Pages

Ads 468x60px

Monday, December 14, 2015

Dkt.Kalemani awaagiza TANESCO kuongeza uzalishaiji wa umeme ifikapo mwishoni mwa Desemba 2015

Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (kushoto) akimsikiliza Naibu Mkurugenzi Mtendaji Tanesco Bw.Decklan Mhaiki alipokuwa akimwonyesha mradi wa Kinyerezi I mara baada ya kuwasili katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam

Meneja Mradi TANESCO Mhandisi Simon Jalima (wa pili kushoto) akimwonyesha  Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa pili kulia) moja ya mtambo unaopokea gesi kutoka mtwara na kuisambaza mpaka kituo cha Ubungo alipofanya ziara ya kuona maendeleo ya mradi huo leo katika eneo la mradi Kinyerezi jijini Dar es Salaam, wa kwanza kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Tanesco Bw. Decklan Mhaiki. 

 Meneja Mradi TANESCO Mhandisi Simon Jalima (wa pili kushoto) akimtembeza Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa pili kulia) kumwonyesha mitambo mbalimbali ya uzalishaji wa umeme uliyopo katika kituo hicho cha Kinyerezi I, jijini Dar es Salaam.

 Mmoja wa wataalamu wa kuendesha mitambo inayosambaza nishati ya umeme uliyozalishwa kwa kutumia gesi (Shift Supervisor) Bw. Mohamed Lanzi akimwonyesha Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kulia) mtambo wa usambazaji wa umeme wa Morogoro unaotokea  Kinyerezi I namna wanavyouendesha.
 Meneja Mradi  wa Kinyerezi Extension kutoka Kampuni ya Sumitomo Japan Bw. Shoji Watanabe akimweleza  Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani ni kwa muda gani mradi huo utakamilika mara baada ya kupewa mkataba wa kuanza kazi hiyo, leo Kinyerezi jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kulia) akitoa maagizo kwa Meneja Mradi  wa Kinyerezi Extension kutoka Kampuni ya Sumitomo Japan Bw. Shoji Watanabe (wa kwanza kushoto) alipokuwa akigua eneo la mradi huo leo Kinyerezi jijini Dar es Salaam, (wa pili kulia) ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Tanesco Bw. Decklan Mhaiki.
 
Na Anitha Jonas –MAELEZO
Tarehe 14/12/2015
Dar es Salaam.

Wizara ya Nishati na Madini imewaagiza watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuhakikisha uzalishaji wa umeme katika Mradi wa Kinyerezi I na Kinyerezi II unakamilika ifikapo mwezi Februari 2016  na kuanza kufanya uzalishaji ilikuongeza kiasi cha nishati ya  umeme kufikia zaidi ya Megawati 100.

Agizo hilo lilitolewa leo na Naibu Waziri, Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani alipofanya ziara yake katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia nishati ya Gesi cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam,hii ni baada ya kuelezwa kuwa kituo hicho kwa sasa kinazalisha 70 Megawati za umeme ambaohautoshelezi kwa matumizi ya watanzania.

“Watanzania wamechoshwa na mgao wa umeme na wanaimani kubwa na uzalishaji wa kituo hiki cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi hivyo wanatarajia umeme wa uhakika katika kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kujipatia kipato”,alisema Dkt.Kalemani.

Hata hivyo Dkt. Kalemani aliwapongeza watendaji wa TANESCO na wakandarasi wanaosimamia uendeshaji wa mitambo hiyo ya uzalishaji huku akiwasihii waongeze jitihada za dhati kwani watanzania bado hawaridhishwi na kiasi cha umeme kinachozalishwa kwa sasa.

Kwa upande wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omari Chambo alisema kuna mradi mpya uitwao Kinyerezi Extension unakaribia kuanzishwa hivi karibuni ambao utazalisha Megawati 345 za umeme na kupitia mradi huu uzalishaji wa umeme utaongezeka kwa kiasi kubwa.

“Tutajitahidi kwa sasa umeme usikatike mara kwa mara na jitihada za kusafisha mitambo miwili ya phase I na Phase II inafanyika na itakapokamilika tunatarajia kuzalisha zaidi ya Megawati 140 za umeme na usafishaji wake unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu”,alisema Mhandisi Chambo.

Naye Naibu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Bw.Decklan Mhaiki alisema mradi wa Kinyerezi Extension ambao utagharimu  jumla ya kiasi cha Dola Milioni 340 unatarajia kuanza hivi karibuni mara baada ya kukamilika kwa Mkataba na malipo ya 15% kwa mkandarasi.

Pamoja na hayo wizara ya Nishati na Madini imetoa angalizo kwa watendaji wote wanaozalisha umeme kwa kutumia maji walinde vyanzo vya maji na kuacha kutumia maji hayo kwa matumizi mengine kama ya kilimo.

Uzalishaji wa umeme kwa kutumia Nishati ya Gesi utasaidia kupunguza gharama za watumiaji wa umeme pamoja na kushusha gharama za uzalishaji.

MAJALIWA AMPOKEA WAZIRI JENISTA NA NAIBU MAWAZIRI MAVUNDE NA POSSI


si14
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama  (wapili kushoto), na Naibu Mawaziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Abdallah Possi  (wapili kulia)  na Anthony Mavunde (kulia) baada ya kuwakabidhi taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu wakati waliporipoti Ofisini kwa Waziri Mkuu kuanza kazi Desemba 14, 2015.
si15
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama (katikati), Naibu Mawaziri Dkt. Abdallah Possi (kulia) na Anthony Mavunde (wapili kulia)) baada ya mawaziri hao kuripoti  Ofisini kwake kuanza kazi Desemba 14, 2015. Kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt, Florence Turuka, Wanne kushoto ni katibu Mkuu Kazi na Ajira, Eric Shitindi na watatu kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Regina Kikula.
si16
Waziri Mkuu, Kassim majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama  (kushoto) na Naibu Mawaziri, Dkt. Abdallah Possi (Wapili kulia) na Anthony Mavunde (kulia) baada ya Waziri huyo na Manaibu wake  kuripoti Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba  14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

si2
Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama na Naibu Mawaziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Abdallah Possi na (wapili kushoto) na Anthony Mavunde (kushoto) wakisalimiana na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waliojitokeza kuwapokea na kuwakaribisha wakati walipoingia Ofisini  kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi , Desemba  14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si3
Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama akipokea maua kutoka kwa mtumishi wa ofisi ya Waziri Mkuu, Numpe mwadumbya (kushoto) baada ya kuwasili ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba 14, 2015. (Picha na Ofisi ya 
Waziri Mkuu)
si4
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama (wapili kushoto)  akishuhudia wakati Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde (wapili kulia ) na  Dkt. Abdallah Possi(kulia) wakipokea maua kutoka kwa Mtumishi wa Ofisi ya Waziri Tina Ambros (kushoto) baada ya kuwasili kwenye ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba 14, 2015. (Picha na Ofisiya Waziri Mkuu)
si5
Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama na Naibu Mawaziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Abdallah Possi na (wapili kushoto) na Anthony Mavunde (kushoto) wakisalimiana na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waliojitokeza kuwapokea na kuwakaribisha wakati walipoingia Ofisini  kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi , Desemba  14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si6
Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama na Naibu Mawaziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Abdallah Possi na (wapili kushoto) na Anthony Mavunde (kushoto) wakisalimiana na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waliojitokeza kuwapokea na kuwakaribisha wakati walipoingia Ofisini  kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi , Desemba  14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si8
Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama na Naibu Mawaziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Abdallah Possi na (wapili kushoto) na Anthony Mavunde (kushoto) wakisalimiana na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waliojitokeza kuwapokea na kuwakaribisha wakati walipoingia Ofisini  kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuanza kazi , Desemba  14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si9
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Desemba 14, 2015 baada ya kuwasili ofisini kuanza kazi . Kushoto ni Naibu Waziri wa  Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Abdallah Possi na kulia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si10
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akiteta na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florence Turuka (kabla ya kuwapokea Waziri na Naibu Mawaziri, Ofisini kwake jijini Dar es salaam, Desemba 14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si11
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama wakati aliporipoti Ofisini kwake jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba 14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si12
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde  wakati aliporipoti Ofisini kwake jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba 14, 2015. Katikati ni Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenisa Mhagama .(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
si13
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt Abdallah Possi   wakati aliporipoti Ofisini kwake jijini Dar es salaam kuanza kazi Desemba 14, 2015. Wapili kushoto  ni Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenisa Mhagama  na kulia ni Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN, AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MABALOZI, AMKARIBISHA WAZIRI WA OFISI YAKE JANUARY MAKAMBA.

DE1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe. Jorge Luis Lopez, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa mazungumzo.
DE2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na  Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe. Jorge Luis Lopez, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mhe Makamu, Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa mazungumzo. Picha na OMR
DE3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Yasemin Eralp, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa mazungumzo. Picha na OMR
DE4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na  Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Yasemin Eralp, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mhe Makamu, Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa mazungumzo. Picha na OMR
DE5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Januari Makamba, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa ajili ya kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo. Picha na OMR
DE6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika mazungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Januari Makamba, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 kwa ajili ya kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo. Picha na OMR

DE8
DE9
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Januari Makamba, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mhe Makamu, Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 14, 2015 alipofika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo.

MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI WALETA MAAFA KATIKA KIJIJI CHA DIHINDA MVOMERO MKOANI MOROGORO

Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akiangalia Ng'ombe walio uwawa katika Mgogoro wa wakulima na Wafugaji uliotokea katika kijiji cha Dihinda kata ya Kanga wilayani Mvomero, katika tukio lililotokea Desemba 12 mwaka huu.
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa wakiwajulia hali watu waliojeruhiwa katika mgogoro wa wakulima na wafugaji uliotokea katika kijiji cha Dihinda kata ya Kanga wilayani Mvomero Desemba 12 mwaka huu.
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akizungumza na Mkuu wa wilaya Mvomero, Betty Mkwasa katika kijiji cha Dihinda kata ya Kanga wilayani Mvomero Desemba 12 mwaka huu, walipotembelea katika kijiji hicho na kuona madhara makubwa yaliyojitokeza katika mgogoro wa wakulima na wafugaji. Nchemba alimwagiza Mkuu wa wilaya Mvomero, Beth Mkwasa kuunda kamati ya Ulinzi na Usalama katika wilaya ya Mvomero ili kamati ihusike maeneo yote ya Nchi yetu ili kuhakikisha wanaimarisha ulinzi maeneo yote yenye migogoro, pia wahakikishe waliosababisha maafa wanakamatwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia. 
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akizungumza na wanachi wa kijiji cha Dihinda waliokusanyika katika eneo lililotokea mauaji ya wanyama na baadhi ya watu kujeruhiwa. 

"Natoa rai kwa Wananchi hususani wa jamii ya Wafugaji na Wakulima, kuwa hakuna ardhi au Mnyama mwenye thamani sawa na Maisha ya Mwanadamu yeyote yule, njia bora na salama ya kutatua migogoro hii inayohusisha wakuliama na wafugaji ni kufuata taratibu za kuonana na Uongozi wa Serikali wa eneo husika hatua kwa hatua, Nawaomba wananchi waache kujichukulia sheria mikononi, tunakwenda kuunda kamati za usuruhishi wa migogoro hii kwa kila kijiji zitakazohusisha pande zote mbili ili kubaini wavamizi wa maeneo na kuwachukulia hatua za kisheria." Alisema Nchemba. 

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA KADHI MKUU WA TANZANIA

0d766169-dd05-48f7-8eb5-58506ff0a6c4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Kadhi Mkuu wa Tanzania, Abdallah Mnyasi, ofisini kwake jijini Dar es salaam Desemba 14, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

BALOZI WA IRAN AMTEMBELEA MZEE MWINYI NYUMBANI KWAKE

 Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kulia) akikabidhi Picha yake rasmi kwa Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mh. Mehdi Aghajafari, wakati alipomtembelea Nyumbani kwake, Mikocheni, Jijini Dar es salaam Disemba 14, 2015.
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kulia) akikabidhi Picha kwa Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mh. Mehdi Aghajafari, inayoonyesha sehemu ya Utamaduni wa Tanzania, wakati alipomtembelea Nyumbani kwake, Mikocheni, Jijini Dar es salaam Disemba 14, 2015.
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mh. Mehdi Aghajafari pamoja na Msaidizi wake mpya, Bw. Ali Bagheni. Balozi huyo alifika nyumbani kwa Mzee Mwinyi kwa kumtambulisha Msaidizi wake huyo Mpya, leo Disemba 14, 2015.

NAIBU WAZIRI WIZARA YA MALIASILI NA UTALII ENG. RAMO MATALA MAKANI AAZA KAZI RASMI LEO KATIKA OFISI YAKE MPYA MPINGO HOUSE

Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Eng. Ramo Matala Makani 
(kushoto) akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru (katikati) ofisini kwake leo tarehe 14 Desemba 2015 baada ya kufika kwa mara ya kwanza toka kuteuliwa kwake na Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli kuwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo. 
Katika salam zake kwa uongozi na watumishi wa Wizara hiyo amewaomba ushirikiano wa dhati kwa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa wakati ili kuleta maendeleo katika sekta ya Maliasili na Utalii nchini. Ameongeza kuwa yeye binafsi hawezi kuleta maajabu Wizarani hapo bila kupewa ushirikiano katika kazi. Pichani kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Ndugu Selestine Gesimba.   
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru (kulia) akitoa taarifa fupi ya muundo pamoja na shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mhe. Naibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Ramo Matala Makani muda mfupi baada ya kuwasili katika ofisi yake mpya iliyopo Mpingo House Jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Eng. Ramo Matala Makani 
(kushoto) akimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru wakati akimpa taarifa fupi ya muundo wa Wizara hiyo leo tarehe 14 Desemba 2015 . (Picha na Hamza Temba wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii)

NAPE AAHIDI KUTOA USHIRIKIANO KWA WANAHABARI NA WASHIKA DAU WAKE


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na Wakurugenzi na Viongozi wa Idara mbali mbali walio chini ya Wizara yake ambapo aliwaambia kuwa atasimamia haki za wasanii zinapatikana na hatokuwa na huruma na wale wanaokwamisha au kudhulumu kazi za wasanii.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiwa ofisini kwake .
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akiwasalimu Viongozi, Wakuu wa Idara kwenye kikao cha kwanza ambapo aliwataka kuzingatia kazi na kuzifanya kwa ufanisi.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na Wakurugenzi na Viongozi wa Idara mbali mbali walio chini ya Wizara yake .

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na Wakurugenzi na Viongozi wa Idara mbali mbali walio chini ya Wizara yake ambapo aliwaambia kuwa atashirikiana nao katika kufanikisha yale yatakayowezesha tasnia ya habari, michezo , utamaduni na sanaa na sanaa kukua.

NCHI ZA AFRIKA ZIWEKEZE NGUVU YA PAMOJA KUPAMBANA NA EBOLA

 Dokta Julius Julian Lutwan kutoka Uganda akitoa mada kwa wadau mbalimbali wa afya kutoka katika mashirika na taasisi mbalimbali za Afrika na Ulaya zinazoshughulikia masuala ya afya katika warsha ya siku mbili inayofanyika mkoani Arusha kujadili njia bora za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola na mengineyo katika bara la Afrika na kwingineko dunia.
Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa mambo ya afya ya CORDS ya nchini Ufaransa Professa Nigel Lightfoot akitoa mada kwa wadau mbalimbali wa afya kutoka katika mashirika na taasisi mbalimbali za Afrika na Ulaya zinazoshughulikia masuala ya afya katika warsha ya siku mbili inayofanyika mkoani Arusha kujadili njia bora za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola na mengineyo katika bara la Afrika na kwingineko duniani.
Na Mwandishi Wetu NCHI za kiafrika zimetakiwa kuweka nguvu ya pamoja kuhakikisha zinapata njia bora na za kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola na kuachana na utegemezi wa misaada kutoka nchi wahisani. Dokta Andrew Kitua wa taasisi ya afya ya Ngalakeri ya Morogoro aliyasema hayo jana katika warsha ya siku mbili ya kujadili njia bora na za kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola inayofanyika mkoani Arusha.
 Alisema kwakuwa bara la afrika ni miongoni mwa waathirika wa magonjwa hayo wadau husika katika sekta ya afya kwa pamoja na serikali za nchi husika hazina budi kuwekeza nguvu katika kutafuta suluhisho la magonjwa hayo. Alisema ingawa tayari kuna jitihada mbalimbali zinafanyika katika mapambano dhidi ya magonjwa hayo lakini bado kumeonekana kuna changamoto kubwa ya kukabiliana nayo katika maeneo yanayoathirika.
 “Waafrika tunahitajika kuweka nguvu ya pamoja katika kuhakikisha tunapata njia bora na za kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola,” “Warsha yetu ya siku mbili inayoshirikisha wadau kutoka mashirika na taasisi mbalimbali za afya itajadili na kubadilishana uzoefu wa jinsi ya kupambana na magonjwa hayo na hatimaye kupata mikakati maalumu ya kuiwekea nguvu dhidi ya mapambano hayo,” alisema Dokta Kitua. Kwa upande wake Professa Julias Lutwan kutoka Uganda alisema nchi zote kwa pamoja bila kujali kama zimewahi kuathirika au la zinahitajika kujiweka tayari kukabiliana na magonjwa hayo. 
Alisema kwa afrika ukanda wa nchi za magharibi zinaonekana kupata athari hiyo kwa kiasi kikubwa unapolinganisha na ukanda wa mashiriki lakini bado kwa pamoja tunahitajika kujiweka sawa kwa tahadhari katika hilo. Kwa upande wa changamoto wanazokabiliana nazo katika tafiti wanazofanya kwa pamoja na mapambano ya jumla ya magonjwa hayo alisema mawasiliano na kada za chini katika maeneo ya vijijini ni miongoni mwa changamoto kubwa. 
Alisema kwa kuwatumia wataalamu mbalimbali wa mawasilino wamejitahidi kwa kiasi kikubwa kurahisisha lugha ya mawasiliano ili jamii ya chini iweze kupata ufahamu wa jinsi ya kupambana na magonjwa husika. Warsha hii inayoshirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya kutoka barani afrika na ulaya imeandaliwa kwa pamoja na taasisi za afya za SACIDS na EAIDSNet na kufadhiliwa na taasisi ya afya ya CORDS ya nchini Ufaransa.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI AWAAGIZA WAKUU WA IDARA KUANDAA TAARIFA ZA IDARA ZAO.


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi akizungumza na wakuu Idara katika wizara ya Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi alipokutana nao leo alipokaribishwa kwa mara ya kwanza katika wizara  hiyo, tangu achaguliwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa wizara, na kuwaagiza wakuu wa idara katika wizara hiyo kutoa taaarifa za idara zao ifikapo jumatatu ya wiki ijayo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi akipokea ripoti ya wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Katibu mkuu wa wizara yaWizara wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Alphayo Kidata. Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula. 
Naibu Waziri wa Wizara Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akipokea ripoti ya wizara ya Ardhi, nyumba na Maendeleo makazi leo walipokutana na wakuu wa idara mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi.
Naibu Waziri wa Wizara Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akizungumza na wakuu wa Idara wa wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam, akizungumzia kuhusiana na wawekezaji ambao watakua hawajaendeleza ardhi ambayo walichukua kwa aajili ya uwekezaji na ardhi hiyo kurudishwa kwa wananchi. Kutoka Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara ya Ardhi Nymba na Maendeleo ya Makazi, Alphayo Midata, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi  na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Ardhi, Nymba na Maendeleo ya Makazi, Selassie Mayunga.
Baadhi ya waandishi wa habari pamoja na wakuu wa Idara za wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi leo jijini Dar es Salaam.
 
Blogger Templates