Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 22, 2015

Rais Dkt. John Pombe Magufuli amsimamisha kazi Mkurugenzi wa (RAHCO),avunja mamlaka ya reli Tanzania (TRL)




magufuli1 (1)

Rais wa Jamhuri ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) Mhandisi Benhadard Tito ili kupisha uchunguzi wa kina kufuatia ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi uliobainika katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema, Rais Magufuli amefikia uamuzi huo baada ya kuitisha kikao cha wataalamu kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za serikali ambazo zinahusika katika utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya kati kwa kiwango cha kisasa yaani “Standard Gauge”
Amesema pamoja na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa RAHCO, Rais Magufuli ameivunja bodi ya RAHCO baada ya kujiridhisha kuwa haikutekeleza ipasavyo wajibu wake katika kusimamia mchakato wa zabuni hiyo na badala yake imeonekana kutetea kilichofanyika.
Aidha Rais Magufuli amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa RAHCO Mhandisi Benhadard Tito kutoa ushirikiano kwa vyombo vya serikali vitakavyofanya uchunguzi zaidi kuhusu mchakato wa Zabuni hiyo.
Pia ameiagiza Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya umma (PPRA) kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya kampuni za ukandarasi zilizopewa zabuni ya ujenzi huo endapo itathibitika kuwa zimeshiriki katika ukiukwaji wa sheria.

Pamoja na kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi Mkuu wa RAHCO Mhandisi Tito na Kuvunjwa kwa Bodi ya RAHACO, Rais Magufuli pia amemuagiza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU kuanza uchunguzi wa kina mara moja kuhusiana na sakaata hilo la ukikwaji wa sheria ya manunuzi katika zabuni ya ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kisasa yaani "Standard Gauge".
Katika hatua nyingine Balozi Sefue amesema, Rais Magufuli amevunja bodi ya Mamlaka ya Reli Tanzania (TRL) kutokana na kutoridhishwa na jinsi bodi hiyo ilivyoshughulikia ripoti ya uchunguzi wa mchakato wa ununuzi wa mabehewa ya treni.

HENNESSY'S 250 YEARS EXHIBITION AT OASIS BAR MASAKI


The owner of Oasis Bar and Lounge Nuru Mosha clarifying something to journalists at the The Hennessy 250's  Exhibitions.
Some pictures related to Hennessy
The Amazing Hennessy bottle
Some paints related to Hennessy 
The event was accompanied by live music
The Hennessy' s bar at Oasis Masaki
*************
By Staff Reporter
The four-day exhibition to mark the 250 years of Hennessy was launched in Dar es Salaam this Monday,  at Oasis Bar, Masaki and it has attracted many people including artists, socialites as well as other arts stakeholders.

The event was accompanied by a live music performance and involved artwork and limited edition bottles done by different artists, profiling the history and heritage of Hennessy.

Speaking with journalists at the Oasis Bar on Monday where the exhibition is taking place, the owner of Oasis Bar and Lounge Nuru Mosha clarified that, The Hennessy 250 Exhibitionis a multidisciplinary event in which the exhibition showcases the treasures of its heritage.

He added that it reflects the vision that Hennessy has always had of itself and the world around it, a taste for the avant-garde and the pull of distant horizons.

" This hybrid cultural event and exhibition at Oasis Wine Bar with accompanying music and live performances, is a reflection of the unique bond that Hennessy has always maintained with the art world" he added.

He also added that since the Hennessy family were early patrons of the arts and have always been close to artists themselves, the exhibition would of course involve the arts.

"This has given us reflections of the longevity and permanence of its products in limited editions with prestigious signatures and even here in Tanzania. Hennessy is very proud to support artistic activities" he said.

WAZIRI KITWANGA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA NIDA JIJINI DAR ES SALAAM

571
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akiwasili Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Kinondoni jijini Dar es Salaam na kupokewa na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu (kushoto). Waziri Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
544
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Brenda Joshua akimfafanulia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai), jinsi wanavyosajili taarifa mbalimbali za waombaji wa vitambulisho. Waziri Kitwanga alitembelea Kituo hicho cha Usajili na kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na NIDA, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na kulia kwa Abdulwakil ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
572
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiieleza jambo menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya NIDA, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo. Watatu kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, wapili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo, na watatu kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
573
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya NIDA, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo.  Watano kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, wanne kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo.

Watendaji wa Tanesco Wazidi Kubanwa Watakiwa Kukamilisha Miradi Kabla Ya Februari Mwakani.

x28
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kulia) akitoa maagizo ya kukamilika kwa mradi huo ifikapo february mwakani kwa Mkurugenzi Mwandamizi wa Miradi TANESCO Bw.Gregory Chegere (wa kwanza kushoto) alipofanya ziara yake leo katika mradi wa  Tanzania Energy Development Access Program (TEDAP) eneo la Mbagala Rangi Tatu,jijini Dar es Salaam,Mradi huo utasaidia kusambaza umeme wenye nguvu ya kutosha na unaotarajia kunufaisha zaidi ya wananchi elfu kumi wa eneo hilo,watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Paul Masanja.
x29
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (kushoto) akitoa maagizo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya SAE Power Lines Bw.Tahir Mehmood (wa kulia) anayejenga mradi wa TEDAP eneo la Kurasini jijini Dar es salaam kuhakikisha mpaka mwanzoni mwa mwakani awe amshafunga Transifoma katika eneo hilo la mradi ni baada ya kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wake katika mradi huo. 
x30
Mhandisi Mkuu wa Miradi TANESCO Bw. Frank Mashalo (wa kwanza kulia) akimweleza  Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa pili kushoto)kuhusu maendeleo ya mradi  TEDAP uliyopo maeneo ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam na (wa kwanza kushoto) ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Paul Masanja.
x31
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (kushoto) akisikiliza malalamiko ya  mmoja wa wateja wa huduma za TANESCO  Bw.Michael Sedyan, Mkazi wa Sinza,hii ni baada ya Naibu waziri kufanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Tanesco Magomeni leo jijini Dar es Salaam.
x32
Afisa Muendesha Mitambo kituo cha TANESCO Kipawa Bibi Zuhura Mmanyi (wa kwanza kulia)akimweleza Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kushoto) namna mitambo ya eneo hilo inavyofanya kazi na maeneo mitambo hiyo inayosambaza umeme ikiwemo eneo la Gongo la mboto,Kiwalani,Segerea,Chang’ombe na Buguruni leo jijiji Dar es Salaam Naibu waziri alipo fanya ziara yake katika ofisi hiyo (wapili kushoto ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Miradi TANESCO Bw.Gregory Chegere na wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Paul Masanja.
x33
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (wa kwanza kushoto) akitoa maagizo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya SAE Power Lines Bw.Stephen Joseph (wa kwanza kulia) anayejenga Mradi wa TEDAP eneo la Gongo la Mboto kuhakikisha umeme unaanza kuwaka katika mitambo hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi Desemba 2015 kwa kuwa kila kitu kimeshakamilika katika mradi huo na malipo yake tayari ameshamaliziwa kulipwa, (wapili kushoto) ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Miradi TANESCO Bw.Gregory Chegere.
x34
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani (kulia) akimsikiliza mmoja wa wateja wa Ofisi ya TANESCO Magomeni Bw.Mohamed Bago Mkazi wa Manzese alipokuwa akitoa kero yake kuhusu kusubiri zaidi ya masaa matatu kupatiwa huduma ya tatizo ya luku yake ambayo haiingizi umeme,hiyo ni baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Tanesco Magomeni.

RAIS MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA SPIKA WA BARAZA LA SENETI NA MJUMBE MAALUM WA RAIS WA JAMHURI YA BURUNDI,PIERRE NKURUNZINZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Ndugu Reverien Ndikuriyo, Spika wa Seneti na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Burundi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Ndugu Reverien Ndikuriyo, Spika wa Seneti na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Burundi.

MAJALIWA AKUTANA NA ASKOFU NGONYANI WA LINDI


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu wa Jimbo Katoliki la LindI Mhashamu, Anthony Ngonyani kwenye Ikulu ndogo ya Ruangwa Desemba 22, 2015.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kizungumza na Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi Mhashamu Anthony Ngonyani kwenye Ikulu ndogo ya Ruangwa Dasemba 22, 2015.

IGWUTA WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KAZI ZAKE


Na Zainabu Hamis wa Globu ya Jami.
CHAMA cha wafanyakazi wa viwanda na sekta mbalimbali(IGWUTA) champongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Joseph Magufuli (Pichani)kwa namna na jinsi anavyofanya kazi yake hasa ile ya kupambana na mafisadi na wanafiki.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Katibu Mkuu wa chama chama cha IGWUTA, Michael Kashamba amesema kuwa,Wamefurahishwa kwa  kumpata Rais Magufuli na wanatoa wito kwa Wafanyakazi wote hapa nchini kujitokeza na kumuunga mkono Rais wetu katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Aidha Kashamba ametoa tamko la kumpongeza Magufuli kuwa ni kiongozi asiyekuwa wa kawaida, Hana ubinafsi na anaweka maslahi ya nchi mbele huku akimfananisha kwa utendaji wa kazi zake ni kama Rais wa awamu ya kwanza Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Pia Kashamba amesema kuwa, Chama chao kinatoa huduma ya kuelimisha na kuhamasisha wanachama kutimiza wajibu wao wa kufanya kazi kwa bidii, nidhamu na uaminifu mkubwa.

Pia IGWUTA inatoa Huduma za utetezi kwa Wanachama dhidi ya uonevu wowote uliofanywa na baadhi ya waajiri hapa nchini.

MAJALIWA AKABIDHI JEZI NA MIPIRA


MJ1
Waziri kuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi seti moja ya jezi na mipira miwili nahodha wa timu ya mpira wa miguu ya  Super Mark ya kijiji cha Nabgulugai wilayani Ruagwa, Paulo Joseph baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo Desemba 21, 2015.
MJ2
Waziri kuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi seti moja ya jezi na mipira miwili nahodha wa timu ya mpira wa miguu ya Super Mark ya kijiji cha Nabgulugai wilayani Ruagwa, Issa Ngele baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo Desemba 21, 2015.
MJ3
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye kijiji cha Narungombe wilayani  Ruangwa Desemba 21, 2015

WAZIRI KITWANGA AKUTANA NA VIONGOZI WAKUU WA JESHI LA POLISI, WAWEKA MKAKATI WA KUKABILIANA NA UHALIFU NCHINI

NGA2
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akitoa taarifa mbalimbali za shughuli zinazofanywa na jeshi hilo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati), wakati Waziri huyo alipofanya ziara Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumza na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo, ambapo walikubaliana kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini.
NGA3
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini. Waziri Kitwanga aliwaambia waandishi wa habari kuwa, wamekubaliana na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini. Wapili kushoto meza kuu ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu.

 Wapili kulia meza kuu ni Naibu IGP, Abdulharam Kaniki. Kulia ni Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi hilo, Paul Chagonja. Kushoto meza kuu ni Kamishna wa Polisi Jamii nchini, Mussa Ali Mussa. Kushoto ni Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova.
NGA4
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati waliokaa), Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu (watatu kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini mara baada ya kikao chao kilichofanya katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Jeshi hilo kumalizika. Waziri Kitwanga alifanya mazungumzo na Viongozi hao na kukubaliana kuweka mikakati ya kupambana na uhalifu.
NGA5
Msafara wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ukiwasili katika lango Kuu la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi hilo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
NGA1
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu wakati alipokuwa anawasili Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi. Waziri Kitwanga alifanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo na kukubaliana kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 
Blogger Templates