Friday, November 27, 2015
KAHAMA NEWS TZ: BREAKING NEWZZ......: RAIS MAGUFULI AMSIMAMISHA KA...
KAHAMA NEWS TZ: BREAKING NEWZZ......: RAIS MAGUFULI AMSIMAMISHA KA...: Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania, Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli amemsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 27 Nov....
BREAKING NEWZZ......: RAIS MAGUFULI AMSIMAMISHA KAZI KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA MAPATO (TRA).
Rais
wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania, Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli
amemsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 27 Nov. 2015, Kamishna Mkuu wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Rished Bade kufuatia ziara ya
kushtukiza ya Waziri Mkuu, Mh. Majaliwa Kasimu Majaliwa mapema leo
asubuhi Bandarini jijini Dar es salaam.
Hatua
hiyo imekuja baada kubaini kupitishwa kwa makontena zaidi ya 300 na
kusababishia hasara Serikali ya zaidi ya shilingi bilioni 80.
Rais
Magufuli pia amemteua Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Philip
Mpango kukaimu nafasi hiyo mpaka hapo uchuguzi utakapo kamilika.
Taarifa
hiyo iliyosomwa na Katibu Mkuu Kingozi, Balozi Ombeni Sefue Ikulu
jijini Dar es salaam, imewataka maofisa wote wa TRA kutosafiri nje ya
nchi mpaka pale uchunguzi dhidi yao utakapo kamilika.
BREAKING NEWZZZZZ....WAZIRI MKUU MAJALIWA AVAMIA BANDARI LEO, AAMRISHA KUKAMATWA KWA MAAFISA KIBAO WA TRA
WAZIRI
MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi maafisa watano na
watumishi watatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutokana na upotevu
wa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 80/-.
Akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA katika ziara ya kushtukiza leo mchana (Ijumaa, Novemba 27, 2015), Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Lusekelo Mwaseba wahahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na kwamba fedha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.
Akitangaza uamuzi huo baada ya kufanya kikao na baadhi ya viongozi wa Serikali bandarini hapo, Waziri Mkuu aliwataja maafisa waliosimamishwa kazi kuwa ni Kamishna wa Forodha, Bw. Tiagi Masamaki na Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Wateja, Bw. Habibu Mponezya.
“Hawa wanasimamishwa kazi. IGP ninaagiza hawa watu wakamatwe na kuisaidia polisi. Hati zao za kusafiria zikamatwe na mali zao zikaguliwe kama zinaendana na utumishi wa umma,” alisema Waziri Mkuu.
Maafisa wengine waliosimamishwa kazi ni Mkuu wa kitengo cha TEHAMA, Bw. Haruni Mpande, Bw. Hamisi Ali Omari (hakutaja ni wa idara gani), na Mkuu wa Kitengo cha Bandari Kavu (ICD In-Charge), Bw. Eliachi Mrema. “Hawa wanasimamishwa kazi hadi uchunguzi utakapokamilika na pia wawe mikononi mwa polisi,” alisema.
Pia aliagiza watumishi watatu wa mamlaka hiyo wahamishwe kutoka Dar es Salaam na kupelekwa mikoani. Watumishi hao ni Bw. Anangisye Mtafya, Bw. Nsajigwa Mwandengele na Bw. Robert Nyoni.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemwagiza Katibu Mkuu wa Hazina, Dk. Servacius Likwelile ambaye alikuwepo kwenye kikao hicho, kuhakikisha kuwa anapeleka wataalamu kutoka Wakala wa Serikali Mtandao (e-Govt) haraka iwezekanavyo ili wakakague mifumo ya taarifa na kubaini jinsi ambavyo wizi huo unafanyika.
“Ninataka uchunguzi uanze kufanyika mara moja, tafuteni njia ambazo zinatumika kama mianya ya wizi kutokea hapa bandarini hadi kwenye ICDs. Nataka hayo makontena yatafutwe hadi yajulikane yako wapi, na fedha hiyo ihakikishwe inarudi serikalini,” alisema.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Bw. Ernest Mangu, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florens Turuka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM, Suleiman Kova, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Bw. Awadh Massawe na viongozi mbalimbali kutoka TRA na TPA.
Mapema akijibu maswali ya Waziri Mkuu, Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Bade alikiri kwamba kuna upotevu wa makontena ambao huwa unafanyika kati ya bandarini na ICDs na hasa ICD ya Ubungo. Akitoa ufafanuzi, alisema kwamba walifanya ukaguzi kwenye ICD moja na kukuta makontena 54 yamepotea kwa njia za wizi. “Hata hivyo, tulipoendelea na ukaguzi, namba iliongezeka na kufikia 327. Tunaendelea kufuatilia kwa kushirikiana na TAKUKURU. Mmiliki wa ICD ametakiwa kulipa faini sh. bilioni 12.6/- na ameshalipa sh. bilioni 2.4/-,” alifafanua.
Alipoulizwa na Waziri Mkuu kama ana majina ya watumishi wanaohusika na wizi huo, Bw. Bade akakiri kwamba anayo lakini siyo kwa wakati huo labda ayapate kutoka kwa wasaidizi wake. Ndipo Waziri Mkuu akamuonyesha orodha ya makontena 349 yenye taarifa zote hadi namba za magari yaliyobeba mizigo hiyo na Bw. Bade akakiri kwamba orodha hiyo ni ya kweli.
“Kwa utaratibu huo hatuwezi kufika, labda baadhi ya watu waondolewe kazini”. Ndipo akaanza kutaja majina ya maafisa hao waliosimamishwa kazi.
Akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA katika ziara ya kushtukiza leo mchana (Ijumaa, Novemba 27, 2015), Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Lusekelo Mwaseba wahahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na kwamba fedha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.
Akitangaza uamuzi huo baada ya kufanya kikao na baadhi ya viongozi wa Serikali bandarini hapo, Waziri Mkuu aliwataja maafisa waliosimamishwa kazi kuwa ni Kamishna wa Forodha, Bw. Tiagi Masamaki na Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Wateja, Bw. Habibu Mponezya.
“Hawa wanasimamishwa kazi. IGP ninaagiza hawa watu wakamatwe na kuisaidia polisi. Hati zao za kusafiria zikamatwe na mali zao zikaguliwe kama zinaendana na utumishi wa umma,” alisema Waziri Mkuu.
Maafisa wengine waliosimamishwa kazi ni Mkuu wa kitengo cha TEHAMA, Bw. Haruni Mpande, Bw. Hamisi Ali Omari (hakutaja ni wa idara gani), na Mkuu wa Kitengo cha Bandari Kavu (ICD In-Charge), Bw. Eliachi Mrema. “Hawa wanasimamishwa kazi hadi uchunguzi utakapokamilika na pia wawe mikononi mwa polisi,” alisema.
Pia aliagiza watumishi watatu wa mamlaka hiyo wahamishwe kutoka Dar es Salaam na kupelekwa mikoani. Watumishi hao ni Bw. Anangisye Mtafya, Bw. Nsajigwa Mwandengele na Bw. Robert Nyoni.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemwagiza Katibu Mkuu wa Hazina, Dk. Servacius Likwelile ambaye alikuwepo kwenye kikao hicho, kuhakikisha kuwa anapeleka wataalamu kutoka Wakala wa Serikali Mtandao (e-Govt) haraka iwezekanavyo ili wakakague mifumo ya taarifa na kubaini jinsi ambavyo wizi huo unafanyika.
“Ninataka uchunguzi uanze kufanyika mara moja, tafuteni njia ambazo zinatumika kama mianya ya wizi kutokea hapa bandarini hadi kwenye ICDs. Nataka hayo makontena yatafutwe hadi yajulikane yako wapi, na fedha hiyo ihakikishwe inarudi serikalini,” alisema.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Bw. Ernest Mangu, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florens Turuka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM, Suleiman Kova, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Bw. Awadh Massawe na viongozi mbalimbali kutoka TRA na TPA.
Mapema akijibu maswali ya Waziri Mkuu, Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Bade alikiri kwamba kuna upotevu wa makontena ambao huwa unafanyika kati ya bandarini na ICDs na hasa ICD ya Ubungo. Akitoa ufafanuzi, alisema kwamba walifanya ukaguzi kwenye ICD moja na kukuta makontena 54 yamepotea kwa njia za wizi. “Hata hivyo, tulipoendelea na ukaguzi, namba iliongezeka na kufikia 327. Tunaendelea kufuatilia kwa kushirikiana na TAKUKURU. Mmiliki wa ICD ametakiwa kulipa faini sh. bilioni 12.6/- na ameshalipa sh. bilioni 2.4/-,” alifafanua.
Alipoulizwa na Waziri Mkuu kama ana majina ya watumishi wanaohusika na wizi huo, Bw. Bade akakiri kwamba anayo lakini siyo kwa wakati huo labda ayapate kutoka kwa wasaidizi wake. Ndipo Waziri Mkuu akamuonyesha orodha ya makontena 349 yenye taarifa zote hadi namba za magari yaliyobeba mizigo hiyo na Bw. Bade akakiri kwamba orodha hiyo ni ya kweli.
“Kwa utaratibu huo hatuwezi kufika, labda baadhi ya watu waondolewe kazini”. Ndipo akaanza kutaja majina ya maafisa hao waliosimamishwa kazi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Maagizo ya Rais Magufuli kuhusu safari za nje za watendaji wa Serikali yaanza kutekelezwa
Kufuatia
maagizo ya Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania aliyoyatoa hivi karibuni ya kusitisha safari za nje kwa
Wizara, Idara na Taasisi za Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa imeanza kutekeleza maagizo hayo kwa kutoa
maelekezo mahsusi kwa Balozi zake nje.
Wizara
imezielekeza Balozi zote zilizopo maeneo mbalimbali duniani kujipanga
ili kushiriki kikamilifu katika kuiwakilisha Serikali kwenye mikutano
yote ya kimataifa na kikanda inayofanyika katika maeneo yao ya
uwakilishi. Tanzania inazo Balozi 35; Balozi Ndogo tatu; Vituo viwili
vya Biashara; na Konseli za Heshima 17 katika nchi mbalimbali. Hizi zote
zitahusika katika kuendeleza utekelezaji wa Diplomasia yetu ya Uchumi
na uwakilishi wa maslahi ya nchi yetu.
Aidha,
hadi sasa Mikutano ambayo tayari imefanyika na Balozi zetu kuwakilisha
ni pamoja na Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Madola (CHOGM)
unaoendelea nchini Malta na Mkutano wa Mawaziri wanaoshughulikia masuala
ya Habari wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
unaofanyika nchini Lesotho.
Aidha,
Wizara inatoa wito kwa Wizara, Idara na Taasisi za Serikali kuwasilisha
mapema taarifa za mikutano inayohusu sekta zao ili kutoa fursa kwa
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuzifanyia kazi kwa
wakati ili kuhakikisha ushiriki wa Tanzania unakuwa wenye tija kwa
taifa.
Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inaungana na wadau wengine
kumpongeza Mhe. Rais Magufuli kwa hatua anazozichukua za kuleta ufanisi
mkubwa wa kazi na kubana matumizi ili kuiwezesha Serikali kuwahudumia
wananchi kikamilifu.
Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
27 Novemba, 2015
Makumbusho ya Taifa yazindua maonyesho ya picha za matukio yanayohusu Albino nchini
Mratibu
wa Maonyesho ya Picha za Alibino kutoka Makumbusho ya Taifa Bibi. Flora
Vicent akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa
hafla ya uzinduzi wa maonyesho hayo jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho
hayo yanafanyika kuanzia tarehe 26 Novemba 2015 hadi tarehe 26 Januari
2016
Katibu
Mtendaji wa Bodi ya Filamu akifuatilia maelekezo ya Picha wakati hafla
ya uzinduzi wa mmaonyesho ya picha maonyesho ya Picha za matukio ya watu
wa jamii ya Albino zilizopigwa katika kambi ya kuwahudumia Albino ya
Kabanga.
Wakiwa katika picha ya pamoja.
KAMPENI YA ABIRIA PAZA SAUTI YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Mkuu
wa Kitengo cha Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu
Msaidizi wa Polisi (ASP), Abel Swai (kulia), akizungumza katika mkutano
na waandishi wa habari Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo, kuhusu kampeni ya
Abiria Paza Sauti iliyozinduliwa Dar es Salaam leo asubuhi.
Na Dotto Mwaibale
MKUU
wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi,
Mohamed Mpinga amesema kila mwananchi anawajibu kuzuia ajali za
barabarani badala ya kudhani kazi hiyo ni ya polisi pekee.
Mpinga
alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Abiria Paza Sauti
iliyozinduliwa Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam leo
asubuhi, ambao ulikwenda sanjari na mabalozi wa Usalama barabarani
(RSA) ambao walitoa elimu kwa abiria kuhusu usalama barabarani.
"Abiria
pazeni sauti pale mtakapoona dereva anaendesha gari lake ndivyo sivyo
na kama mtapaza sauti itasaidia kupunguza ajali hapa nchini" alisema
Kamanda Mpinga.
Waziri Mkuu Majaliwa azindua ununuzi wa hisa za Benki ya Walimu- MCB
MWILI WA MAWAZO KUAGWA KITAIFA KATIKA UWANJA WA FURAHISHA JIJINI MWANZA
Mkutano wa Naibu Katibu Mkuu Chadema Salum Mwalimu na Wanahabari Jijini Mwanza hii leo.
Naibu
Katibu Mkuu Chadema, Salum Mwalimu akionyesha kibali kilichotolewa na
Manispaa ya Ilemela ili kuruhusu ibada ya kumuaga Marehemu Mawazo
Kufanyika kesho katika Uwanja wa Furahisha
Mkutano wa Naibu Katibu Mkuu Chadema Salum Mwalimu na Wanahabari Jijini Mwanza hii leo (hawapo pichani).
Kushoto ni Ezekiel Wenje na Kulia ni Grace Kihwelu ambae ni Mbunge Viti Maalumu Chadema Mkoani Kilimanjaro
Singo
Kigaila Benson ambae ni Mkurugenzi wa Mafunzo Chadema (Kushoto) akiwa
na Peter Mekele ambae ni Mwenyekiti Chadema Kanda ya Ziwa Victoria
(Kulia)
Husna Amri Said ambae ni Mwenyekiti BAWACHA Wilayani Geita
Viongozi na Makada wa Chadema
Mkutano wa kutoa ratiba za kuuaga mwili wa Marehemu Mawazo kwa wanahabari Jijini Mwanza hii leo
Wanahabari.
Na:Binagi Media Group
Mwili wa aliekuwa
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Geita Marehemu
Alphonce Mawazo, kesho unatarajiwa kuagwa Jijini Mwanza kabla ya kusafirisha
kwenda Mkoani humo kwa ajili ya Mazishi.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Salum Mwalimu, amesema Marehemu Mawazo
ataagwa Kitaifa kwa taratibu za chama hicho, katika uwanja wa Furahisha Jijini
Mwanza.
Amesema ratiba hiyo itatanguliwa na ratiba ya kifamilia ya kuuaga
mwili huo, ambayo itafanyika asubuhi Nyegezi Jijini Mwanza ambako ni nyumbani
kwa Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mdogo wa Marehemu Mawazo hiyo ikiwa
ni baada ya mwili wake kutolewa katika Hospitali ya Rufaa Bugando
ulikohifadhiwa.
Mwalimu amebainisha kwamba mwili huo utasafirishwa hiyo kesho
kwenda Mkoani Geita kuanzia majira ya saa nane mchana ambapo wakazi wa Mkoa huo
pia watapata fursa ya kuuagwa kesho kutwa jumapili.
Ameeleza kwamba kuanzia majira ya saa mbili asubuhi, shughuli za
kuuaga mwili huo zitafanyika Kimkoa katika Uwanja wa Magereza Mjini Geita na
baadae kusafirisha kwenda Katoro ambapo wakazi wa Jimbo lake la Busanda
watapata fursa ya kuuaga mwili huo.
Mwalimu ametanabaisha kwamba, baada ya shughuli zote hizo
kukamilika, mazishi ya Marehemu Mawazo yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu
katika Kijiji cha Chikobe Jimbo la Busanda Mkoani Geita.
Shughuli zote hizo zinatarajiwa kuongozwa na Mwenyekiti wa Chadema
Taifa Freeman Mbowe, Viongozi waandamizi wa Chama hicho akiwemo Frederick
Sumaye, aliekuwa mgombea urais wa Ukawa Edward Lowasa, wabunge pamoja na makada
wa Chadema.
Ratiba za Mazishi ya Marehemu Mawazo ambae aliuawa Novemba 14
mwaka huu na watu wasiojulikana, zimejiri baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza
jana kuondoa zuio la Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza, lililokuwa zinazuia mwili
huo kuagwa Jijini Mwanza kutokana na hofu ya kiusalama pamoja na uwepo wa
mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo zuio hilo liliondolewa katika kesi
iliyofunguliwa na baba mlezi wa Mawazo, Mchungaji Charles Lugiko baada mvutano
mkali wa siku nne mahakamani hapo.
NHIF YAKAMILISHA UJENZI WA KITUO CHA KISASA CHA UCHUNGUZI NA MATIBABU KILICHOJENGWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mfuko wa NHIF, Michael Mhando akizungumza wakati wa makabidhiano ya kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma.
Mkurugenzi mtendaji kampuni ya ujenzi Tanzania Building Works Ltd, Mohamed Iqbal Moray(kushoto), akimkabidhi funguo za kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NHIF Michael Mhando.
Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na uwezeshaji wa mfuko wa NHIF, Deusdedit Rutazaa akizungumza wakati wa makabidhiano ya kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma
Wafanyakazi wa mfuko wa NHIF na wa Hospitali ya rufaa ya Dodoma wakishiriki makabidhiano ya kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma.
Jengo la ujenzi wa kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma
Sehemu ya jengo la ujenzi wa kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma
Sehemu ya jengo la ujenzi wa kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma
MFUKO wa Taifa
wa Bima ya afya(NHIF) umekamilisha ujenzi wa kituo cha
kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Dodoma ambacho kitasaidia kupunguza msongamano
wa wagonjwa katika hospitali hiyo.
Akizungumza
katika makabidhiano ya jengo hilo, Kaimu Mkurugenzi wa NHIF, Michael
Mhando, alisema kituo hicho kitakuwa cha kisasa na kitatoa huduma mbalimbali
ikiwemo huduma za CT-Scan na kitafunguliwa kabla ya mwezi januari mwakani ili
“NHIF umelipatia ufumbuzi
tatizo la msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kukamilisha
ujenzi wa jengo hili ambalo limegharimu kiasi cha sh. Bilioni sita ikiwa ni
pamoja na vifaa vya matibabu na samani,”alisema Mkurugenzi huyo.
Alisema
ujenzi wa huo umeanza tangu mwaka 2008 na litakuwa na uwezo wa kuchukua vitanda
34 vya
wagonjwa.
wagonjwa.
“Kituo hichi
kitakuwa na vyumba vya madaktari, maabara, upasuaji, chumba cha kutolea
dawa, mapokezi, chumba cha wagonjwa mahututi,
chumba cha dharura, mfumo wa miito ya wauguzi, na vifaa tiba vya kisasa,”alisema
Mhando
Alisema kitatoa
huduma kwa wanachama wa mfuko huo, wananchi wa Mkoa wa Dodoma na mikoa jirani.
SERIKALI YAKANUSHA KUHUSU HAZINA KUACHWA TUPU
Na Jovina Bujulu-Maelezo
Serikali
imekanusha taarifa zinazosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa
Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa amekomba
fedha hazina na kuiacha Serikali bila fungu lolote.
Hayo
yamesemwa jijini dare es salaam na Kamishina wa Bajeti kutoka Wizara ya
Fedha Bwa. John Cheyo huku akiwataka wananchi kupuuza habari hiyo kwani
hazina ukweli wowote.
“Hazina
inazo pesa za kutosha na tunajivunia kufanya uchaguzi wa mwaka huu,
kununua mashine za BVR kwa kutumia pesa za watanzania bila kutegemea
msaada wowote kutoka nje ya nchi na kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu
ya juu mwaka huu” alisema Bwa. Cheyo.
Pia
aliongeza kuwa serikali imeendelea kugharamia miradi mbalimbali ya
maendeleo ikiwemo ujenzi wa bomba la gesi ambalo limekamilika hivi
karibuni, vinu vya kuchakata gesi na ujenzi wa barabara nchini.
Aliendelea
kusema kwamba mfumo wa serikali wa bajeti unaiwezesha serikali kupanga
vipaumbele vya matumizi kulingana na bajeti ilivyopangwa ambapo fedha
zinazokusanywa kupitia mfuko mkuu wa serikali ndizo hutumika.
Bajeti
iliyoidhinishwa na Bunge kwa kipindi cha 2015-2016 ni shilingi Trilioni
22.5 na bajeti hiyo inatengenezewa mpango wa makusanyo na matumizi kwa
kulipia mishahara ya wafanyakazi na miradi mbalimbali iliyoidhinishwa.
Pia
katika matumizi mengine bajeti hiyo inalipia chakula cha wanafunzi,
mikopo ya wanafunzi elimu ya juu, ununuzi wa dawa na vifaa tiba na
chakula cha hifadhi ya taifa.
ROSE MUHANDO KUNOGESHA TAMASHA LA KUSHUKURU DIAMOND JUBILEE
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa matamasha ya muziki wa injili
nchini Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es
salaam wakati alipofafanua mambo mbalimbali kuhusu maandalizi ya tamasha
la kushukuru baada ya kufanyika na kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa
Tanzania salama salimini.
Msama
amesema maandalizi yanaendelea vizuri na amemtangaza rasmi mwimbaji
Rose Muhando kama mmoja wa waimbaji wa muziki wa injili watakaoshiriki
katika tamasha hilo, linalotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond
Jubilee Desemba 25 na kushirikisha waimbaji wa kimataifa kutoka nchi za
Afrika na Ulaya, ambapo ameongeza kwamba mazungumzo bado yanaendelea na
waimbaji wengine kutoka nje ya nchi.
Katika
picha katikati ni Mwimbaji wa muziki wa Injili Rose Muhando akishiriki
katika mkutano huo na kushoto ni William Kapawaga mmoja wa waratibu wa
Tamasha hilo kutoka Kampuni ya Msama Promotion.
Mwimbaji
wa muziki wa Injili Rose Muhando akiwaelezea waandishi wa habari jinsi
alivyojiandaa kutumbuiza katika tamasha hilo la kushukuru, Kulia ni
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama.
baadhi
ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakimsikiliza
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion wakati alipokuwa akizungumza
nao jijini Dar es salaam kuhusiana na Tamasha hilo.
Subscribe to:
Posts (Atom)