Waziri
 wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akiangalia Ng'ombe walio 
uwawa katika Mgogoro wa wakulima na Wafugaji uliotokea katika kijiji cha
 Dihinda kata ya Kanga wilayani Mvomero, katika tukio lililotokea 
Desemba 12 mwaka huu.
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akiwa na Mkuu 
wa wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa wakiwajulia hali watu waliojeruhiwa 
katika mgogoro wa wakulima na wafugaji uliotokea katika kijiji cha 
Dihinda kata ya Kanga wilayani Mvomero Desemba 12 mwaka huu.
 Waziri
 wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akizungumza na Mkuu wa 
wilaya Mvomero, Betty Mkwasa katika kijiji cha Dihinda kata ya Kanga 
wilayani Mvomero Desemba 12 mwaka huu, walipotembelea katika kijiji 
hicho na kuona madhara makubwa yaliyojitokeza katika mgogoro wa wakulima
 na wafugaji. Nchemba alimwagiza Mkuu wa wilaya Mvomero, Beth Mkwasa 
kuunda kamati ya Ulinzi na Usalama katika wilaya ya Mvomero ili kamati 
ihusike maeneo yote ya Nchi yetu ili kuhakikisha wanaimarisha ulinzi 
maeneo yote yenye migogoro, pia wahakikishe waliosababisha maafa 
wanakamatwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia.
Waziri
 wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akizungumza na Mkuu wa 
wilaya Mvomero, Betty Mkwasa katika kijiji cha Dihinda kata ya Kanga 
wilayani Mvomero Desemba 12 mwaka huu, walipotembelea katika kijiji 
hicho na kuona madhara makubwa yaliyojitokeza katika mgogoro wa wakulima
 na wafugaji. Nchemba alimwagiza Mkuu wa wilaya Mvomero, Beth Mkwasa 
kuunda kamati ya Ulinzi na Usalama katika wilaya ya Mvomero ili kamati 
ihusike maeneo yote ya Nchi yetu ili kuhakikisha wanaimarisha ulinzi 
maeneo yote yenye migogoro, pia wahakikishe waliosababisha maafa 
wanakamatwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia. 
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, Mwigulu Nchemba akizungumza na
 wanachi wa kijiji cha Dihinda waliokusanyika katika eneo lililotokea 
mauaji ya wanyama na baadhi ya watu kujeruhiwa. 
"Natoa rai kwa Wananchi hususani wa jamii ya Wafugaji na Wakulima,
 kuwa hakuna ardhi au Mnyama mwenye thamani sawa na Maisha ya Mwanadamu 
yeyote yule, njia bora na salama ya kutatua migogoro hii inayohusisha 
wakuliama na wafugaji ni kufuata taratibu za kuonana na Uongozi wa 
Serikali wa eneo husika hatua kwa hatua, Nawaomba wananchi waache 
kujichukulia sheria mikononi, tunakwenda kuunda kamati za usuruhishi wa 
migogoro hii kwa kila kijiji zitakazohusisha pande zote mbili ili 
kubaini wavamizi wa maeneo na kuwachukulia hatua za kisheria." Alisema 
Nchemba. 
 
 
 
 
 
 



 
 
0 comments:
Post a Comment