Mkurugenzi
  wa taasisi ya utafiti wa mambo ya afya ya CORDS ya nchini Ufaransa  
Professa Nigel Lightfoot akitoa mada kwa wadau mbalimbali wa afya kutoka
  katika mashirika na taasisi mbalimbali za Afrika na Ulaya  
zinazoshughulikia masuala ya afya katika warsha ya siku mbili  
inayofanyika mkoani Arusha kujadili njia bora za kupambana na magonjwa  
ya mlipuko kama Ebola na mengineyo katika bara la Afrika na kwingineko  
duniani. 
Na
 Mwandishi Wetu
NCHI za kiafrika zimetakiwa kuweka nguvu ya pamoja kuhakikisha zinapata 
njia bora na za kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola na
 kuachana na utegemezi wa misaada kutoka nchi wahisani.
Dokta Andrew Kitua wa taasisi ya afya ya Ngalakeri ya Morogoro aliyasema
 hayo jana katika warsha ya siku mbili ya kujadili njia bora na za 
kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola inayofanyika 
mkoani Arusha.
 Alisema
 kwakuwa bara la afrika ni miongoni mwa waathirika wa magonjwa hayo 
wadau husika katika sekta ya afya kwa pamoja na serikali za nchi husika 
hazina budi kuwekeza nguvu katika kutafuta suluhisho la magonjwa hayo.
Alisema ingawa tayari kuna jitihada mbalimbali zinafanyika katika 
mapambano dhidi ya magonjwa hayo lakini bado kumeonekana kuna changamoto
 kubwa ya kukabiliana nayo katika maeneo yanayoathirika.
 “Waafrika
 tunahitajika kuweka nguvu ya pamoja katika kuhakikisha tunapata njia 
bora na za kudumu za kupambana na magonjwa ya mlipuko kama Ebola,”
“Warsha yetu ya siku mbili inayoshirikisha wadau kutoka mashirika na 
taasisi mbalimbali za afya itajadili na kubadilishana uzoefu wa jinsi ya
 kupambana na magonjwa hayo na hatimaye kupata mikakati maalumu ya 
kuiwekea nguvu dhidi ya mapambano hayo,” alisema Dokta Kitua.
Kwa upande wake Professa Julias Lutwan kutoka Uganda alisema nchi zote 
kwa pamoja bila kujali kama zimewahi kuathirika au la zinahitajika 
kujiweka tayari kukabiliana na magonjwa hayo. 
Alisema
 kwa afrika ukanda wa nchi za magharibi zinaonekana kupata athari hiyo 
kwa kiasi kikubwa unapolinganisha na ukanda wa mashiriki lakini bado kwa
 pamoja tunahitajika kujiweka sawa kwa tahadhari katika hilo.
Kwa upande wa changamoto wanazokabiliana nazo katika tafiti wanazofanya 
kwa pamoja na mapambano  ya jumla ya magonjwa hayo alisema mawasiliano 
na kada za chini katika maeneo ya vijijini ni miongoni mwa changamoto 
kubwa. 
Alisema
 kwa kuwatumia wataalamu mbalimbali wa mawasilino wamejitahidi kwa kiasi
 kikubwa kurahisisha lugha ya mawasiliano ili jamii ya chini iweze 
kupata ufahamu wa jinsi ya kupambana na magonjwa husika.
Warsha hii inayoshirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya kutoka 
barani afrika na ulaya imeandaliwa kwa pamoja na taasisi za afya za 
SACIDS na EAIDSNet na kufadhiliwa na taasisi ya afya ya CORDS ya nchini 
Ufaransa.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment