Shabiki wa Msanii Vanessa Mdee akiwa kwenye pozi la Red Carpet wakati
 wa Tamasha la “Trust Divas Only” ambalo lilifanyika katika hoteli ya 
Malaika Beach Resort jijini Mwanza mwishoni mwa wiki. Tamasha hilo 
ambalo ni maalum kwa ajili ya akina dada ni mahususi kwa ajili ya utoaji
 elimu ya afya ya uzazi na maendeleo yao ya baadae.
Msanii wa Bongo fleva Vanessa Mdee, akipiga picha na baadhi ya 
mashabiki wake wakati wa Tamasha la “Divas only” ambalo ni mahusisi kwa 
ajili ya kuwaelimisha madiva mbalimbali kuhusu elimu ya afya ya uzazi. 
Tamasha hilo la mwisho lilifanyika katika ukumbi wa Malaika Beach Resort
 jijini Mwanza baada ya kuzunguka katika majiji ya Dodoma na Mbeya 
katika wiki zilizopita.
Msanii wa Bongo fleva Vanessa Mdee akiwa kwenye picha ya pamoja na 
wafanyakazi wa TRUST wakati wa Tamasha la “Divas only” ambalo ni 
mahusisi kwa ajili ya kuwaelimisha akina dada kuhusu elimu ya afya ya 
uzazi. Tamasha hilo lilifanyika katika ukumbi wa Malaika Beach Resort 
jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.
Wafanyakazi wa TRUST wanaohusika na mpango wa kuelimisha wasichana 
juu ya elimu ya uzazi wakiwa jukwaani tayari kwa kufungua Tamasha la 
“Divas Only” kwa kucheza muziki. Tamasha hilo lilifanyika katika ukumbi 
wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.
Madiva mbalimbali wakijiandikisha wakati wa ufunguzi wa Tamasha la
 “Divas Only”ambalo lilikuwa maalum kwa ajili ya kuwaelimisha akina dada
 juu ya afya ya uzazi na maendeleo yao ya baadae. Tamasha hilo ambalo 
lilipambwa vilivyo na burudani toka kwa Msanii Vanessa Mdee lilifanyika 
mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza.
Msanii
 wa Bongo fleva Vanessa Mdee akitumbuiza kwenye Tamasha la “Trust Divas 
Only” lililofanyika katika hoteli ya Malaika Beach Resort jijini Mwanza 
mwishoni mwa wiki. Tamasha hilo ni maalum kwa ajili ya kina dada na 
limekua likitoa elimu juu ya afya ya uzazi na maendeleo ya baadae ya 
madiva hao tokea uzinduzi wa mfululizo wa matamasha hayo jijini Dodoma 
wiki mbili zilizopita.
TAMASHA la “Trust Divas only” limefunga pazia lake rasmi usiku wa 
kuamkia leo katika ukumbi wa Malaika Beach resort uliopo pembezoni mwa 
ziwa Victoria jijini Mwanza. Wakazi na madiva wa mkoa huo walijitokeza 
kwa wingi kushuhudia Tamasha hilo la mwisho na la aina yake lakini 
kikubwa zaidi kupata elimu na hamasa juu ya uzazi wa mpango na mambo 
yanayowahusu wakina dada katika kupanga maendeleo yao ya baadae.
Aliyelipamba Tamasha hilo si mwingine bali ni diva wa nguvu na msanii
 wa kizazi kipya Vanessa Mdee ambaye tokea awali amekua akishirikiana na
 Trust katika mfululizo wa matamasha hayo yaliyoanza rasmi wiki mbili 
zilizopita jijini Dodoma.
Mara baada ya kupanda jukwaani na kuporomosha burudani ya nguvu 
Vanessa alionekana kushangiliwa kila kona na madiva hao waliokuwa 
wakiimba sambamba na msanii huyo ambae alifanikiwa kukata kiu ya madiva 
wengi wa mkoa huo waliojitokeza kwa wingi kushuhudia burudani yake.
Mfululizo wa matamasha hayo ya Trust ambayo ni chapa ya njia za 
kisasa za uzazi wa mpango zenye kuaminika pamoja na bidhaa na huduma za 
maisha na urembo zinazotengenezwa kwa ajili ya wanawake yamefikia tamati
 baada ya kuzunguka kwa muda wa wiki tatu kwenye miji mitatu tofauti ili
 kuhamasisha madiva mbalimbali wajipange kwa ajili ya mafanikio yao ya 
baadae. Trust ipo katika kumsaidia diva wakati wote wa safari hii.
“Ni furaha yangu kubwa kuwa tumeweza kukamilisha zoezi hili kwa 
ufanisi mkubwa tangu tulipozindua matamasha haya jijini Dodoma”… alisema
 Meneja Masoko wa Trust Sialouise Shayo.
Bi. Shayo aliongeza kuwa katika zoezi zima wamefanikiwa kuwafikia 
madiva lukuki katika mikoa yote mitatu waliyoitembelea ambapo kwa pamoja
 wameweza kufurahi, kuelimishana na kujifunza kutoka kwa wataalamu mambo
 mbalimbali zikiwemo njia nyingi bora za uzazi wa mpango kama njia ya 
kitanzi ambayo ni bora sana  na ina ufanisi wa zaidi ya asilimia 99.9.
Kama wewe ni Diva wa Trust ama unataka kujua Trust inahusu nini, 
Tutafute kupitia ofisi zetu zinazopatikana Dodoma, Mbeya na Mwanza au 
kwa kupitia tovuti yetu (trustlife.co.tz) na ututembelee leo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment