Mkalimani wa lugha ya alama 
akifafanua mazungumzo kwa alama kwa baadhi ya wajumbe wa Shirikisho la 
Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wakati wa  mkutano wa
 shirikisho hilo na Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu) Dk. Abdalla Possi 
(hayupo pichani), jana jioni (Jumatano, Desemba 16, 2015), katika ukumbi
 wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu (Sera,Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi 
Jenista Mhagama (Mb), (katikati) akimsikiliza  Mwenyekiti wa Shirikisho 
la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Amon Mpanju 
wakati shirikisho hilo  lilipo kutana na Naibu Waziri (Watu wenye 
Ulemavu) Dk. Abdalla Possi (wa kwanza kushoto), jana jioni (Jumatano, 
Desemba 16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, 
Jijini Dar es Salaam, (wa tatu kulia), Naibu Katibu Mkuu Ofisi  ya 
Waziri Mkuu, Bibi. Regina Kikuli.
Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu) 
Dk. Abdalla Possi, akiteta  jambo na mmoja wa wajumbe wa Shirikisho la 
Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) mara baada ya 
kukutana na wajumbe wa shirikisho hilo  jana jioni (Jumatano, Desemba 
16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar
 es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Shirikisho la
 Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wakifuatilia 
mazungumzo ya mkutano huo, wakati wa  mkutano wa shirikisho hilo na 
Naibu Waziri (Watu wenye Ulemavu) Dk. Abdalla Possi, jana jioni 
(Jumatano, Desemba 16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya 
Waziri Mkuu, Jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………….
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia, 
(Sera,Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi 
Jenista Mhagama (Mb), amelitaka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye 
Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) kuondoa tofauti zao ili kuweza 
kushirikiana na serikali ya awamu ya tano ambayo imedhamiria kuimarisha 
na kulinda haki za watu wenye ulemavu.
 
“Mnapaswa kuhakikisha kuwa wale wote wanaoleta tofauti zenu 
kuwashughulikieni mapema katika vikao vyenu ili muweze kushirikiana na 
sisi katika kuhakikisha mnapata haki ya kulindwa , kuheshimiwa na 
usalama. Tunataka nchi yetu baada ya miaka mitano iwe katika historia 
nzuri kwa kuwajali watu wenye ulemavu”. Amesema.
 
Ametoa wito huo wakati akizungumza na Shirikisho la Vyama vya 
Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) jana jioni (Jumatano, Desemba 
16, 2015), katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dar
 es Salaam.
 
Bibi Mhagama alisema: “Tunapaswa tusimuangushe Rais Magufuli kwa
 imani aliyoionesha kwenu na kuteua Naibu waziri anayeshughulikia 
masuala yanayowahusu ambayo yanaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu,” 
alisema.Awali akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa shirikisho 
hilo, Amon Mpanju pamoja na kumshukuru Waziri na Naibu Waziri 
anayeshughulikia (Watu wenye ulemavu) kwa kuitisha mkutano uliolenga 
kujadili vipaumbele vya watu wenye ulemavu nchini pamoja na nchi 
zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi alimuomba waziri huyo kuhairisha 
ili waweze kukamilisha uaiinishaji changamoto zao vizuri.
 
“Tunaomba mheshimiwa waziri utupatie muda zaidi tuweze ili 
tuweze kuainisha vizuri zaidi changamoto zetu ambazo naamini Naibu 
waziri mwenye dhamana ya kushughulikia watu wenye ulemavu amabye pia 
tunaimani naye sana ataweza kubaini masuala yanayotuhusu na kuweza 
kuyatekeleza katika majukumu yake” alisema.
 
Mkutano huo uliandaliwa na Naibu Waziri anayeshughulikia watu 
wenye Ulemavu Dk. Abdalla Possi, pia ulihudhuliwa na Katibu Mkuu Ofisi 
ya Waziri Mkuu aliye wakilishwa na Naibu wake, Bibi. Regina Kikuli na 
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri 
Mkuu, Obey Assery.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment