Mkuu
 wa Kitengo cha Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu
 Msaidizi wa Polisi (ASP), Abel Swai (kulia), akizungumza katika mkutano
 na waandishi wa habari Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo, kuhusu kampeni ya 
Abiria Paza Sauti iliyozinduliwa Dar es Salaam leo asubuhi.
Na Dotto Mwaibale
MKUU
 wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi, 
Mohamed Mpinga amesema kila mwananchi anawajibu kuzuia ajali za 
barabarani badala ya kudhani kazi hiyo ni ya polisi pekee.
Mpinga
 alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Abiria Paza Sauti 
iliyozinduliwa Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam leo 
asubuhi, ambao ulikwenda sanjari na mabalozi wa Usalama barabarani 
 (RSA) ambao walitoa elimu  kwa abiria kuhusu usalama barabarani.
"Abiria
 pazeni sauti pale mtakapoona dereva anaendesha gari lake ndivyo sivyo 
na kama mtapaza sauti itasaidia kupunguza ajali hapa nchini" alisema 
Kamanda Mpinga.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment