Naibu
 Waziri, Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiongea na 
watendaji wa Wizara na Taasisi alipokutana nao katika ukumbi wa Wizara 
ya Fedha na Mipango.  Akizungumza na uongozi wa Wizara na Taasisi Mhe. 
Dkt. Ashatu Kijaji aliwaasa viongozi kutekeleza majukumu waliyokabidhiwa
 na kuhakikisha bajeti ya Serikali inalenga vipaumbele vinavyogusa 
wananchi katika kutekeleza ahadi ya Serikali.
Naibu
 Waziri, Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akijadiliana
 na watendaji wa Wizara na Taasisi kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara 
pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara.
Katibu
 Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. 
Servacius Likwelile akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri Wizara ya Fedha na
 Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji kabla ya kuanza majadiliano na 
watendaji wa Wizara na Taasisi.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment