Waziri
 wa Katiba na Sheria, Dk.Harrison Mwakyembe (Kushoto) akizungumza na 
waandishi wa habari wakati mkutano wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na 
Udhamini (RITA) juu ya utekelezaji wa agizo la kusitisha usajili bodi za
 wadhamini, Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa 
Sifuni Mchome.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa RITA, Emmy Hudson (Kulia) akitoa taarifa 
ya utekelezaji wa agizo la Waziri wa Katiba na Sheria Dk.Harrison 
Mwakyembe la kusitisha usajili wa bodi za wadhamini leo jijini Dar es 
Salaam. Kushoto ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk.Harrison Mwakyembe.  
Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni 
Mchome.
Sehemu ya wajumbe wa bodi wakimsikiliza Waziri wa Katiba na 
Sheria, Dk.Harrison Mwakyembe hayupo pichani leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe amesema kuwa 
wakati wa uchguzi mkuu kumekuwa na utitiri wa vikundi  ambavyo  
havionekani kazi zake  na mwisho wa siku vinaomba msamaha wa kodi.
Akizungumza leo na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, 
Mwakyembe  amesema kutokana na utitiri wa vikundi hivyo aliagiza Wakala 
wa Usajili ,Ufilisi na Udhamini (RITA),  kusitisha usajili wa vikundi 
hivyo na kufanya uchambuzi ni vikundi  ambavyo viko hai na vina vigezo 
kwa mujibu wa sheria.
Amesema kufanya usajili wa vikundi ambavyo kimsingi hafifanyi kazi
 iliyokusudiwa mwisho wa siku kuna uwezekano wa kusajili vikundi ambavyo
 ni hatarishi kwa taifa.
Aidha amesema kuwa kutokana na uchambuzi ambao umefanywa na 
kubainika kuwepo kwa vikundi 180 ambavyo vinatakiwa kufutwa kutokana na 
kushindwa kutimiza masharti ya bodi za udhamini.
Mwakyembe baada uchambuzi huo ameitaka RITA kuendelea na kazi 
usajili bodi za wadhamini kwa kufuata taratibu zote na kuwa na taarifa 
zao.
Nae Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa (RITA), Emmy Hudson amesekuwa katika 
uchambuzi huo kuna changamoto ambazo zilijitokeza ikiwa baadhi bodi za 
wadhamini kubadili ofisi pamoja na kubadili majina bila kufuata sharia.
Amesema kuwa bodi za wadhamini wengine wanamiliki mali bila kufuata sheria kwa mujibu sheria za RITA.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment