Bado tupo kwenye headlines za uchaguzi 2015 ambapo msanii mkongwe wa HipHop Tanzania Joseph Haule (Profesa Jay) ni mmoja wa wawashindi wa kiti cha ubunge kwenye uchaguzi huu akiwa amechukua jimbo la Mikumi Morogoro na anachosubiri kwa sasa ni kuingia bungeni.
Prof. ameongea na millardayo.com >>>‘Nawashukuru
 sana wananchi wa Mikumi kwa kuniamini na kunipa dhamana hii kubwa, 
watanzania wameniamini kwa sababu ya upeo mkubwa ambao Mungu 
amenipa, naamini sana katika umoja na mshikamano….! na ndiomaana 
nimekuwa nasisitiza hata katika kampeni zangu, lazima tushikamane watu 
wote wa vyama vyote na hata wasio na vyama ili kuikomboa Mikumi yetu ‘ –
‘Changamoto
 kubwa ni maji, elimu, miundo mbinu pamoja na ajira, nitaendelea 
kuwatumikia wananchi wangu kwasababu wao ndio wamenituma Dodoma, mimi 
kuwa mwanamuziki halitonizuia kuwawakilisha wananchi…. nitaendelea kuwa 
mwanamuziki na huwenda nikafanya muziki ule wa juu zaidi kwasababu 
nategemea kukutana na watu wa juu zaidi’– PROFESSOR J
Unaweza ukabonyeza play hapa chini kumsikiliza Professor Jay akizungumza kuhusu ushindi wake wa kiti cha Ubunge
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment