Mh.
 Prof. Mbarawa akiongea na menejimenti ya Dawasco na Dawassa kwenye 
ukumbi wa Dawasco gerezani,mwishoni mwa wiki jijini Dar.(picha na 
Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii) .
Mh.
 Prof. Makame Mbarawa akisaini kitabu cha wageni akiwa na Naibu 
waziri,Injinia Isack Kamwelwe (kushoto), pamoja na katibu mkuu na naibu 
katibu mkuu wa wizara ya maji (kulia) katika ofisi ya afisa mtendaji 
mkuu wa Dawasco. 
 Waziri wa maji mh. Prof. Makame Mbarawa akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Dawasco mapema leo alipotembelea makao makuu ya ofisi hizo
Afisa
 Mtendaji Mkuu wa Dawasco Injinia Cyprian Luhemeja akiwa na waziri wa 
maji Prof. Makame Mbarawa mara tu baada ya kuwasili katika ofisi hizo
Shirika
 la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco) limetakiwa kuongeza 
idadi ya wananchi wanaopata Maji jijini Dar es salaam kutoka wateja 
148,000 waliopo sasa hadi wateja milioni 1 ifikapo Juni  2016.
Akiongea
 na Menejimenti ya Dawasco na Dawasa ikiwa ni siku moja tangu 
kuchaguliwa kwake Waziri wa Maji Mh. Prof Makame Mbarawa alizitaka 
Taasisi hizo kuweka mkakati wa lazima utakao hakikisha wateja milioni 
wanaunganishwa kwenye mtandao wa Majisafi na salama kwa wakazi wote 
jijini.
“Tumekuja
 kutekeleza ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa bungeni kuhusu Maji. 
Aliahidi Serikali ya awamu ya tano pamoja na mambo mengine watahakikisha
 wana mtua Mama ndoo kichwani” alisema Mh Waziri.
Aliongeza
 kuwa lazima taasisi hizi mbili zijue wajibu wake kwa wananchi na 
kutekeleza ahadi ya Rais ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kutafuta 
Maji na hata wakiyapata gharama zisiwe juu, ameitaka Dawasco kuhakikisha
 inawahimiza wateja wake wote na taasisi za serikali kulipia Ankara za 
Maji kwa wakati.
Aidha
 amewahimiza Dawasa kuboresha mtandao wa Majitaka ili kuwafikia wateja 
wengi zaidi wanaohitaji huduma hiyo ya Majitaka na kuepusha usumbufu kwa
 wananchi unaotokana na Majitaka hayo kuendelea kumwagika ovyo katika 
mitaa mingi ya jiji.“Hakikisheni mnaboresha mfumo wote wa Majitaka, 
uendane na mahitaji ya sasa ya jiji ili kuwapunguzia wananchi kupata 
kero mbalimbali zinazotokana na uchavu wa miundombinu ya Majitaka” 
alisema Mh.Mbarawa.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment