
Mkuu
 wa Mkoa wa Mbeya  Mh.Amos Makalla amezindua Kivuko cha Kiteputepu 
kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya baada wananchi hao kupata
 shida ya kuvuka na kuhatarisha maisha kwa Kuvusha Watoto kwenda Shule 
kwa Kuogelea, kukosa huduma za Jamiii hasa Mto unapojaa Maji 
Tarehe 10 Juni Mhe Jenista Mhagama,Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha Maafa alifika kujionea changamoto hiyo na Ofisi
 yake ilichangia shilingi Milioni 10 na mnamo Tarehe 16 Juni Mkuu wa 
Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Halmashauri alipatikana Mkandarasi na 
alimpa Wiki 2 amalize Kazi na akahaidi Tarehe 8 Julai Kuwa tayari  na 
ahadi hiyo ameitimiza.
Gharama
 ya Ujenzi wa Kivuko ni Shilingi Milioni 58 na kufuatia Uzinduzi huo 
Wakazi wapatao 700 wa Kitongoji cha Kibundungulu wameanza kukitumia 
Kivuko hicho kwa kupita kwa Miguu na Pikipiki
Amewataka
 kukitunza Kivuko hicho kwani Ujenzi wa Daraja la kudumu unahitaji Fedha
 nyingi zaidi ya Bilioni 1.5 hivyo ni vema wakakitunza kivuko hicho 
kwasasa kwani kwa kiasi kikubwa kitapunguza tatizo la kuvuka na kwenda 
Vijiji vingine

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya katika hafra ya uzinduzi wa Kivuko cha Kiteputepu.

Muonekano wa kivuko hicho kwa juu.

Baadhi ya wacheza ngoma wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wakitoa burudani.








 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment