Taarifa ninayokusogezea ni ya David Kafulila aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kusini, tunafahamu ana kesi Mahakamani ya kupinga matokeo ya ubunge 2015 jimbo
 la Kigoma Kusini kesi ipo Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, taarifa 
ikufikie kuwa Kafulila baada ya kufika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma 
akasomewa kesi mpya ambayo anakiri hakuwa anaifahamu mwanzo kwenye 
sentensi zake; – David Kafulila
David Kafulila
‘Nilifikishwa mahakamani kwa kesi mpya ukiachilia kesi ya kwanza ya kupinga matokeo ya uchaguzi 2015
 jimbo la Kigoma kusini, awali nilikuwa nikijua ninakesi moja katika 
mahakama ya hakimu mkazi kigoma kwa madai kwamba nilimdhalilisha 
aliyekuwa mkuu wa wilaya Khadija Nyembo tangu mwaka 2013….nikiwa mahakamani nikapewa tena kesi nyingine ni kesi ya kuhamasisha wananchi wasichangie mchango wa maabara; – David Kafulila
‘Bado 
msimamo wagu utabaki palepale kwamba nitaendelea kupigania nchi yangu, 
kesi hizi zote katika mahakama ya hakimu mkazi Kigoma ukitazama hati za 
mashitaka yote ya Kafulila hapa Kigoma zimeandaliwa na kusainia na DPP makao makuu Dar es salam inawezekanaje;- Kafulila
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment