Pages

Ads 468x60px

Monday, November 9, 2015

MAKAMU WA RAIS, MAMA SAMIA AKABIDHIWA OFISI RASMI NA DKT. BILAL, AKARIBISHWA RASMI NA WAFANYAKAZI WA OFISI YAKE.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akipokea nyaraka za Ofisi kutoka kwa Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati wa makabidhiano ya Ofisi yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam,leo No 9, 2015. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Sazi Salula.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisaini Kitabu cha wageni wakati alipoingia Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kukabidhiwa Ofisi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo Nov 9, 2015  Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia kwake), Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Sazi Salula na Naibu Katibu Mkuu wake, baada ya makabidhiano ya Ofisi yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam,leo Nov 9,2015.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi Binafsi ya Makamu wa Rais, baada ya bakabidhiano ya Ofisi yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 9, 2015.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi yake wakati alipowasili kwenye Ofisi yake kwa mara ya kwanza leo baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Bilal. Wafanyakazi hao walijipanga kumpokea huku wakiimba, kupiga makofi na vigeregre wakati akiwasili.

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA ASHIRIKI HAFLA YA DUA YA KUOMBEA TAIFA AMANI, JIJINI DAR


SU1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akihutubia wakati wa hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani,iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Agape Television Network (ATN) Dkt. Anny Fernandes, wakati wa  hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani,iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU3
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Agape Television Network (ATN) Dkt. Anny Fernandes, wakati wa  hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani,iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU4
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik, akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jana. Picha na OMR
SU5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akiagana na baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla ya kuliombea Taifa amani wakati akiondoka ukumbini baada ya kuhutubia katika hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani,iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU6 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akishiriki dua ya pamoja na baadhi ya viongozi, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani Tanzania, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jana Nov 7 2015. Picha na OMR
SU8
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa, akizungumza wakati wa hafla hiyo, alipokuwa akiomba dua maalumu. Picha na OMR
SU9
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla ya kuliombea Taifa amani wakati alipokuwa akiwasili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee kwa ajili ya kuhudhuria hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU10
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Kamanda Suleiman Kova, wakati alipokuwa akiwasili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee kwa ajili ya kuhudhuria hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU11
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Libelata Mulamula, wakati alipokuwa akiwasili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee kwa ajili ya kuhudhuria hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU12
Baadhi ya viongozi wakiwasili kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee
SU13
Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Taifa Bara, Philip Mangula akiteta jambo na aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha TLP, Maximillian Lymo, wakati walipokuwa kwenye hafla maalumu ya kuliombea Taifa Amani, iliyoandaliwa na Kamati ya Amani, jijini Dar es Salaam jana Nov 7, 2015. Picha na OMR
SU14
Sheikh Alhad Mussa, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini ukumbini humo.

Dr. Ssali buys AMI hospital assets, opens international hospital in Dar

Sali International Hospital has acquired all assets belonging to former African Medical Investment (AMI) Hospital which closed business in Dar es Salaam five months ago (May). 
The hospital proprietors, Dr. Edward Tamale-Ssali and his wife Kate Ssali, apart from buying AMI assets, has added more modern equipments and moved to put up a state of the art international hospital at the same premise in Masaki area in Tanzania, which opened its doors for patients early October this year.
Dr. Ssali, a consultant Obstetrician and gynaecologist with diverse experience having worked in this specialty in several hospitals in the UK and other countries, says the investment would break new grounds for healthcare in Tanzania.Briefing a section of journalists who toured the facility recently, Dr. Ssali said he had been under immerse pressure to open the facility from potential clients who were desperately in need of quality services in a good environment. 
“A lot of potential clients ranging from local residents, business men, international and local dignitaries as well as tourists have dropped by the hospital enquiring about the services and expressed their excitement to have such a hospital in town. A lot of health services we offer here were not available since AMI closed and patients had to be flown out of the country to acquire specialized services,” said Dr Ssali.
He said, shortly after announcing start of its operations, the hospital has been attending to an impressive number of out and in-patients, with a steady increase in the patients’ numbers. Dr. Sali said the positive response to the hospital from clients from all walks of life signals a positive business projection.  
“The support we have been getting from the local community and uptake in patient numbers since we started has been gratifying. Our responsibility is to ensure that the trust they place in this facility and their confidence in the services we provide are upheld at all times,” said Dr. Ssali.
He said that as patients’ numbers continue to increase, the road ahead looks promising, adding that; “There is no doubt that the excellent services at Sali International Hospital gives our health facility an upper hand in Tanzania market. It is a journey that is worth a ride.” 
Dr. Ssali, told journalists that his hospital focuses on becoming a leading supplier of private specialist hospitals services across Tanzania, as well as East and Central Africa offering quality in and outpatient services, with plans to root its operations in Tanzania market.  
“We are fortunate to have a number of highly respected specialists on board with extensive experience in areas such as internal medicine, gynecology, cardiology and pediatrics. They are also well versed in treating patients from different cultural backgrounds. Their skills and experience will undoubtedly be of great benefit to our patients.
“Although we have recalled some former AMI specialists, we have also recruited specialists from local medical field with exceptional medical service records and international expatriates, with focus on racial dynamics. This gives SIH an added advantage to serve a rage of patients, thereby raising our performance and hence positively influences our balance sheet portfolio,” he said.   
 
According to Dr. Sali, the 30-bed hospital specializes in medical and surgical disciplines and offers a delivery room, 24-hours emergency center, X-ray department, haemodialysis unit, CT-scan center, 4D ultrasound, neonatal ICU beds, well equipped Intensive Care Unit (ICU) and fully fledged theaters. 
Dr. Sali mentioned that although the hospital opened its doors to patients early last month (October), official opening is scheduled to happen in three months time.

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII WATOA TAARIFA YA UGONJWA WA KIPINDUPINDU


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donan Mmbando akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya Mlipuko wa Ugonjwa wa kipindupindu uliopo sasa ulianza mnamo 15 Agosti 2015, katika Manispaa ya Kinondoni na baadae kusambaa katika Manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam leo jijini Dar es Salaam.
  Waandishi  wa habari wakimsikiliza  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donan Mmbando, leo jijini Dar es Salaam
Wadau mbalimbali wakiwa katika mkutano huo leo  jijini Dar es Salaam
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MLIPUKO wa Ugonjwa wa kipindupindu umesambaa katika mikoa 14  na kufikia wagonjwa 7825 na vifo 106.

Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Donan Mmbando amesema kati ya wagonjwa wote waliougua 3746 sawa na asilimia 67 wanatoka katika mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema kuwa  Mikoa inayotoa taarifa ya kuwepo wagonjwa wapya ni Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, Dodoma, Mwanza, Arusha, Mara, Singida na Tanga.

 Mmbando amesema kuwa  ugonjwa huo umeripotiwa katika mikoa mingine ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Pwani, Singida, Mara, Arusha, Tanga, Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Iringa, Kilimanjaro, Dodoma, Kigoma, Geita pamoja na Rukwa.

Aidha amesema hadi kufikia Novemba 8,2015  idadi ya wagonjwa waliokwisha kuripotiwa tangu mlipuko uanze hapa nchini ni 7825 na vifo 106 amabo ni asilimia 1.3 ya waliougua.

Amesema hatua walizozichukua kwa ugonjwa huo ni kutoa dawa, vifaa vya maabara na vifaa kinga kwa mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Morogoro.
Aliongeza kuwa  Wizara imepokea maombi kutoka mikoa ya Singida, Arusha, Tanga, Mwanza, Mara na Geita kati ya Oktoba 15 mwaka huu  na yanashughukuliwa na utawala, Kupima vipimo vya maabara na kufuatilia ubora wa vipimo kutoka katika mikoa iliyofanya uchunguzi na kuthibitisha uwepo wa ugonjwa huo, Kupeleka timu za watalaam kutoka ngazi ya Mkoa na Taifa kusaidiana na timu za Wilaya husika. 

Aidha tarehe 28 Oktoba 2015, Timu ya Kitaifa ilienda katika mikoa ya Tanga, na Singida na vilevile mkoa wa Manyara pia timu ilienda kwa ajili ya kufuatilia tarifa za kuwepo kwa ugonjwa wa kuhara na kutapika – taarifa ya timu hizi inakamilishwa na itawasilishwa.

Mmbando amesema hatua nyingine Kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya juu ya ufuatiliaji wa ugonjwa na utoaji wa matibabu ,Kutoa elimu ya kwa umma kupitia vyombo vya habari hususani radio na runinga. Aidha, mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini yametolewa, Kuandaa “Water safety plan” kwa kushirikisha wadau mbalimbali ikiwemo WHO, PSI, CDC, MSF, Redcross na USAID. Aidha mpango mkatati huu utajikita kwanza kwa jiji la Dar es salaam kwa kuanzia na hapo baadae itaenda katika mikoa mingine.
Amesema changamoto katika ugonjwa huo ni,Mwitikio hafifu wa jamii juu ya kukabiliana na ugonjwa huu,Jamii kutokuzingatia kanuni za afya na mazingira,Ushiriki mdogo wa sekta nyingine katika kupambana na ugonjwa huu,Ukosefu wa pesa za kuwalipa watumishi wa afya wanaohusika katika zoezi la kukabiliana na ugonjwa huu.

BODI YA MIKOPO YAKANUSHA TAARIFA ZINAZOENEA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII


BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
AWAMU YA PILI YA WANAFUNZI WALIOPANGIWA MIKOPO KWA 2015/2016
BODI  ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuutaarifu umma kuwa kuna taarifa zinazosambazwa na baadhi ya mitandao ya kijamii kuwa Bodi haitatoa mikopo kwa waombaji wapya kwa mwaka wa masomo 2015/2016. Taarifa hizo si za kweli na hivyo Bodi inauomba umma kuzipuuza. 

Aidha, Bodi ya Mikopo inapenda kutoa taarifa kwamba hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 40,836 wa mwaka wa kwanza. Katika awamu ya kwanza, Bodi ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282 waliofanikiwa kupata mikopo na katika Awamu ya Pili iliyotolewa tarehe 9 Novemba, 2015 jumla ya waombaji 28,554 wamepangiwa mikopo.

Majina ya waombaji waliofanikiwa kupata mikopo kutoka katika awamu zote mbili yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb.go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili.

Lengo la Bodi ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wenye sifa kupata mikopo katika mwaka wa masomo 2015/2016, ambao ni 50,830, wanapata mikopo.
Aidha, Bodi inapenda kuwasihi waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa unaendelea.
           
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

NEWZ ALERT: MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI,AMJULIA HALI BI HELLEN KIJO BISIMBA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za Binadam,Bi Hellen Kijo Bisimba aliyelazwa hospital ya Agakhan mapema leo kufuatia ajali ya gari aliyoipata mwishoni mwa wiki barabara ya Al-Hassan Mwinyi jijini Dar, Dkt Magufuli pia amefanya ziara ya kushtukiza katika hopsitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwemo pia alitembelea wodi mbalimbali za wagonjwa na kuwajulia hali zao.
 
Blogger Templates