Mgeni
 rasmi Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Edda Sanga(kushoto)  pamoja na 
Mkurugenzi washirika lisilo la kiserikali nchini la International 
Association of Women in Radio and Television (IAWRT) Tanzania Bi. Rose 
Haji Mwalimu wakizindua ripoti ya utafiti kuhusu mwanamke au mtoto wa 
kike anavyopewa nafasi hasa kwenye vyombo vya habari.
 
 
 
 
Bi
 Razia Mwawanga kutoka IAWRT akifungua mkutano wakati wa uzinduzi wa 
ripoti ya utafiti kuhusu wanawake wanavyopewa nafasi hasa katika vyombo 
vya habari hasa hapa nchini.(Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja blog)
Mkurugenzi
 wa Shirika lisilo la kiserikali nchini la International Association of 
Women in Radio and Television (IAWRT) Tanzania Bi. Rose Haji Mwalimu 
akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa ripoti ya utafiti kuhusu 
wanawake wanavyopewa nafasi hasa katika vyombo vya habari hasa hapa 
nchini
Mgeni
 rasmi Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Edda Sanga(kushoto) akiwahamasisha 
wanawake kuwa na uthubutu ili kuyafikia malengo waliyojiwekea na 
kutojiona hawawezi kisa wao ni watoto wa kike, kulia ni Mkurugenzi wa 
IAWRT Tanzania Bi. Rose Haji Mwalimu.
 
Wajumbe wa IAWRT  wakiangalia moja ya filamu inayohusu nafasi ya mwanamke hasa katika jamii.
Wajumbe wa mkutano huo wakiendelea kutoa maoni yao kuhusu usawa wa kijinsia  katika ngazi mbalimbali za maamuzi.
 
Katika ripoti iliyotelewa awali na Shirika 
lisilo la kiserikali nchini la International Association of Women in 
Radio and Television Tanzania (IAWRT), imeonyesha kwamba wanawake au 
mtoto wa kike hapewi nafasi ya moja kwa moja katika kutoa taarifa au 
katika shughuli za kufanya maamuzi katika ngazi mbali mbali tofauti na 
watoto wa kiume au mwanaume. 
Utafiti huo umebaini kwamba mbali na 
kutopewa mtoto wa kike nafasi ya kufanya maamuzi katika ngazi tofauti, 
ambapo wamesema inapelekea wanaume kupata kipato kikubwa zaidi ya 
wanawake.
Katika
 hafla hiyo mgeni rasmi alikuwa ni Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Edda Sanga, 
ambapo ameiomba serikali na vyombo vya habari kuwapa kipaumbele wanawake
 katika ngazi tofauti tofauti za uongozi ili kuweza kuondoa lile tabaka 
lililopo kati ya mwanamke na mwanaume, na pia inaweza kuchangia katika 
maendeleo na mabadiliko ya nchi kiujumla. 
Aliongezea
 kwa kusisitizia kuwa wanawake wenyewe washirikiane na wajitume pale 
wanapopata fursa katika matukio, na pale wanapofanikiwa warudi kuja 
kusaidia kuinua wanawake wengine ambao bado hawajaweza kufika pale 
panapohitajika. 
 
Akizungumza Mkurugenzi wa Shirika lisilo la 
kiserikali nchini la International Association of Women in Radio and 
Television (IAWRT) Tanzania, Bi. Rose Haji Mwalimu alisema kwa wanawake 
inabidi wajitambue na pia wajue thamani zao katika jamii ili waweze 
kufikia malengo yao.
 
Hayo
 aliyasema wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Utafiti kuhusu Mwanamke au 
mtoto wa kike anavyopewa nafasi hasa kwenye vyombo vya habari ambapo 
ilionekana mtoto wa kike hapewi nafasi sawa na mtoto wa kiume.
Hii imekuwa ni changamoto hasa kwa nchi za Afrika kutomthamini mtoto wa kike.
Pia lisisitiza kuwa licha ya juhudi nyingi 
za wanahabari na taasisi za habari kuwainua wanawake na wasichana katika
 vyombo vya habari mathalani Radio bado juhudi zinakabiliana na 
changamoto kadhaa licha ya kuzaa matunda kwa sehemu ndogo na kupelekea 
mwanaume kuwa na nafasi kubwa katika vyombo hivyo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment