Tuesday, December 15, 2015
BANK YA MKOMBOZI YAFUNGUA TAWI JIPYA MJINI BUKOBA.
MVUA ILIONYESHA LEO JIJINI DAR
CHAMA CHA SANAA CHA TINGATINGA CHATILIANA SAINI MKATABA WA MIAKA MITANO WA KUFANYA KAZI NA KAMPUNI YA BRICOLEUR HOLDINGS YA NCHINI JAPAN
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan, Bi. Yu Shiran
(katikati) akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu
kushirikiana kufanya kazi za sanaa na Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga,
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kulia ni Mwenyekiti wa
Kikundi cha Sanaa (Tingatinga), Bwana Zachi Chimwanda na kushoto ni
Mkurugenzi pia wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan, Bwana
Shoji Tsuchiya.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Bwana Godfrey Mngereza
(kushoto) akifafanua jambo wakati wa utiaji saini wa Mkataba wa
makubaliano kati ya Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga na Kampuni ya
Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan. Katikati ni Wakurugenzi
wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan Bwana Shoji Tsuchiya
pamoja na Bi. Yu Shiran.
Na
Tupokigwe Marco na Mwanahamisi Matasi
Chama cha Sanaa
cha uchoraji picha maarufu kama Tinga Tinga kimetiliana saini Mkataba wa
Makubaliano wa miaka mitano wa kufanya kazi kwa pamoja na Kampuni ya
Bricoleur Holdings Co. Ltd ya nchini Japan utakaokiwezesha chama hicho
kunufaika kwa kuuza kazi zake Kimataifa.
Akiongea leo
wakati wa utiaji saini wa Mkataba huo, Mwenyekiti wa Chama cha Sanaa cha Tinga
Tinga, Bwana Zachi Chimwanda ameeleza kuwa, utiaji saini wa Mkataba huo utakua
chachu ya maendeleo katika kuwakomboa wasanii wachoraji katika kipato chao na
kuboresha hali zao za kimaisha kwakuwa kazi zao sasa zitakuwa zikiuzwa ndani na
nje ya nchi.
Kwa upande wake
Katibu Mtendaji wa Baraza la Wasanii la Taifa (BASATA), Bwana Godfrey Mngereza
alieleza kuwa Mkataba waliosaini kati ya Tinga Tinga na watu wa Bricoleur
Holdings Co. Ltd utaimarisha kazi za Wasanii katika fani ya uchoraji ikiwemo
kuongeza vipato vyao.
''Sanaa ni kazi
lakini pia ni biashara, imefika wakati kwa wasanii kufaidika na jasho lao,
kampuni hii watakua wakitafuta masoko kule Japan ili kazi hizi za wachoraji
toka Tanzania ziweze kununuliwa hali ambayo itawaongezea kipato'', alisema
Mngereza.
Aliongeza kuwa
Mkataba uliosainiwa kati ya pande zote mbili umepitia taratibu zote za kiserikali
na Taasisi zinazohusika na mambo ya sanaa na maslahi ya msanii na msanii yule
aliyehusika katika kuchora picha fulani atanufaika na mkataba huo.
''Kwa msanii
atakehusika binafsi na uchoraji picha mkataba utamwezesha kujua atanufaika vipi
na kwa muda gani'', aliongeza Mngereza.Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Kampuni ya Bricoleur Holdings Co. Ltd, Bi. Yu Shiran ameeleza
kuwa mpango huo wa Mkataba kati yao na Tingatinga una lengo la kukitangaza
Chama hicho cha wachoraji wa Tanzania Kimataifa.
‘’Kwa kutumia taarifa
za kidijiti za Tingatinga tutaweza kushirikiana na watengenezaji mbalimbali wa
bidhaa, na ili kulithibitisha hili, sisi na Tingatinga tumekuwa katika mjadala
wa takriban mwaka mzima sasa’’, alisema Bi. Shiran.
Tinga Tinga Arts
Group lilianzishwa nchini Tanzanja na Edward Saidi Tingatinga ambaye alifariki
mwaka 1972 ambapo kwa sasa kundi hilo lipo maeneo ya Oysterbay jijini Dar es
Salaam kikijihusisha na sanaa ya uchoraji.
TAFFA YAIBUA MAPYA YA UTOROSHAJI WA KONTENA
Rais
wa Chama cha Mawakala wa Forodha (Taffa), Stephen Ngatunga (kulia),
akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na njia
zinazotumika kuiba mapato ya serikali bandarini na katika Idara ya
Forodha, Jijini Dar es Salaam jana. kushoto ni maofisa waandamizi wa
chama hicho. Picha na Mpigapicha Wetu
Rais
wa Chama cha Mawakala wa Forodha (Taffa), Stephen Ngatunga (kushoto),
akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na njia
zinazotumika kuiba mapato ya serikali bandarini na katika Idara ya
Forodha, Jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Ofisa Mwandamizi wa chama
hicho, Ernest Kallaghe.
Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CHAMA cha Mawakala wa Forodha nchini (TAFFA) kimesema kuwa wizi wa
kontena bandari ya Dar es Salaam na kusababisha serikali kukosa mapato
ni tatizo la muda mrefu ambalo ni limekuwa likisababishwa na watumishi
wa bandari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Rais
wa TAFFA, Steven Ngatunga amesema tatizo lilojitokeza ya uondoshaji wa
kontena 329 katika bandari Kavu ya Azam ilitokana na baadhi ya watumishi
wa baadhi ya benki na Bandari kuingilia taarifa katika mfumo na
kusababisha serikali kukosa mapato.
Ngatunga amesema kuwa tatizo la serikali kukosa mapato katika
bandari ya Dar es Salaam walishagundua lakini serikali ilishindwa
kuchukua hatua mpaka serikali ya awamu ya tano kugundua hilo na hatua
zimechukuliwa kwa wale waliohusika.
Amesema TAFFA itatoa ushirikiano kwa kile ambacho wanakiona katika
bandari ya Dar es Salaam juu ya watu wanaosababisha serikali kukosa
mapato kwa maslahi yao binafsi.
Aidha amesema kuwa kuna kampuni zilionekana kuwa zipo kwa ajili ya
kukwepa kodi ya serikali ambazo chama kiliona na kupeleka malalamiko
ambayo mwisho wa siku kukawepo urasimu wa kukutana viongozi ambao
wanaweza kushughilikia hilo.
Amesema baadhi ya mawakala walilipia kontena lakini wanaambiwa
malipo hayakufanyika huku wakiwa na kumbukumbu za malipo na kusababisha
kutilia shaka juu ya uadilifu wa watumishi wa benki pamoja na bandari.
TAFFA imesema haiko tayari kwenda na mawakala ambao wanaharibu
taaluma hiyo na kusababishia serikali kukosa mapato ambayo ndio ya
kufanyia maendeleo nchini.
Amesema kuwa kuna kampuni 73 zimefungwa wakati hawahusiki katika
katika uondoshaji wa kontena katika bandari na bandari kavu kutokana na
kampuni hizo kuwa kulipia kontena zinazodaiwa kukwepa kodi.
MAWAKILI ZINGATIENI MAADILI YA TAALUMA YA SHERIA - JAJI MKUU
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akizungumza
na Mawakili 104 walioapishwa leo jijini Dar es salaam. Mhe. Chande amewataka Mawakili
hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia weledi na maadili ya taaluma yao.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande (katikati) akiwa
na Majaji na Watendaji wa Mahakama wakati wa zoezi la kuwaapisha Mawakili wapya
104 katika viwanja vya Karimjee leo jijini Dar es salaam.
Juu na Chini - Mawakili wakiwa wamesimama mbele ya Jaji Mkuu kabla ya
kuapishwa.
Mawakili walioapishwa wakiwa katika picha ya pamoja na
Jaji Mkuu Mhe. Othman Chande na Watendaji wa Mahakama ya Tanzania.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akiongoza
maandamano ya Majaji na Watendaji wa Mahakama wakati wa hafla ya 53 ya kuwapokea
na kuwaapisha Mawakili wapya 104 iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee leo
jijini Dar es salaam.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju
(kulia) akiwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam leo wakati wa
hafla ya 53 ya kuwapokea na kuwaapisha Mawakili wapya 104.
(Na. Aron Msigwa - Dar es salaam).
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande amewataka Mawakili
kote nchini kufanya kazi zao kwa kuzingatia weledi na maadili ya taaluma ya
Sheria na kwamba wasisite kuwaeleza ukweli wateja wao wanaopeleka mashauri
Mahakamani ili kuepuka kupoteza muda na gharama katika masuala yanayoweza
kupatiwa ufumbuzi nje ya Mahakama.
Akizungumza na Mawakili wapya 104 waliohitimu Shule ya
Sheria kwa mwaka 2015 wakati wa hafla ya
53 ya kuwapokea na kuwaapisha iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee leo
jijini Dar es salaam amesema kuwa msingi mkubwa wa kazi yao umejengwa katika
uzingatiaji wa maadili ya taaluma ya sheria.
Amewataka Mawakili hao kubadilika kifikra kwa kuwa
Mawakili Bora ili kujenga imani na uaminifu kwa jamii wanayoihudumia na
kuongeza kuwa sasa wameingia kwenye utaratibu wa kutambuliwa rasmi na
Mahakama ya Tanzania kwa kuwezeshwa kufanya shughuli za uwakili kwenye mahakama
ya Tanzania maeneo mbalimbali nchini.
“Naomba mtambue kuwa kila
Wakili ni Ofisa wa Mahakama hivyo mnao wajibu na jukumu la kusoma, kufuatilia
mashauri mbalimbali ili kuwa na uhakika wa kesi mnazosimamia kuliko kuzitegemea
Mahakama”
Aidha, ameeleza kuwa yapo mambo ambayo yamekua yakifanywa
na baadhi ya Mawakili wasio waaminifu yanayochafua sura ya Taaluma ya Sheria
ikiwemo kutumia nyaraka za kughushi, kuvunja Kanuni na Maadili ya Taaluma huku
baadhi yao wakijikuta wakiingia katika mgogoro na Mamlaka zinazosimamia kitaaluma
taaluma hiyo.
“Nawataka mzingatie sheria,
kanuni na Maadili ya Uwakili, hata hivyo tuna chombo kinachosimamia maadili
yenu, wapo takribani 176 waliokiuka maadili na hawa wanashughulikiwa kwa mujibu
wa Sheria ili kulinda maadili na utendaji wa taluma yenu” Amesisitiza Mhe. Othman.
Amewataka watimize
wajibu wao kwanza kwa wananchi watakaouhudumia pamoja na Mahakama ya Tanzania
ambayo inawataka kufanya kazi zao kwa kuzingatia Sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.
Mhe. Othman amefafanua kuwa Mahakama ya Tanzania
inaendelea na Mkakati wa kupunguza mrundikano wa Kesi Mahakamani kwa
kuhakikisha kuwa kesi zote zinazofikishwa Mahakamani zinamalizika katika kipindi cha chini ya mwaka
1.
Ameeleza kuwa silimia 47 ya kesi zaidi ya 200
zilizokuwepo Mahakama Kuu katika kipindi cha miaka 4 iliyopita zimeendelea
kusisikilizwa kwa ubora na sasa zimebaki asilimia 17 ya kesi hizo jambo
linaonyesha kuongezeka kwa ufanisi wa Mahakama.
Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe.
George Masaju akiwakaribisha Mawakili hao katika familia ya sheria Tanzania
amesema kuwa katika jamii wanao mchango mkubwa katika kuhakikisha Haki na Usawa
vinadumishwa nchini.
Amesema
mawakili hao kabla ya kuapishwa na kuingizwa
kwenye utaratibu wa kutambuliwa kuwa Mawakili wamepitia na kufauru
vigezo vya
kitaaluma vilivyowekwa ili kulinda heshima ya Taaluma ya sheria
nchini.Amewaeleza kuwa mara baada ya kupokea viapo vyao wameingia
kwenye utumishi wa umma kutekeleza majukumu yao ya kikatiba na kuongeza
kwamba
wao kama wanasheria wanatakiwa kuzingatia weledi wa taaluma yao.
Amewataka kuwa makini katika utendaji wao kwa kuepuka
kuwa sehemu ya migogoro na kuepuka kuegemea upande wowote watakapokuwa
wakitimiza majukumu yao ili kuendelea kujenga jamii ya kistaarabu na ya
kidemokrasia.
" Naomba mkumbuke kuwa mna wajibu mkubwa kwa watu
mtakaokuwa mnawahudumia, zingatieni maadili maana ninyi sasa ni sehemu ya
Mahakama ya Tanzania, fanyeni kazi kwa weledi na umakini mkubwa"
Amesisitiza.Amesema utekelezaji wa majuku yao ya kila siku ni
sehemu ya utumishi wao katika umma hivyo wasiruhusu aina yoyote ya ukiukwaji wa
maadili yakitika kutimiza majukumu yao na kuwasaidia wananchi wasiokuwa na
kipato/ wananchi masikini watakakao omba msaada wao wa kisheria.
Aidha amewataka wawe wabunifu, kufanya kazi kwa bidii
na kujiendeleza pale inapowezekana ili waweze kuwa msaada kwa wananchi walio na
kiu ya kupata huduma kutoka kwao.Kwa upande wake Rais wa Chama cha Wanasheria
Tanganyika (TLS) Charles Rwechungura akizungumza wakati wa wa kuwakaribisha
mawakili hao 134 amesema kuwa wao kama Chama cha Wanasheria wanayofuraha ya
kuwakaribisha wanachama wapya kwenye uwanja wa Sheria nchini.
Amesema mawakili hao wameingia katika wakati muafaka
kuongeza nguvu katika kuwahudumia wananchi huku akieleza kuwa shule ya
Wanasheria Tanzania itaendelea kutoa mafunzo na kusimamia viwango vya taaluma
ya sheria nchini na kuwataka mawakili hao kulinda heshima ya taaluma ya sheria
kwa kutoa huduma bora kwa umma.
WAZIRI UMMY MWALIMU AWATAKA WATUMISHI WA SEKTA YA AFYA KUTOFANYA KAZI KWA MAZOEA
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (aliyesimama) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika leo (15.12.2015) Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Donald Mmbando na wa pili kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Hamis Kigwangalla.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (aliyesimama) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika leo (15.12.2015) Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Donald Mmbando na kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Hamis Kigwangalla.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika leo (15.12.2015) Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii mara baada ya kulifungua Baraza hilo leo (15.12.2015) Jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Hamis Kigwangalla (wa tano kutoka kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Donald Mmbando.
PICHA NA ISMAIL NGAYONGA- MAELEZO
Na Ismail
Ngayonga
MAELEZO
Dar Es
Salaam
15.12.2015
SERIKALI imewataka watumishi
wa sekta ya afya nchini kutofanya kazi kwa mazoea na badala yake kufanya kazi
kwa bidii na uadilifu ili kufikia malengo yaliyowekwa.
Hatua
hiyo inaelezwa itasiaidia kurahisisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa
wananchi kwa kutoa huduma bora na zinazofikiwa kwa wakati.
Akifungua
mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa iliyokuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy
Mwalimu alisema kila mtumishi wa umma anapaswa kutekeleza kwa bidii ilani ya
Chama Tawala ya mwaka 2015.
“Sekta
ya Afya imeingizwa kwenye mpango wa Tekeleza kwa Matokeo makubwa sasa, ili
tuyakifia matokeo makubwa sasa pamoja na mambo mengine tunahitaji kubadilika
sana katika utendaji wetu wa kazi” alisema Mwalimu.
Aidha Waziri huyo alisema alisema pamoja na
mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa katika sekta ya afya, Wizara hiyo hiyo hiyo
haina budi kuakabiliana na chyangamoto mbalimbali zinazojitokeza ikiwemo vifo
vya akina mama wajawazito wakati wa kujifungua.
Kwa
mujibu wa Waziri Mwalimu aliwataka watumishi wa Wizara hiyo kutekeleza kwa
vitendo maagizo yaliyotolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika hotuba
yake ya kuzindua Bunge la 11, kwani hotuba yake ni dira ya maelekezo rasmi ya
masuala muhimu yanayopaswa kutekelezwa na kusimamiwa katika kipindi cha miaka
mitano.
Kwa
upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Donald Mmbando alisema katika
kutekeleza mpango wa tekeleza kwa matokeo makubwa sasa, Serikali imeanisha
maeneo 4 ya utekelezaji ili kuboresha huduma bora za afya kwa wanachi.
Dkt.
Mmbando alianisha maeneo hayo kuwa ni pamoja mgawanyo wa watumishi wa kada ya
afya, upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa
tiba na vitendanishi, ubora wa huduma pamoja na kupunguza vifo vya akina mama
wajawazito na watoto.
“Katika
kutekeleza haya, wiki ijayo tutazindua mpango mkakati wa miaka 5 wa sekta ya
afya (2016-20), ambapo tutahakikisha kuwa yote yaliyoanishwa katika Ilani ya
Chama Tawala tunaweza kuyafikia na kuyatekeleza” alisema Dkt. Mmbando
KAMPUNI YA TINGATINGA IMEINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA BRICOLEUR HOLDINGS Co.LIMITED YA JAPAN.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan, Bi. Yu Shiran
(katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu
kushirikiana kufanya kazi za sanaa na Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga,
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kulia ni Mwenyekiti wa
Kikundi cha Sanaa Tingatinga, Bwana Zachi Chimwanda na kushoto ni
Mkurugenzi pia wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan, Bwana
Shoji Tsuchiya.
Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA),
Bwana Godfrey Mngereza akiwa na wanakikundi cha Sanaa cha Tingatinga na
wajapani wakonyesha vibao vilivyochorwa na kikundi cha Sanaa cha Tinga
Tinga jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Bwana
Godfrey Mngereza (kushoto) akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati
wa kusaini Mkataba wa makubaliano kati ya Kikundi cha Sanaa cha
Tingatinga na Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan. Katikati ni
Mkurugenzi wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan Bwana Shoji
Tsuchiya pamoja na Bi. Yu Shiran.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan Bwana
Shoji Tsuchiya (kulia) wakibadilishana mikataba na kupeana mikono na
Mwenyekiti wa Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga, mbele ya waandishi wa
habari leo jijini Dar es Salaam katika wa mkutano uliofanyika katika
Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo
ya Japan Bi. Yu Shiran.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwasikiliza na wakati wa kusaini
wa Mkataba wa Makubaliano ya kufanya kazi na Kikundi cha Sanaa cha
Tingatinga na Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan uliofanyika
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO)
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii..
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii..
Na Zainabu Hamis,Globu ya Jamii.
CHAMA Cha Wasanii wa uchoraji picha aina ya Tingatinga imeingia
mkataba wa miaka tano (5) na kampuni ya Bricoleurholdings Co.Limited ya
nchini Japan, kwa ajili ya kuwatafutia soko nchini Japan
Makabidhiano ya Mkataba huo yamefanyika leo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kampuni ya Bricoleurholdings Co.Limited, Shoji
Tsuchiya amemkabidhi mkataba huo Mwenyekiti wa Chama Cha Tingatinga,
Zack Chimwanda, amesema kuwa kazi hii ya uchoraji wa picha aina ya
Tingatinga imeanza nchini Tanzania ikiwa na mwanzilishi wake Edward Said
Tingatinga ambaye alifariki dunia mwaka 1970 na jina la hilondipo
lilipopatikana kutokana na yeye.
Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Hakimiliki Nchini (Cosota) Doreen
Sinane,amesema kuwa kampuni ya BricoleurholdingsCo,Limited itakuwa
inafanya kazi ya kuuza na kutafuta soko la picha zinazotengenezwa na
wanachama wa Tingatinga.
Kwa upande wa Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA)
Godfrey Ngereza, amesema kuwa sanaa ya uchoraji ni kazi kama kazi
nyingine pia ni biashara inayomfanya msanii kupata kipato pamoja na
kuliingizia taifa mapato.
SIMBACHAWENE AAGIZA TAKA ZILIZOKUSANYWA WAKATI WA UHURU ZIZOLEWE
wafanyakazi wa wizara ya ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora wakimsikiliza waziri wao George Simbachawene.
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo mjini Dodoma.
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo mjini Dodoma.
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George
Simbachawene akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Jumanne Sagini
alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma.
Naibu waziri nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora, Selemani Jaffo akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Jumanne Sagini alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akisaini kitabu mara baada ya alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma.
Naibu waziri nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora, Selemani Jaffo akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Jumanne Sagini alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene akisaini kitabu mara baada ya alipowasili makao makuu ya ofisi hizo mjini Dodoma.
WAZIRI
wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George
Simbachawene amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurungenzi
wote wa halmashari nchini kuhakikisha wanazoa taka zote zilizokusanywa
wakati wa siku ya uhuru kabla ya tarehe 20 mwezi huu.Kauli hiyo aliitoa
wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa
kikao cha kumkaribisha katika ofisi ya Tamisemi mjini Dodoma.
Alisema kuwa hataki kuona hadi ifikapo tarehe 20 ya mwezi huu kuwa uchafu wa siku ya uhuru bado unaendelea kulalamikiwa na watu kuwa bado haijaondolewa katika maeneo uliokusanywa.“Hadi ifikapo tarehe hiyo sitaki kusikia uchafu bado haujaondolewa katika maeneo ulipokusanywa toka siku ya uhuru lakini pia unapoondolewa huo kuna uchafu mwingine unakuja hivyo basi watendaji wanaohusika wa hakikishe kuwa wanaanda maeneo ya kuupeleka”alisema Simbachawene.
Aidha aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wa kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani awamu ya tano ya haitaendelea kuwalea watendaji wavivu.Kwa upande wake,Naibu Waziri wa wizara hiyo Suleiman Jaffo, aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wao wa zamani ili waweze kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuweza kuboresha maisha ya wananchi.
Alisema kuwa hataki kuona hadi ifikapo tarehe 20 ya mwezi huu kuwa uchafu wa siku ya uhuru bado unaendelea kulalamikiwa na watu kuwa bado haijaondolewa katika maeneo uliokusanywa.“Hadi ifikapo tarehe hiyo sitaki kusikia uchafu bado haujaondolewa katika maeneo ulipokusanywa toka siku ya uhuru lakini pia unapoondolewa huo kuna uchafu mwingine unakuja hivyo basi watendaji wanaohusika wa hakikishe kuwa wanaanda maeneo ya kuupeleka”alisema Simbachawene.
Aidha aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wa kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani awamu ya tano ya haitaendelea kuwalea watendaji wavivu.Kwa upande wake,Naibu Waziri wa wizara hiyo Suleiman Jaffo, aliwataka watumishi wa Tamisemi kubadilika katika utendaji wao wa zamani ili waweze kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuweza kuboresha maisha ya wananchi.
Uongozi wa Wizara yenye dhamana na Sanaa wakutana na Viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa kujadili namna ya kuboresha tasnia ya Sanaa nchini
: Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati)
akizungumza na viongozi wa mashirikisho ya sanaa wakati wa kikao cha
kuchanganua changamoto zilizopo katika tasnia ya sanaa jana Jijini Dar
es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Sanaa Bibi. Leah Kihimbi na
kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo
Rais wa Shirikisho la Sanaa za
Maonyesho Bibi. Agnes Lukanga (wapili kulia) akichangia mada wakati wa
kikao kilichoandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
kuchanganua changamoto zilizopo katika tasnia ya sanaa jana Jijini Dar
es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Filamu Bw.
Simon Mwakifamba (wapili kushoto) akifafanua jambo wakati wa kikao
kilichoandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
kuchanganua changamoto zilizopo katika tasnia ya sanaa jana Jijini Dar
es Salaam. Kushoto ni msemaji wa Shirikisho la Filamu Bw. John Kallage.
Baadhi ya viongozi wa mashirikisho
ya sanaa wakifuatilia kwa makini mada zilizokua zikiendelea wakati wa
kikao kilichoandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
kuchanganua changamoto zilizopo katika tasnia ya sanaa jana Jijini Dar
es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (watatu kulia
waliokaa) katika picha ya pamoja na viongozi wa mashirikisho ya sanaa
baada ya kumaliza kikao cha kuchanganua changamoto zilizopo katika
tasnia ya sanaa jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi
Msaidizi Sanaa Bibi. Leah Kihimbi, wapili kushoto ni Katibu Mtendaji
Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo na watatu kushoto ni Rais wa Shirikisho
la Filamu Bw. Simon Mwakifamba.Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
ENHANCE AUTO YAKABIDHI GARI KWA MSHINDI WA SHINDANO LA MATUMIZI BORA YA MITANDAO YA KIJAMII

Kamanda wa Kikosi Usalama barabarani, Mohamed Mpinga (kulia) akimkabidhi zawadi ya gari aina ya Toyota Sarf, mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jackson Kapongo aliyeshinda kupitia mchezo wa Matumizi bora ya Mitandao ya Kijamii iliyoendeshwa na Kampuni ya Enhance Auto ya Jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Enhance Auto, Aatif Farooq Butt.Picha na Father Kidevu Blog.

Mkurugenzi wa Enhance Auto, Aatif Farooq Butt akionesha stika za kuhamasisha usalama barabarani ambazo pia zilizinduliwa na Kamanda Mpinga.

Meneja Mauzo Enhance Auto, Ayaka Kashida akionesha shindano jipya ambalo mshindi atajishindia Toyota Noah mpya.

Jackson Kapongo akiwa katika gari yake Toyota Sarf na pembeni yake ni Kamanda Mpinga.

Hii ndio gari jipya Toyota Sarf aliyo jishindia Kapongo. SOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Wageni mbalimbali waalikwa wakifuatilia tukio hilo.

Bahati na sibu ilichezeshwa na wateja kujishindia mipira .

Mkurugenzi wa Enhance Auto, Aatif Farooq Butta akitoa maelezo ya bahati nasibu ya kushinda mipira.
Na Father Kidevu
MHITIMU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jackson Kapongo ameibuka mshindi na kukabidhiwa gari aina ya Toyota surf lenye thamani ya zaidi ya sh milioni 24 katika shindano lililochezeshwa na kampuni ya kuuza magari ya Enhance Auto.
Kapongo alikabidhiwa gari lake hilo na Kamanda wa Polisi Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga baada ya kushinda katika shindano lililoendeshwa na Enhance Auto likiwataka washiriki kuonesha ni namna gani wanaweza kutumia mitandao ya kijamii na kujiletea manufaa.
Akizungumza kampuni hiyo, Mpinga alisema imekuwa ikichezesha shindano hilo kila mwaka na kushirikisha nchi mbalimbali Afrika ambapo kwa mwaka jana mshindi alipatikana kutoka Zambia lakini kwa mwaka huu ameshinda mtanzania hivyo ni jambo la kujivunia.
Alisema mbali na kutoa zawadi lakini kampuni hizo za magari zinajukumu kubwa la kutoa mchango kwa usalama barabarani kwa kutoa elimu sambamba na kuuza magari yenye viwango vinavyokubalika ili kuepusha ajali zisizo za lazima.
"Natoa wito kwa kampuni zingine kuwekeza katika usalama barabarani na wasifikirie tu kuuza magari bali wahakikishe magari yanakuwa salama na wanaoendesha wanakuwa salama... tuagize magari yenye viwango mana ajali nyingi pia zinasababishwa na ubovu wa magari" alisema.
Mapema Mkurugenzi wa Enhance Auto, Aatif Farooq Butt alisema shindano hilo mshiriki anatakiwa kushiriki kwa kuchagua mitandao yao ya kijamii kwa wingi zaidi na lilishirikisha nchi ambazo wanafanya nao biashara ikiwemo Botswana, Burundi, Jamhuri ya Kongo, Malawi, Msumbiji, Sudan ya Kusini, Uganda, Zambia, Zimbabwe na Tanzania.
Subscribe to:
Posts (Atom)