Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donan Mmbando akizungumza na 
waandishi wa habari hawapo pichani juu ya Mlipuko wa Ugonjwa wa 
kipindupindu uliopo sasa ulianza mnamo 15 Agosti 2015, katika Manispaa 
ya Kinondoni na baadae kusambaa katika Manispaa zote za Mkoa wa Dar es 
Salaam leo jijini Dar es Salaam.
  Waandishi  wa habari wakimsikiliza  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donan Mmbando, leo jijini Dar es Salaam
Wadau mbalimbali wakiwa katika mkutano huo leo  jijini Dar es Salaam
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MLIPUKO wa Ugonjwa wa kipindupindu umesambaa katika mikoa 14  na kufikia wagonjwa 7825 na vifo 106.
Akizungumza
 na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya 
Afya na Ustawi wa Jamii, Donan Mmbando amesema kati ya wagonjwa wote 
waliougua 3746 sawa na asilimia 67 wanatoka katika mkoa wa Dar es 
Salaam.
Amesema
 kuwa  Mikoa inayotoa taarifa ya kuwepo wagonjwa wapya ni Dar es Salaam,
 Morogoro, Pwani, Dodoma, Mwanza, Arusha, Mara, Singida na Tanga.
 Mmbando
 amesema kuwa  ugonjwa huo umeripotiwa katika mikoa mingine ya Tanzania 
ikiwa ni pamoja na Pwani, Singida, Mara, Arusha, Tanga, Mwanza, 
Shinyanga, Morogoro, Iringa, Kilimanjaro, Dodoma, Kigoma, Geita pamoja 
na Rukwa.
Aidha 
amesema hadi kufikia Novemba 8,2015  idadi ya wagonjwa waliokwisha 
kuripotiwa tangu mlipuko uanze hapa nchini ni 7825 na vifo 106 amabo ni 
asilimia 1.3 ya waliougua.
Amesema
 hatua walizozichukua kwa ugonjwa huo ni kutoa dawa, vifaa vya maabara 
na vifaa kinga kwa mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Morogoro.
Aliongeza
 kuwa  Wizara imepokea maombi kutoka mikoa ya Singida, Arusha, Tanga, 
Mwanza, Mara na Geita kati ya Oktoba 15 mwaka huu  na yanashughukuliwa 
na utawala, Kupima vipimo vya maabara na kufuatilia ubora wa vipimo 
kutoka katika mikoa iliyofanya uchunguzi na kuthibitisha uwepo wa 
ugonjwa huo, Kupeleka timu za watalaam kutoka ngazi ya Mkoa na Taifa 
kusaidiana na timu za Wilaya husika. 
Aidha 
tarehe 28 Oktoba 2015, Timu ya Kitaifa ilienda katika mikoa ya Tanga, na
 Singida na vilevile mkoa wa Manyara pia timu ilienda kwa ajili ya 
kufuatilia tarifa za kuwepo kwa ugonjwa wa kuhara na kutapika – taarifa 
ya timu hizi inakamilishwa na itawasilishwa.
Mmbando
 amesema hatua nyingine Kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya juu ya 
ufuatiliaji wa ugonjwa na utoaji wa matibabu ,Kutoa elimu ya kwa umma 
kupitia vyombo vya habari hususani radio na runinga. Aidha, mafunzo kwa 
waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini 
yametolewa, Kuandaa “Water safety plan” kwa kushirikisha wadau 
mbalimbali ikiwemo WHO, PSI, CDC, MSF, Redcross na USAID. Aidha mpango 
mkatati huu utajikita kwanza kwa jiji la Dar es salaam kwa kuanzia na 
hapo baadae itaenda katika mikoa mingine.
Amesema
 changamoto katika ugonjwa huo ni,Mwitikio hafifu wa jamii juu ya 
kukabiliana na ugonjwa huu,Jamii kutokuzingatia kanuni za afya na 
mazingira,Ushiriki mdogo wa sekta nyingine katika kupambana na ugonjwa 
huu,Ukosefu wa pesa za kuwalipa watumishi wa afya wanaohusika katika 
zoezi la kukabiliana na ugonjwa huu.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment