Rais Dk.Jakaya Kikiwete akizundua kampuni ya Soko la Bidhaa  katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Serena jijini Dar es Salaam.
Rais Dk.Jakaya Kikwete akiwa 
katika picha ya pamoja na Menejimenti na Bodi ya Kampuni ya Soko la 
Bidhaa wakati wa uzinduzi wa kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Rais Dk.Jakaya Kikwete akizungumza
 wakati uzinduzi wa Kampuni ya Soko la Bidhaa iliyofanyika katikza 
ukumbi wa Serena jijini Dar es Salaam Oktoba 30, 2015.
Waziri wa Fedha na Uchumi,Saada Mkuya akizungumza na wakati uzinduzi wa kampuni ya Soko la bidhaa  jijini Dar es Salaam.
Sehemu wataalam mbalimbali wakiwa wamekekti katika uzinduzi wa Kampuni ya Soko la Bidhaa  jijini Dar es Salaam.
Rais Dk.Jakaya Kikwete amesema kuanza kwa kampuni ya soko la 
bidhaa kutasaidia wakulima kupata soko la uhakika na kukuza uchumi 
pamoja na kupata bima katika kilimo.
 
Hayo ameyasema leo wakati uzinduzi wa Kampuni ya soko la bidhaa 
jijini Dar es Salaam,Dk.Kikwete amesema wakulima wamekuwa wakilima 
lakini masoko yao hayana uhakika na kilimo hakina tija.
 
Amesema kuwa mfumo utasaidia wakulima kupata bei ya uhakika wa 
kuuza mazao yao na wanunuzi kufahamu bei ya soko la bidhaa 
wanayoihitaji.
Dk.Kikwete ameitaka watu wanaofanya kazi kuwa waaminifu katika 
kuweza kuwafanya wakulima wanufaike na soko hilo kwa kuwaletea maendeleo
 ya kuendeleza na kuachana na kutafuta masoko ambayo mwisho wa siku 
wanauza kwa hasara.
 
Aidha amesema soko la bidhaa litawaondolea wakulima ukopwaji 
ambao umekuwa ukiwakatisha tamaa na kushindwa kuendeleza kilimo chenye 
tija.
Amesema wakulima wamekuwa wakifanya kazi zao za kilimo wakiwa na
 changamoto kubwa ya kukosa soko la uhakika na kufanya mazao kununuliwa 
na watu wachache kwa bei ya chini.
 
Dk.Kikwete amesema wakulima wakiwa wana soko la uhakika 
kutafanya waweze kuingia katika bima kutokana na kilimo kuonyesha mwanga
 katika sekta hiyo.Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Soko la Bidhaa (TMX),Nasama Masinda 
amesema kuwa soko hilo wataanzia mazao ya Ufuta,Korosho pamoja na mpunga
 .
 
Amesema wamejipanga katika kuhakikisha wanaweka uwazi wa soko 
katika bidhaa hizo kwa wanunuzi na wauzaji kuwa na bei inayoendana na 
soko.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment