Pages

Ads 468x60px

Tuesday, December 22, 2015

WAZIRI KITWANGA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA NIDA JIJINI DAR ES SALAAM

571
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akiwasili Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Kinondoni jijini Dar es Salaam na kupokewa na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu (kushoto). Waziri Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
544
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Brenda Joshua akimfafanulia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai), jinsi wanavyosajili taarifa mbalimbali za waombaji wa vitambulisho. Waziri Kitwanga alitembelea Kituo hicho cha Usajili na kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na NIDA, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na kulia kwa Abdulwakil ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
572
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiieleza jambo menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya NIDA, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo. Watatu kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, wapili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo, na watatu kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
573
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya NIDA, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo.  Watano kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, wanne kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates