Aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Kahama Mjini, James Lembeli ameelezea kinachoendelea katika maisha yake ya kisiasa hasa baada ya kushindwa katika uchaguzi wa mwaka huu akiwa ndani ya chama chake kipya cha Chadema.
Akiongea
  katika taarifa rasmi kwa wananchi wa jimbo hilo, Lembeli amesema kuwa 
 hivi sasa atajikita zaidi katika shughuli za chama chake pamoja na  
shughuli alizokuwa akizifanya kabla ya kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Alisema
  kuwa ataendelea kufanya kazi zake na mashirika ya kimataifa kama 
mjumbe  wa Bodi mbalimbali. Pia, ataendelea kufanya kazi ya kusimamia 
radio  yake (Kahama FM) ambayo amedai kuwa taarifa zilizosambazwa kuwa 
ameiuza  kulipa deni la mkopo aliopewa kuendesha kampeni sio za kweli.
Pia,
  Lembeli amewashukuru wananchi waliojitokeza kumuunga mkono na kuahidi 
 kuendelea kushirikiana nao katika masuala ya maendeleo na ataendeelea  
kushirikiana nao kukamilisha miradi mbalimbali aliyokuwa ameanza  
kuitekeleza kwa juhudi zake binafsi.
Kadhalika,
  Lembeli amekanusha taarifa zilizokuwa zimesambazwa kuwa alikamatwa na 
 jeshi la polisi mara tu baada ya Jumanne Kishimba wa CCM kutangazwa 
kuwa  mshindi.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment