SHIRIKA
 la ndege la Etihad, ndege rasmi ya taifa za Falme za kiarabu na 
Cognizant (NSADAQ: CTSH), shirika linaloongoza kwa huduma za teknolojia 
ya habari, ushauri na biashara, leo wametangaza makubaliano ya kimkakati
 yatakayoendesha mabadiliko ya kidijitali pande zote za shirika hilo 
pamoja na washirika wake.
Chini
 ya mpango wao wa miaka mitatu wenye thamani ya mamilioni ya madola, 
Cognizant watawasaidia Etihad kufafanua mkakati wao wakidigitali na 
kutengeza dhana mpya ambayo itatumika katika kutoa huduma bora kwa 
wageni wao watakaosafiri popote na ndege za Etihad.
Kwa kuleta pamoja mikakati ya kidijitali, teknolojia, sekta na 
uzoefu wa ubunifu, Cognizant watafanya utafiti wa hali ya sasa ya 
biashara na teknolojia ya shirika la ndege la Etihad na kutumia utafiti 
huo kutengeneza mazingira ya kidijitali ya kiwango cha hali ya juu, 
itakachowezesha usambazaji kupitia idhaa nyingi, ugawaji wa wateja kwa 
kina zaidi na kubinafsisha ujuzi katika masoko.
Kwa kutumia taarifa mbalimbali na ufahamu wa mteja, Cognizant 
italiwezesha shirika la ndege la Etihad na washirika wake, kuelewa zaidi
 mahitaji ya wageni wake.
Kwa kuunganisha tafiti hizi na mazoea bora, michakato na 
teknolojia, shirika hilo litawapa wageni wake suluhisho, ofa 
zitakazoendana na kila mteja kwa mapenzi yake na itaboresha huduma 
zinazotolewa katika safari nzima kutokana na hali ya uaminifu wao na 
upendeleo wa mteja kama vile bidhaa na huduma, kuchagua wapendapo kukaa 
wakati wa safari, chaguo la mlo, safari kipindi cha sikukuu na 
kadhalika. Kwa shirika hili, hii inamaanisha kufungua mitiririko mipya 
ya mapato, kuongeza chapa na kutengeneza fursa nyingine za kibiashara.
Afisa Mkuu wa Biashara wa shirika la Etihad Peter Baumgartner, 
alisema, “Wageni wetu wamezidi kugeukia idhaa za kidijitali zaidi 
kujiunga nasi na hivyo tunatambua umuhimu wa kuwafikishia ubora wa 
kipekee na usio wa dosari katika sehemu zote tunazofikia. Ushirikiano 
wetu na Cognizant utatusaidia kufikia kiwango bora katika safari za 
kidijitali ambayo itawaburudisha wateja kuanzia kupanga safari hadi 
kununua tiketi, kwenye uwanja wa ndege na kwenye ndege, na itaboresha 
uaminifu wa wageni kwa kuwavutia na kuwashirikisha wageni  katika njia 
mpya na za kisasa.”
Robert Webb ambae ni Afisa Mkuu Habari na Teknolojia wa shirika la
 Ndege la Etihad, alisema “Ushirikiano huu ni muhimu kwa mikakati yetu 
teknolojia na uvumbuzi ambayo hutuimarisha na washirika wetu katika 
kujipanga upya kuwapatia wageni wetu huduma bora katika safari zao 
ambayo inaendana wakati wa safari na tamati yake. Tumechagua Cognizant 
kwa sababu wanaongoza katika programu za kidijitali, uzoefu wa 
kidigitali kwenye huduma za usafiri, ukarimu na ushirikiano wa muda 
mrefu na shirika na pia ni viongozi katika dunia ya teknolojia.”
Afisa Mtendaji Mkuu wa Cognizant, Francisco D’Souza, alisema: 
“Tumefurahia kushirikiana na Etihad kutengeneza shirika la ndege lenye 
kuwapa kilicho bora wateja wake wakati wa safari zao kwa kutumia nguvu 
ya teknolojia ya kisasa. Kwa Cognizant, mfumo wa kidijitali’ inamaanisha
 kuwa na uwezo wa kuunganisha teknolojia, takwimu za kisayansi, vifaa, 
ubunifu na mikakati ya kibiashara kubadili mifumo na uzoefu.
 Ushiriki huu unaweka alama ya kuungana kwa mashirika mawili yenye
 kasi ya uongozi ambayo mikakati yao ya ukuaji inabebwa na uvumbuzi wa 
kidijitali. Timu ya kazi za kidijitali ya Cognizant inafurahia na 
kutegemea mengi kwa kusaidiana na shirika la ndege la Etihad pamoja na 
washirika wake ikiwemo kuleta udhibiti, urahisi na uwazi kwa msafiri wa 
kisasa. 
Muamko wa kidijitali utazidi kuimarisha shirika la Etihad katika 
kuwa na chapa yenye kiwango cha hali ya juu kwa kutoa huduma bora kwa 
wateja.
Kama sehemu ya ushirikiano huu, Cognizant itasimamia program za 
Etihad na kuziunganisha katika jukwaa jipya la kidijitali. Kituo cha 
ubora wa kidijitali itaanzishwa kuendesha uvumbuzi pamoja na washirika 
wakuu wa kiteknolojia wa Etihad.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment