Jaji  Mkuu na Mwanasheria Mkuu Mstaafu, Mark Boman akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 
JAJI 
Mkuu na Mwanasheria Mkuu Mstaafu, Mark Boman amesema kuwa Makamu wa 
Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja Zanzibar, Maalim Seif Hamad akubali 
uchaguzi urudiwe Zanzibar kwani kama alishinda atashinda tena kutokana 
na waliompigia katika uchaguzi ulifutwa watampIgia kura tena.
Boman 
ameyasema hayo leo jijini Dar eS Salaam , wakati akizungumza na 
waandishi wa habari amesema kuwa Maalim kujitangazia kuwa ameshinda ni 
suala ambalo halikufuata utaratibu hivyo kutokana na mazingira hayo 
uchaguzi ufanyike ili kupata Rais wa Serikali ya Zanzibar.
“Kurudia uchaguzi Zanzibar ni jambo lisilo epukika lakini wakae na
 kuangalia dosari zilizojitokeza na kufuta uchaguzi lazima lishughukiwe 
kisheria bila kufanya hivyo kunaweza kuleta matatizo”amesema Jaji 
Mstaafu, Boman.
Amesema kuwa uchaguzi uliofanyika Zanzibar walitakiwa kukaa na 
kuona wapi walikosea katika kuondoa changamoto hizo ambapo ilikuwa ngumu
 kutokana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha 
na wajumbe walishindwa kuafikiana.
Hata hivyo Boman ametaka suala la katiba lazima lishughulikiwe 
kuacha kwake ni aibu ya nchi kutokana na mabilioni ya fedha yametumika 
katika mchakato huo.
Amesema kuwa migogoro inayotokea ya ardhi na wafugaji pamoja 
wakulima inatokana na kutokuwa na katiba ambayo ndio ingekuwa suluhu ya 
utatuzi wa migogoro hiyo.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment