Rais
 wa Chama cha Mawakala wa Forodha (Taffa), Stephen Ngatunga (kulia), 
akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na njia 
zinazotumika kuiba mapato ya serikali bandarini na katika Idara ya 
Forodha, Jijini Dar es Salaam jana. kushoto ni maofisa waandamizi wa 
chama hicho. Picha na Mpigapicha Wetu
Rais
 wa Chama cha Mawakala wa Forodha (Taffa), Stephen Ngatunga (kushoto), 
akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na njia 
zinazotumika kuiba mapato ya serikali bandarini na katika Idara ya 
Forodha, Jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Ofisa Mwandamizi wa chama 
hicho, Ernest Kallaghe.
Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
CHAMA cha Mawakala wa Forodha nchini (TAFFA) kimesema kuwa wizi wa
 kontena bandari ya Dar es Salaam na kusababisha serikali kukosa mapato 
ni tatizo la muda mrefu ambalo ni limekuwa likisababishwa na watumishi 
wa bandari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Rais 
wa TAFFA, Steven Ngatunga amesema tatizo lilojitokeza ya uondoshaji wa 
kontena 329 katika bandari Kavu ya Azam ilitokana na baadhi ya watumishi
 wa baadhi ya benki na Bandari kuingilia taarifa katika mfumo na 
kusababisha serikali kukosa mapato. 
Ngatunga amesema kuwa tatizo la serikali kukosa mapato katika 
bandari ya Dar es Salaam walishagundua lakini serikali ilishindwa 
kuchukua hatua mpaka serikali ya awamu ya tano kugundua hilo na hatua 
zimechukuliwa kwa wale waliohusika.
Amesema TAFFA itatoa ushirikiano kwa kile ambacho wanakiona katika
 bandari ya Dar es Salaam juu ya watu wanaosababisha serikali kukosa 
mapato kwa maslahi yao binafsi.
Aidha amesema kuwa kuna kampuni zilionekana kuwa zipo kwa ajili ya
 kukwepa kodi ya serikali ambazo chama kiliona na kupeleka malalamiko 
ambayo mwisho wa siku kukawepo urasimu wa kukutana viongozi ambao 
wanaweza kushughilikia hilo.
Amesema baadhi ya mawakala walilipia kontena lakini wanaambiwa 
malipo hayakufanyika huku wakiwa na kumbukumbu za malipo na kusababisha 
kutilia shaka juu ya uadilifu wa watumishi wa benki pamoja na bandari.
TAFFA imesema haiko tayari kwenda na mawakala ambao wanaharibu 
taaluma hiyo na kusababishia serikali kukosa mapato ambayo ndio ya 
kufanyia maendeleo nchini.
Amesema kuwa kuna kampuni 73 zimefungwa wakati hawahusiki katika 
katika uondoshaji wa kontena katika bandari na bandari kavu kutokana na 
kampuni hizo kuwa kulipia kontena zinazodaiwa kukwepa kodi.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment