Mkurugenzi
 wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa matamasha ya muziki wa injili 
nchini Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es 
salaam wakati alipofafanua mambo mbalimbali kuhusu maandalizi ya tamasha
 la kushukuru baada ya kufanyika na  kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa 
Tanzania salama salimini.
Msama
 amesema maandalizi yanaendelea vizuri na amemtangaza rasmi mwimbaji 
Rose Muhando kama mmoja wa waimbaji wa muziki wa injili watakaoshiriki 
katika tamasha hilo,  linalotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond 
Jubilee Desemba 25 na kushirikisha waimbaji wa kimataifa kutoka nchi za 
Afrika na Ulaya, ambapo ameongeza kwamba mazungumzo bado yanaendelea na 
waimbaji wengine kutoka nje ya nchi.
Katika
 picha katikati ni Mwimbaji wa muziki wa Injili Rose Muhando akishiriki 
katika mkutano huo na kushoto ni William Kapawaga mmoja wa waratibu wa 
Tamasha hilo kutoka Kampuni ya Msama Promotion.
Mwimbaji
 wa muziki wa Injili Rose Muhando akiwaelezea waandishi wa habari jinsi 
alivyojiandaa kutumbuiza katika tamasha hilo la kushukuru, Kulia ni 
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama.
baadhi
 ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakimsikiliza 
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion wakati alipokuwa akizungumza 
nao jijini Dar es salaam kuhusiana na Tamasha hilo.
 
 
 
 
 
 



 
 
0 comments:
Post a Comment