Jumuiya
 ya Wazanzibari Waishio Nchini Marekani (ZADIA), imekuwa ikifuatilia kwa
 karibu na makini zaidi zoezi zima la Uchaguzi Mkuu visiwani Zanzibar na
 Tanzania kwa ujumla. Kwa kiasi kikubwa mchakato wa uchaguzi ulifanyika 
kwa njia za amani na utulivu.
Hata hivyo ZADIA imeshtushwa mno na tamko la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mh. Jecha Salim Jecha la kutangaza kuufuta Uchaguzi Mkuu Zanzibar na matokeo yake.
Hata hivyo ZADIA imeshtushwa mno na tamko la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mh. Jecha Salim Jecha la kutangaza kuufuta Uchaguzi Mkuu Zanzibar na matokeo yake.
Ama
 kwa hakika kitendo hicho hakikuwa cha busara na kinapelekea kurudisha 
nyuma maendeleao ya demokrasia Zanzibar, na vilevile hakiashirii 
mustakbali mwema kwa nchi yetu tuipendayo. 
Wazanzibari wameelezea maoni na matakwa yao kwenye visanduku vya kupigia kura, na maoni na matakwa yao hayo yanapaswa kusikilizwa na kuheshimiwa.
Wazanzibari wameelezea maoni na matakwa yao kwenye visanduku vya kupigia kura, na maoni na matakwa yao hayo yanapaswa kusikilizwa na kuheshimiwa.
Kwa
 hivyo, ZADIA inatoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar, 
kumalizia mchakato mzima wa kuhesabu kura kwa majimbo yaliyobakia na 
kutoa matokeo ya mwisho ya Uchaguzi na kumtangaza mshindi ili kuiepusha 
Zanzibar yetu tuipendayo kuingia katika hali ya mtafaruku na mifarakano 
isiyokuwa na tija bali kuleta hasara.
ZADIA
 pia inaungana na jumuiya zote za kimataifa ambazo zimetoa msimamo wao 
juu ya uchaguzi wa Zanzibar, hasa ubalozi wa Marekani nchini Tanzania, 
ambao ni kiungo madhubuti kati ya Wazanzibari walioko Zanzibar na wenzao
 wanaoishi nchini Marekani. 
Aidha,
 tunapenda kumkumbusha Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dakta Ali Mohammed 
Shein kuwa Wazanzibari walimpa amana kubwa ya kuwaongoza, na kwa hivyo 
ni wajibu wake kuienzi amana hiyo kwa kuchukuwa hatua za kiungwana za 
kuitoa Zanzibar kwenye mgando huu wa kisiasa. Hali hii iliyopo sasa 
inaleta wasiwasi miongoni mwa raia na imekua ikiathiri maisha yao ya 
kila siku, na ikiachwa kuendelea huenda ikaathiri pia mustakbali maisha 
yao kwa jumla.
ZADIA
 pia inamtolea wito Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri 
Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kutumia mamlaka yake 
aliyonayo kuhakikisha Zanzibar inatoka kwenye mkwamo huu wa kisiasa na 
kwamba anaondoka madarakani akiiacha Zanzibar ikiwa katika hali ya amani
 na utulivu. Kwa kufanya hivyo atauthibitishia ulimwengu kuwa kweli 
Tanzania ni kisima cha amani.
Na
 mwisho tunawaomba Wazanzibari, wapenzi wa Zanzibar, na Watanzania wote 
kwa ujumla popote pale walipo, wajitahidi kufanya mawasiliano na Jumuiya
 nyengine za Kimataifa ili ziingilie kati suala hili kabla nchi yetu 
haijaingia kwenye mtafaruku mkubwa wa kisiasa na kijamii na hata 
kupelekea kuhatarisha amani ya nchi yetu.
Mungu Ibariki, Zanzibar.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment