Pages

Ads 468x60px

Monday, December 14, 2015

AIRTEL FURSA YAENDELEA KUBORESHA MAISHA YA MKULIMA WA MBOGAMBOGA

 Meneja masoko wa kampuni ya Airtel kanda ya Ziwa, Emmanuel Raphael (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na kijana Innocent  Aloyce baada ya kumkabidhi  zawadi ya Toyo, alipomtembelea katika shamba lake
mkoani Mwanza wilaya ya Misungwi ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” kwa nyanja mbalimbali miezi sita iliyopita.
 Meneja masoko wa kampuni ya Airtel kanda ya Ziwa, Emmanuel  Raphael (kushoto) akimwangalia  kijana Innocent  Aloyce baada ya kumtembelea katika shamba lake mkoani Mwanza wilaya ya Misungwi ambaye ni
miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa  “Tunakuwezesha” kwa nyanja mbalimbali miezi sita iliyopita.
Meneja masoko wa kampuni ya Airtel kanda ya Ziwa, Emmanuel  Raphael (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na kijana Innocent  Aloyce baada ya kumkabidhi  zawadi ya Toyo, alipomtembelea katika shamba lake
mkoani Mwanza wilaya ya Misungwi ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” kwa nyanja mbalimbali miezi sita iliyopita huku akishuhudiwa na ndugu na wafanyakazi  wa Airtel.      
    
Jijini Mwanza  Wilaya ya Misungwi, kampuni ya Airtel kupitia mradi  wake wa *Airtel  Fursa Tunakuwezesha imefurahishwa na juhudi zilizoonyeshwa na kijana   Innocent Aloyce mkaazi wa kijiji cha Mwalogwabagole ambaye ameonyesha   mafanikio katika shughuli zake za ulimaji mbogamboga na nyanya  tangu    kupatiwa  mashine ya kuvuta maji kwa ajili ya umwagiliaji pamoja na jembe  la plau miezi mitatu iliopita.

Airtel kupitia mradi wake wa Airtel Fursa Tunakuwezesha, umeendelea
kuwawezesha zaidi vijana  uliowashika mkono,  wanaozidi kuonyesha mafanikio katika kuboresha shughuli zao mbalimbali za kijasiriamali.Ikiwa na lengo la   kuwakwamua vijana kiuchumi na kujiajiri wao wenjewe ili kuondokana na   tatizo la ukosefu wa ajira .

Akielezea changamoto za usafirishaji wa mazao yake  mjasiliamali huyu
ameeleza tofauti anayoiona mara baada ya kukabidhiwa chombo cha
usafirishaji mazao kutoka kampuni ya simu  ya mkononi ya Airtel
walipomtembelea shambani kwake mwishoni mwa wiki hii na kuona maendeleo  yake ya shughuli zake za ulimaji.

Katika kukabidhi pikipiki kwa ajili ya usafirishaji mazao kwa  Innocent,
meneja masoko wa kampuni ya Airtel kanda ya Ziwa, Emmanuel Raphael
amewataka vijana kuiga mfano unaaonyeshwa na Innocent.

Aliongeza kwa kusema “vijana inabidi waachane na dhamira ya kutaka kukaa tu   vijiweni na kusubiri watafutiwe ajira. Ni juhu di zao wao wenyewe ndio    zitakazoweza kuwakomboa na kupata maendeleo kama alivyoweza kufanikiwa  Innocent.

Kufuatia kushikwa kwake mkono na Airtel leo hii  Innocent meweza
kubadilisha maisha yake na familia yake. Hiyo nawahimiza vijana wasikate
tamaa na kujitokeza kwa wingi kwa kuchangamkia fursa hii na nyingine nyingi  
zinazowazunguka”, .

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates