah(Mnec). Viongozi wengine wanaohudhuria kikao hicho ni Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho Ndg. Hamid Mhina (Mnec), Katibu Mtendaji Ally S. Hapi, Katibu mtendaji Daniel Zenda, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa kutoka Shirikisho Joseph Chitinka,Katibu uchumi na Fedha Richard Luhende, katibu wa siasa na uenezi Fikiri Mzome na katibu wa uhamasishaji Mganwa Nzota.
JAJI MARK BOMANI AMSHAURI MAALIM SEIF AKUBALI UCHAGUZI URUDIWE
Jaji Mkuu na Mwanasheria Mkuu Mstaafu, Mark Boman akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
JAJI
Mkuu na Mwanasheria Mkuu Mstaafu, Mark Boman amesema kuwa Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja Zanzibar, Maalim Seif Hamad akubali
uchaguzi urudiwe Zanzibar kwani kama alishinda atashinda tena kutokana
na waliompigia katika uchaguzi ulifutwa watampIgia kura tena.
Boman
ameyasema hayo leo jijini Dar eS Salaam , wakati akizungumza na
waandishi wa habari amesema kuwa Maalim kujitangazia kuwa ameshinda ni
suala ambalo halikufuata utaratibu hivyo kutokana na mazingira hayo
uchaguzi ufanyike ili kupata Rais wa Serikali ya Zanzibar.
“Kurudia uchaguzi Zanzibar ni jambo lisilo epukika lakini wakae na
kuangalia dosari zilizojitokeza na kufuta uchaguzi lazima lishughukiwe
kisheria bila kufanya hivyo kunaweza kuleta matatizo”amesema Jaji
Mstaafu, Boman.
Amesema kuwa uchaguzi uliofanyika Zanzibar walitakiwa kukaa na
kuona wapi walikosea katika kuondoa changamoto hizo ambapo ilikuwa ngumu
kutokana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha
na wajumbe walishindwa kuafikiana.
Hata hivyo Boman ametaka suala la katiba lazima lishughulikiwe
kuacha kwake ni aibu ya nchi kutokana na mabilioni ya fedha yametumika
katika mchakato huo.
Amesema kuwa migogoro inayotokea ya ardhi na wafugaji pamoja
wakulima inatokana na kutokuwa na katiba ambayo ndio ingekuwa suluhu ya
utatuzi wa migogoro hiyo.
WATANZANIA WANNE WAPATA TUZO ZA UANDISHI WA FASIHI YA KISWAHILI AFRIKA
Afisa
Masoko wa Alaf, Theresia Mmasy akizungumza na waandishi wa habari
(Hawapo pichani)jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwandishi wa kitabu
cha Kolonia Santita, Enock Maregesi na Mwandishi wa Ushairi la Kifaurongo, Christopher Budebah.
Mkuu
wa Idara ya Fasihi ya Mawasiliano na Uchapishaji (TATAKI) WA wa chuo
kikuu cha Dar es Salaam akiwa na baadhi ya viongozi ya ALAF Limited.
Mshiriki
wa Taaluma ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa, Adrian
Mtembei akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Mwandishi wa kitabu cha Kolonia Santita, Enock Maregesi akipokea ua kutoka kwa Meneja Huduma na Masooko Alaf ,Piyush Kanti Nath leo wakati wa kuwapongeza washindi wa uanishi wa fasihi za kiswahili Afrika.
Mwandishi
wa kitabu cha Kolonia Santita, Enock Maregesi akizungumza na waandishi
wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na tuzo aliyoipata katika
uandishi wa wa kitabu cha Kolonia ya Santita.
Mwandishi wa Ushairi la Kifaurongo, Christopher Budebah akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.
KWA
mara ya kwanza Lugha ya Kiswahili imeingia katika rekodi ya dunia kwa
watanzania wanne kuchomoza katika tuzo ya waandishi ya Fasihi Afrika.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mshiriki wa Taaluma ya
Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa, Adrian Mtembei amesema
lugha ya Kiswahili ya kujivunia kutokana na watanzania wenye lugha yao
kuwa washindi.
Washindi
wa tuzo hizo ni Enock Maregesi ambaye aliandika Kolonia
Santita,Chiristophee Bubebah, Anna Manyaza aliandika Penzi la Damu,
Mohamed Ghassani aliandika N’na Kwetu.
Walioshiriki
katika tuzo hiyo walikuwa 65 na kuweza kuibuka watu wanne ambao ni
washindi wakitokea nchini na sherehe hizo zilifanyika Nchini Kenya.
Amesema
kwa lugha ya kifaransa na Kiingereza zimekuwa zikijitokeza kila mwaka
kwa watu kuandika riwaya na mashairi lakini Kiswahili imekuwa
ikisahaulika hivyo na kufanya Chuo Cornell Nchini Marekani iliamua
kufanya hivyo kuwa watu kuandika Riwaya na Mashairi.
Katika
tuzo hizo Kampuni ya watengenezaji wa Mabati ya Alaf ilizamini tuzo
hizo na kutaka watu wajitokeze katika kuinua lugha ya Kiswahili duniani.
Afisa
Masoko wa Alaf, Theresia Mmasy amesema kazi wataendelea kushirikiana na
watanzania katika kukuza Kiswahili katika kudhamini tuzo hizo.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yatangaza Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele
(Picha zote na Benedict Liwenga)
Na Shamimu Nyaki.
Serikali kupitia Mpango wa wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yasiyopewa
kipaumbele leo imetangaza tarehe 19
hadi 23 mwezi huu kuwa itaanza zoezi la kugawa dawa kwa makundi yanayopaswa
kupata dawa za magojwa hayo.
Tamko hilo limetolewa
na Katibu mkuu wa Wizara Ya Afya na Ustawi wa Jamii,Wazee,na Watoto Bw. Donald Mmbando
alipokuwa anazungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake jijini Dar es
Salaam na kusema kuwa Magonjwa ambayo hayapewi
kipaumbele ni Usubi,Vikope (Trakoma), Matende,
Mabusha,Ngiri maji, na Minyoo ya tumbo hivyo dawa hizo zitasaidia kupunguza tatizo.
Ameongeza kuwa zoezi hilo la ugawaji
wa dawa litatekelezwa katika vituo vyote vya Afya, Zahanati,Hospitali, shule za
msingi na sekondari,sokoni,vituo vya usafiri,pamoja na Ofisi za Serikali na
Mashirika ya Umma na hivyo wananchi wanaombwa kujitokeza kwa wingi kupata huduma hiyo ambayo haina malipo
yoyote.
Katibu Mkuu huyo amesema
kuwa wahusika wakuu katika kupatiwa dawa hizo ni Watu wote kuanzia miaka
mitano na kuendelea,isipokuwa watoto chini ya miaka mitano,wajawazito, mama anaenyonyesha mtoto chini ya siku saba na
Wagonjwa Mahututi.
“Tunataka kulinda afya zao na Uhai
wao hivyo tunaomba wafuate maelekezo vizuri”.Alisema Bw Mmbando.
Aidha zoezi hilo litatekelezwa katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Singida,
Dodoma,Mtwara, Lindi na Pwani kwa ajili ya kujikinga na kutibu
magonjwa hayo na Mikoa mingine iliyobaki
itafanya zoezi hilo katika ngazi ya
jamii na shuleni mwishoni mwa mwezi Januari kuendelea hadi Februari
2016.
Naye Mratibu wa Mpango huo Dkt
Edward kirumbi ameeleza kuwa takwimu zainaonyesha kuwa magonjwa
yasiyopewa kipaumbele hapa nchini ni kubwa ambapo ugonjwa wa Usubi umeenea
zaidi katika mikoa sita ikiongozwa na Dodoma, Ugonjwa wa Minyoo ya tumbo
wagonjwa million 13, kichocho ,Matende na Mabusha tathmini za awali zinaonyesha
mikoa 18 imeathirika kwa kuwa na
wagonjwa million 12.
Vile vile Dkt
Kirumbi ameeleza kuwa Magonjwa haya yamekuwa na athari kubwa hasa kwa
kuathiri nguvu kazi ya Taifa hivyo wananchi wanapaswa kupata dawa hizo ambazo
zitakuwa zinatelewa kwa mwaka mara moja ili kukinga upungufu wa Damu, kuuwa vimelea
vya ugonjwa huo, kupungua kwa magonjwa ya ngozi, na kuongeza virutubisho bora
mwilini.
Hata hivyo jamii inapaswa kupewa
elimu zaidi kuhusu Magonjwa haya kwa vile bado haijaelewa athari za magonjwa
haya kwa kiasi kikubwa hasa kwa maeneo
ya vijijini ambayo ndio waathirika wakubwa.
MHAGAMA; alitaka SHIVYAWATA kuondoa tofauti zao
Mkalimani wa lugha ya alama
akifafanua mazungumzo kwa alama kwa baadhi ya wajumbe wa Shirikisho la
Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wakati wa mkutano wa
shirikisho hilo na Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu) Dk. Abdalla Possi
(hayupo pichani), jana jioni (Jumatano, Desemba 16, 2015), katika ukumbi
wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera,Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi
Jenista Mhagama (Mb), (katikati) akimsikiliza Mwenyekiti wa Shirikisho
la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Amon Mpanju
wakati shirikisho hilo lilipo kutana na Naibu Waziri (Watu wenye
Ulemavu) Dk. Abdalla Possi (wa kwanza kushoto), jana jioni (Jumatano,
Desemba 16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu,
Jijini Dar es Salaam, (wa tatu kulia), Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya
Waziri Mkuu, Bibi. Regina Kikuli.
Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu)
Dk. Abdalla Possi, akiteta jambo na mmoja wa wajumbe wa Shirikisho la
Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) mara baada ya
kukutana na wajumbe wa shirikisho hilo jana jioni (Jumatano, Desemba
16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar
es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Shirikisho la
Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wakifuatilia
mazungumzo ya mkutano huo, wakati wa mkutano wa shirikisho hilo na
Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu) Dk. Abdalla Possi, jana jioni
(Jumatano, Desemba 16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya
Waziri Mkuu, Jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………….
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia,
(Sera,Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi
Jenista Mhagama (Mb), amelitaka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye
Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) kuondoa tofauti zao ili kuweza
kushirikiana na serikali ya awamu ya tano ambayo imedhamiria kuimarisha
na kulinda haki za watu wenye ulemavu.
“Mnapaswa kuhakikisha kuwa wale wote wanaoleta tofauti zenu
kuwashughulikieni mapema katika vikao vyenu ili muweze kushirikiana na
sisi katika kuhakikisha mnapata haki ya kulindwa , kuheshimiwa na
usalama. Tunataka nchi yetu baada ya miaka mitano iwe katika historia
nzuri kwa kuwajali watu wenye ulemavu”. Amesema.
Ametoa wito huo wakati akizungumza na Shirikisho la Vyama vya
Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) jana jioni (Jumatano, Desemba
16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar
es Salaam.
Bibi Mhagama alisema: “Tunapaswa tusimuangushe Rais Magufuli kwa
imani aliyoionesha kwenu na kuteua Naibu waziri anayeshughulikia
masuala yanayowahusu ambayo yanaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu,”
alisema.Awali akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa shirikisho
hilo, Amon Mpanju pamoja na kumshukuru Waziri na Naibu Waziri
anayeshughulikia (Watu wenye ulemavu) kwa kuitisha mkutano uliolenga
kujadili vipaumbele vya watu wenye ulemavu nchini pamoja na nchi
zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi alimuomba waziri huyo kuhairisha
ili waweze kukamilisha uaiinishaji changamoto zao vizuri.
“Tunaomba mheshimiwa waziri utupatie muda zaidi tuweze ili
tuweze kuainisha vizuri zaidi changamoto zetu ambazo naamini Naibu
waziri mwenye dhamana ya kushughulikia watu wenye ulemavu amabye pia
tunaimani naye sana ataweza kubaini masuala yanayotuhusu na kuweza
kuyatekeleza katika majukumu yake” alisema.
Mkutano huo uliandaliwa na Naibu Waziri anayeshughulikia watu
wenye Ulemavu Dk. Abdalla Possi, pia ulihudhuliwa na Katibu Mkuu Ofisi
ya Waziri Mkuu aliye wakilishwa na Naibu wake, Bibi. Regina Kikuli na
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri
Mkuu, Obey Assery.
MREFA YAANDAA KOZI YA LESENI C
SHIRIKISHO
la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa kushirikiana na Chama cha Soka Mkoa
wa Mbeya (MREFA) wameandaa kozi ya makocha wa mpira wa miguu Leseni C,
itakayofanyika jijini Mbeya kuanzia Disemba 21- 04 Januari, 2016.
Jumla
ya makocha 46 kutoka katika kanda ya Nyanda za Juu Kusini wanatazamiwa
kushiriki kozi hiyo ya wiki mbili, ambayo itaendeshwa na wakufunzi Kidao
Wilfred na Salum Madadi.
Washiriki
wa kozi hiyo ni Mussa Kasalika, Steven Viera, Golya, Mlekwa, Matokeo
Sigalla, Ernest Nkandi, Felix A. Sosteness, Michael Mwamaja, Daniel
Mwaisabila, Deus Nsheka, Albert Gama, Joseph Abiero, Simon Mwapili,
Bahati Mwaipopo, Willy Ngailo, Charles Makwaza, Paul Msyahila, Osward
Morris, Jacob Ndago, Castor Mahona, Ambilikile Albion, Jumanne Nsunye,
Gowdin Mulenga.
Wengine
ni Abel Shizya, Matatizo Abdallah, Michael Kasekenya, Thomas Kasombwe,
James Wanyato, Rose Njobelo, Amos Chiwaya, Baraka Kibanga, Mohamed
Dondo, Josephat Digna, Shabani Mwaibara, Lucas Kibaja, Yusuph Mlekwa,
Joel Makitta, Josiah Steven, Rashid Kasiga, Charles Njango, Alex
Lusekelo, Shabani Kazumba, Ismail Suleiman, Ibrahim Kasegese, Simon
Bernard, Anthony Mwamlima, Christian Simkoko.
BOMOA BOMOA YATIKISA TENA WAKAZI WA BONDE LA MTO MSIMBAZI JIJINI DAR LEO.
Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi
wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za jiji la Dar es salaam zitafanya zoezi
la kuondoa wavamizi maeneo yote ya Mabondeni, kingo za mito na za
Bahari, maeneo ya wazi, maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi
zaidi ya 150 katika jiji la Dar es salaam. Bomoa bomoa ya leo
inaendelea katika Bonde la mto msimbazi.
Mkuu
wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira
Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari
(hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo
ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga
katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali
zao mapema.
Mkuu
wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira
Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari
(hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo
ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga
katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali
zao mapema.
Wananchi wakitoa samani pamoja na vitu mbalimbali ndani ya nyumba zao ili kupisha ubomoaji wa nyumba zilizo maeneo hatarishi. 

Wananchi pamoja na polisi (Wazee wa kazi) wakiangalia ubomoaji unavyoendelea bila vurugu.
Vijana wakiokota vitu mbalimbali katika maeneo yaliyobomolewa leo jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakiwa maeneo hatarishi ambayo yanasubiri kubomorewa.
Uondoaji wa vyuma katika nyumba inayongoja kubomolewa.
Vitu mbalimbali vikiwa vimetolewa nje ili kupisha ubomoaji wa nyumba.
BANKI YA BARCLAYS WAZINDUA OFISI MPYA JIJINI DAR ES SALAAM
Mwenyekiti
wa bodi wa Benki ya Barclays hapa nchini, Ramadhani Dau akikata utepe
kuashiria uzinduzi wa ofisi mpya kwenye ghorofa ya pili ya jengo la
benki hiyo lililopo jengo la Makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es
Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays
Tanzania, Kihara Maina akiwa na baadhi ya wadau wa benki hiyo wakati wa
kuzindua ofisi ya benki hiyo ghorofa ya pili ya benki hiyo.
Mwenyekiti
wa bodi wa Benki ya Barclays hapa nchini, Ramadhani Dau akifungua
kitambaa kuashiria uzinduzi wa ofisi ya benki hiyo katika jengo la
benki ya Barclays ghorofa ya pili leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina akishuhudia wakati akifungua kitambaa hicho.
Mkurugenzi
mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina akizungumza
na wafanyakazi wa benki ya Barclays hapa nchini (hawapo pichani) leo
jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Barclays hapa nchini wakimsikiliza Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina.
Baadhi ya wanabodi ya benki ya Barclays wakimsikiliza Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina mara baada ya kuzindua ofisi mpya leo jijini Dar es Salaam.
Uongozi wa StarTimes waishukuru Serikali kwa ushirikiano mzuri inaowapa
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akimkaribisha ofisini kwake
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Star Times Tanzania Bi. Zuhura Hanif leo jijini
Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akielezea jambo wakati wa
mazungumzo baina yake na uongozi wa Star Times waliomtembelea ofisini kwake leo
jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes
Tanzania Bw. LEO Liofang na Makamu wa Rais wa StarTimes Africa Bw. Eric Xue
Makamu wa Rais wa StarTimes Africa Bw.
Eric Xue afafanua jambo wakati wa mazungumzo baina ya wawakilishi wa StarTimes na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel (kulia) leo jijini Dar
es Salaam.Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw. LEO Liofang.
Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes
Tanzania Bw. LEO Liofang akielezea
jambo wakati wa mazungumzo baina ya wawakilishi wa StarTimes na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel leo
jijini Dar es Salaam.Katikati ni Makamu wa Rais wa StarTimes Africa Bw. Eric
Xue
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi ya Kadi ya
Krismasi aliyokabidhiwa kwa niaba ya uongozi wa StarTimes Tanzania na Afisa
Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw. LEO Liofang. Katikati ni Makamu wa Rais
wa StarTimes Africa Bw. Eric Xue
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akishukuru mara baada ya kupokea
zawadi ya Kadi ya Krismasi aliyokabidhiwa kwa niaba ya uongozi wa StarTimes
Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw. LEO Liofang (kushoto).
Katikati ni Makamu wa Rais wa StarTimes Africa Bw. Eric Xue
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel(mwenye tai) akitoa neno la
shukrani kwa uongozi wa StarTimes kwa kumtembelea ofisini kwake na kuipongeza
Serikali kwa ushirikiano inaowapa katika kutekeleza wajibu wao kama wabia wa
habari hapa nchini.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO Bw.
Assah Mwambene,Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw. LEO Liofang,Makamu
wa Rais wa StarTimes Africa Bw. Eric Xue na Makamu wa Rais wa StarTimes
Tanzania Bi. Zuhura Hanif
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel(katikati)akiwa katika picha ya
pamoja na wawakilishi wa StarTimes Tanzania walipomtembelea ofisini kwake leo
jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO
Bw. Assah Mwambene, Makamu wa Rais wa
StarTimes Africa Bw. Eric Xue, Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw.
LEO Liofang na Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania Bi. Zuhura Hanif
Subscribe to:
Comments (Atom)



































