Pages

Ads 468x60px

Saturday, November 14, 2015

KAMPUNI YA NIKO INSURANCE LIMITED YABADILI JINA NA KUWA SANLAM GENERAL INSURENCE


 Afisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Insuarence Ndugu Manasseh Kawaloka  Akitoa Hotuba yake Kwenye halfa ya Kampuni ya NIKO Insuarence Limited Ilipobadili Jina na kuwa Sanlam General Insuarence.
Kampuni ya Bima Niko limited Imebadili jina na kuwa Sanlam General Insuarence Limited.

Mabadiliko hayo yanalenga Kupanua Wigo Na kuimarisha uwepo wake Nchini Tanzania na Afrika Mashariki  kwa Jumla.Sanlam General Insuarence Itaendelea Kutoa Huduma Mbalimbali za BimaKwa Wateja Binafsi na Mashirika Nchini Tanzania.Huduma za Sanlam General Insuarence  ni Pamoja na za Biashara na Binafsi kama vile Magari,Moto Na Nyinginezo.
   Sanlam General Insuarence  Yenye Makao Makuu yake Nchini Afrika KusiniInamiliki 46%ya Hisa za Niko.Kupitia Kampuni yake Tanzu ya Masoko yanayokua yaani Sanlam Emerging Markerts..
Picha  ya Viongozo wa Kampuni ya Sanlan Pamoja na NIKO Insuarence wakiwa wameshikana mikono Mara baada ya Uzinduzi wa Sanlam General Insuarence.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Insuarence Ndugu Manasseh Kawaloka Alisema Kuwa Sanlam Group ni Kampuni yenye Heshima Kubwa,Hivyo Mabadiliko ya NIKO Insuarence Kuwa Sanlam General Insuarence  Utaleta Ufanisi wa Hali ya Juu Pamoja Utendaji wa Kibiashara Kwa Kampuni Hiyo.Akieleza zaidi alisema Watanzania  sasa watapata nafasi zaidi ya Kupata Aina mbalimbali za Bidhaa za Bima Zenye ubunifu kufidia Majanga Binafsinna ya Kibiashara .
Kampuni ya Iliyobadili Jina Sanlam General Insuarence  Inatoa Huduma Mbalimbali za Bima Katika Wigo Mpana Kwa Wateja  Binafsi Pamoja na Mashirika  Nchini Tanzania .Huduma Zitolewazo na Kampuni ya Bima ya Sanlam General Insuarence  Zinalenga Biashara na Watu Binafsi Kama Magari ,Moto ,Uhandisi pamoja na Bima Maalum.Kabla ya Kubadili Jina Kampuni ya NIKO Insuarence Imekuwa Ikitoa Huduma Nchini Tangu Mwaka 2005.
Ndugu Josep Mungai Mkurugenzi Mtendaji wa Sanlam General Insuarence Akitoa Hotuba yake wakati wa Uzinduzi huo.
Mabadiliko ya NIKO Insuarence Limited kuwa Sanlam General Insuarence  Yanafuatia Mabadiliko ya Kampuni ya African Life Assuarence ya Tanzania na Kuwa Sanlam Life Insuarence.Sanlam General Insuarence  Inatoa utaalamu na Uzoefu wa Hali ya Juu kwa Wateja wake Pamoja na Wadua wengine wanaofanya kazi na Kampuni hiyo.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates