Pages

Ads 468x60px

Featured Posts

Wednesday, October 26, 2016

FULL TIME EFL CUP: MANCHESTER UNITED 1 v 0 MANCHESTER CITY, MATA AMBEBA MORINHO NYUMBANI OLD TRAFFORD!


English Football League Cup, Football League Cup - Fourth Round

VIKOSI:
Man Utd wanaoana XI:
De Gea, Valencia, Rojo, Blind, Shaw, Carrick, Ander Herrera, Mata, Pogba, Rashford, Ibrahimovic
Akiba: Depay, Lingard, Young, Romero, Fellaini, Schneiderlin, Darmian
Man City: Caballero, Maffeo, Otamendi, Kompany, Clichy, Garcia, Fernando, Sane, Jesus Navas, Iheanacho, Nolito
Akiba: Sterling, Gundogan, Aguero, Kolarov, Fernandinho, Adarabioyo, Gunn

Sunday, July 10, 2016

MATUMIZI YA TIKETI ZA KAWAIDA KATIKA MABASI YA UDART MWISHO JULAI 30 MWAKA HUU



Mabasi ya Shirika la Mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (UDART) yakiwa makao makuu ya Udart Jangwani jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (UDART), David Mgwassa (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu matumizi ya kadi badala ya tiketi. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Fedha wa Kampuni ya MaxMalipo walioingia ubia ma Udart katika mpango huo, Deogratius Lazari.
Mkuu wa Idara ya Fedha wa Kampuni ya MaxMalipo walioingia ubia ma Udart katika mpango huo, Deogratius Lazari (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
Meneja wa Uhusiano wa Udart, Deus Bugaywa (kushoto), akichangia jambo kwenye mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea

Na Dotto Mwaibale

SHIRIKA la Mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (UDART), imetangaza kaunzia Julai 30 mwaka huu kuwa ni mwisho wa matumizi ya tiketi za kawaida kwa abiria badala yake zitatumika kadi.

Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa UDART, David Mgwassa wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu matumizi ya kadi badala ya tiketi.

" Tiketi zitaendelea kutumiwa na wanafunzi lakini watu wengine wote watatumia kadi maalumu za kupandia mabasi yetu" alisema Mgwassa.

Alisema Udart imepunguza bei ya kadi hizo kutoka sh.4500 ya awali hadi kufikia sh.2000 ili kutoa fursa kwa kila mwananchi wa kuweza kuipata kadi hizo na kuzitumia.

Mgwassa alisema kadi ziliuzwa ni 55,000 na zilizobaki ni 150,000.

Mkuu wa idara ya Fedha wa Kampuni ya MaxMalipo walioingia ubia ma Udart katika mpango huo, Deogratius Lazari alisema wateja wataweza kulipia kadi hizo kupitia kwa mawakala wao waliopo katika vituo vyote vya udart na kwa njia ya mitandao yote ya simu.

India yaipatia Tanzania dola milioni 500 za Kimarekani kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo



India imeipatia Tanzania dola za Kimarekani milioni 500 kwa ajili ya miradi ya maendeleo ili kukuza ushirikiano wa kiuchumi baina nchi hizi mbili
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni wake, Waziri Mkuu wa India, Mheshimiwa Narendra Modi.
“Tunaishukuru India ambayo imeonyesha utayari wa kushirikiana nasi kiuchumi katika kilimo, TEHAMA, maji, Elimu, Afya na Ulinzi,” amesema Rais Magufuli.Rais Magufuli pia amesema ushirikiano wetu na India utatoa fursa kwa Tanzania kutimiza azma yake ya kuwa na uchumi wa viwanda kwani katika ziara hii Waziri Mkuu ameambatana na wafanyabiashara takriban 50 ambao wanaangalia fursa za kibiashara hapa nchini.

“India ni mdau wetu mkubwa wa  kibiashara  na uhusiano huu umekuwa ukikua kwani mauzo ya bidhaa za Tanzania nchini India yameongezaka toka thamani ya  dola za kimarekani milioni 187 mwaka 2005 hadi dola bilioni 1.29 mwaka 2015,”alisema Rais Magufuli.Aidha, Rais Magufuli amesema kuwa India itatoa fedha kwa nchi ya Tanzania kwa ajili ya kilimo cha Dengu ambayo ni fursa ya ajira kwa watanzania na kuinua kipato cha wananchi.

Rais Magufuli ameeleza kufurahishwa kwake na miradi ya India ikiwemo mradi unaojulikana kama Making India, mradi ambao unatumia malighafi zinazopatikana nchini na kutumia nguvu kazi ya nchini ambao utapunguza tatizo  la ajira katika Taifa la Tanzania.

Amebainisha kuwa India iko tayari kushirikiana na Tanzania kwenye miradi ya gesi ikizingatiwa kuwa aina mbali mbali za gesi zinazidi kugunduliwa hapa nchini. Katika suala la gesi India iko tayari kutoa utaalamu na wataalamu kwa ajili miradi ya gesi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa India , Mhe. Narendra Modi ameishukuru Tanzania kwa ukarimu alioupata hapa nchini na akaahidi kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya nchi hizi mbili.Amesema India italeta watu wake, utaalaamu na teknolojia yake kwa Tanzania, jambo ambalo litaongeza ushirikiano wa kiuchuni kati India na Tanzania.

Waziri Mkuu huyo amemaliza ziara yake ya kiserikali  ya siku mbili nchini na kuondoka kuendelea na ziara katika nchi nyingine za Ukanda wa Afrika Mashariki.

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi aondoka nchini baada ya kukamilisha ziara ya siku mbili nchini Tanzania




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Waziri Mkuu wa India Narendra Modi katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kabla ya kuondoka katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili nchini.

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akishukuru kabla ya kuondoka baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili nchini.
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akipungia mkono vikundi vya utamaduni vilivyokuwa vikitoa buradani katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili nchini.
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akiwa na watoto wa Kitanzania wenye asili ya kihindi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akiwa na watoto wa Kitanzania wenye asili ya kihindi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wafanyakazi wa kitengo cha mizigo katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JINIA jijini Dar es Salaam mara baada ya kumsindikiza mgeni wake Waziri Mkuu wa India Narendra Modi. PICHA NA IKULU


India na Tanzania zasaini mikataba ya miradi ya maendeleo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Waziri Mkuu wa India Narendra Modi katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.




Na. Immaculate Makilika- MAELEZO


Serikali ya India na Tanzania zimesaini mikataba ya miradi ya maendeleo katika sekta za maji, kilimo, viwanda, teknolojia ya habari na mawasiliano na afya katika kuimarisha mahusiano ya nchi hizo mbili ili kusaidia wananchi wake.


Mikataba hiyo imesainiwa leo, wakati Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi alipokua akifanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.


Mikataba wa kwanza uliosainiwa inahusisha mradi wa kusambaza maji katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.


Aidha, mkataba wa pili unahusisha mradi wa kusambaza maji Zanzibar ambao unatarajiwa kugharimu dola  za kimarekani milioni 92 ambapo mradi huo unatarajiwa kufikia miji 17 nchini na mkataba mwingine utahusisha mafunzo ya ufundi yatakayosaidia kuzalisha wataalamu mbalimbali.


“Lengo letu ni kusaidiana  na kuimarisha mahusianao yetu katika kukuza uchumi na kutengeneza fursa mpya za ajira kwa wananchi wetu” alisema Waziri Modi.


Waziri Modi aliongeza kuwa Serikali ya India itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuongeza wigo wa biashara na hatimaye kukuza uchumi wa nchi hizo.


Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli alisema Serikali India imekua na ushirikiano mzuri na Tanzania hasa katika masuala ya maendeleo ambapo imeweza kuwekeza nchini kiasi shilingi za Kimarekani dola bilioni 2.4 na kuzalisha  ajira 54,176.


Baadhi ya misaada iliyotolewa na Serikali ya India ni pamoja na  mashine ya vipimo vya ugonjwa wa kansa katika hospitali ya Bugando, itakayosaidia wakazi wa kanda ya ziwa na nchi nzima kwa ujumla pamoja na kuongeza na kuimarisha ushirikiano kati ya Shirika la viwanda vidogo vigodo la India kushirikiana na Tanzania katika kukuza viwanda vidogo na vya kati nchini.


Katika masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano, Serikali hiyo imeahidi kuleta wataalamu wao nchini Tanzania kwa lengo la kutengeneza program mbalimbali ili kuisaidia Tanzania katika masuala ya ulinzi wa mitandao pamoja na kutengeneza namna bora za ukusanyaji wa mapato ya nchi.


Katika masuala ya viwanda, Serikali ya India imeahidi kuanzisha viwanda vya kutengeneza dawa za binadamu  zitakazotibu   magonjwa mbalimbali ikiwemo malaria, figo na kisukari, ikiwa ni pamoja na kutengeneza vifaa tiba vitakavyotumika katika hospitali mbalimbali nchini kwa lengo la kupunguza gharama ya kununua vifaa hivyo nje ya nchi.


Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa nchi ya India ina uhitaji mkubwa wa mazao ya kilimo hasa jamii ya kunde hivyo akawataka wakulima kutumia fursa hiyo kuzalisha mazao hayo kwa wingi.


“India inauhitaji wa tani 200 za mazao jamii ya kunde, wakulima mnatakiwa kuzalisha mazao hayo kwa wingi kwa vile tayari kuna soko la uhakika, na tutahakikisha madalali hawatakuwepo ili mkulima asikandamizwe” alisema Rais Magufuli.


Katika sekta ya uwekezaji nchini, India ni nchi ya tatu kwa uwekezaji Tanzania ikifuatiwa na Uingereza pamoja na China.

Sentensi za RC Paul Makonda kuhusu ugeni wa Waziri Mkuu wa India…


Ni July 10, 2016 ambapo Tanzania imepata ugeni kutoka kwa Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi ambae kupitia ujio wake  ameahidi kusaidia katika utekelezaji wa Miradi ya Maji Dar es Salaam na Pwani, pia kusaidia kuendeleza sekta za Habari na Mawasiliano, Viwanda vidogo vidogo na Vyakati, Kilimo, Afya na masuala ya Usalama nchini, Ikulu  Dar es Salaam.
Baada ya Waziri hiyo kutoa ahadi hizo sasa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alisema….‘Imekuwa siku ndefu ila yenyemafanikio makubwa sana kwa Taifa langu na watanzania wote. Hongera sana Rais wetu, hongera pia Waziri Mkuu wa India’- RC Paul Makonda
Karibu tena Tanzania. Fursa zinazotafutwa na viongozi wetu naomba tuzitumie tusiishie kulalamika tu. Sasa kilimo cha mazao jamii ya kunde soko lipo tena la uhakika. kwa tani laki 1 tunaigiza dola Milioni 300, je kwa tani Milioni 7 si itakuwa dola bilioni kadhaa. Vijana tuchangamke India wanahitaji zaidi ya tani Milioni 7 ya mazao ya kunde,choroko na dengu- RC Paul Makonda

Friday, July 8, 2016

MKUU WA MKOA WA MBEYA AZINDUA KIVUKO CHA KITEPUTEPU WILAYANI RUNGWE NA KUWATAKA WANANCHI KUKITUNZA KITEPUTEPU HICHO..


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya  Mh.Amos Makalla amezindua Kivuko cha Kiteputepu kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya baada wananchi hao kupata shida ya kuvuka na kuhatarisha maisha kwa Kuvusha Watoto kwenda Shule kwa Kuogelea, kukosa huduma za Jamiii hasa Mto unapojaa Maji 

Tarehe 10 Juni Mhe Jenista Mhagama,Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha Maafa alifika kujionea changamoto hiyo na Ofisi yake ilichangia shilingi Milioni 10 na mnamo Tarehe 16 Juni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Halmashauri alipatikana Mkandarasi na alimpa Wiki 2 amalize Kazi na akahaidi Tarehe 8 Julai Kuwa tayari  na ahadi hiyo ameitimiza.

Gharama ya Ujenzi wa Kivuko ni Shilingi Milioni 58 na kufuatia Uzinduzi huo Wakazi wapatao 700 wa Kitongoji cha Kibundungulu wameanza kukitumia Kivuko hicho kwa kupita kwa Miguu na Pikipiki

Amewataka kukitunza Kivuko hicho kwani Ujenzi wa Daraja la kudumu unahitaji Fedha nyingi zaidi ya Bilioni 1.5 hivyo ni vema wakakitunza kivuko hicho kwasasa kwani kwa kiasi kikubwa kitapunguza tatizo la kuvuka na kwenda Vijiji vingine

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya katika hafra ya uzinduzi wa Kivuko cha Kiteputepu.
Muonekano wa kivuko hicho kwa juu.
Baadhi ya wacheza ngoma wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wakitoa burudani.


DOLE LA KATI LA MBUNGE MR SUGU LILILOSABABISHA AFUNGIWE BUNGENI



Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Mr Sugu' akiwaonesha wabunge wa CCM dole la kati Bungeni Dodoma hivi karibuni, kitendo ambacho kilitafsiliwa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwa ni tusi, hivyo kupewa adhabu ya kutohudhuria vikao kumi vya Bunge.
 
Blogger Templates