Katika
 kupambana na wimbi la kupunguza umaskini hapa nchini, kampuni ya 
Mawasiliano ya Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa “Airtel FURSA 
Tunakuwezesha” unaendelea kutoa mafunzo ya biashara ya ujasiriamali kwa 
vijana wenye lengo la kuwawezesha na kuwainua vijana hapa nchini .
Mafunzo
 hayo ya biashara ambayo yamekuwa yakiendeshwa hapa nchini katika mikoa 
mbali mbali , wiki ijayo yatafanyika Dar Live  Mbagala Kuu karibu na Big
 Bon  siku ya Jumanne tarehe 15 ili kuwawezesha vijana kuweza 
kukabiliana na wimbi hili gumu la kuendesha biashara na kuweza kukidhi 
mahitaji yao ya kila siku na kuweza kuinua uchumi wa nchi hii.
Akizungumzia
 kuhusu mafunzo hayo ambayo yamekuwa yakiendelea hapa nchini, Meneja 
huduma kwa jamii  wa Airtel , bi Hwa Bayumi, alisema “mafunzo haya 
yanalengo la kuwasaidia vijana wenye umri kati ya miaka 18- 24 ambao 
wanakiu ya kujikwamua na umasikini. Vile vile “Airtel FURSA 
Tunakuwezesha” Airtel inawawezesha vijana kwa kuwapatia elimu ya 
biashara na nyenzo za kuimarisha biashara zao.
Hivyo
 basi tunapenda kuwakaribisha vijana wote waishio jijini Dar Es Salaam 
kuweza kuhudhuria mafunzo haya ambayo yatatolewa bure kabisa bila 
gharama yoyote. Ili kijana aweze kushiriki  anatakiwa kufika pale Dar 
Live siku ya jumanne tarehe 15 kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi 
jioni.
Vile
 vile ili kijana kushiriki au kufaidika na mpango wa Airtel Fursa 
atatakiwa kutuma ujumbe mfupi kwenda kwa namba 15626 na kuweka maelezo 
yafuatayo:- Jina, Umri, aina ya biashara na eneo. 
Pia
 wanaweza kutuma maombi yao kwa kupitia barua pepe 
airtelfursa@tz.airtel.com ambapo watatakiwa kutuma jina kamili, umri, na
 aina ya biashara. Maelezo kuhusu program ya Airtel FURSA pia 
yanapatikana kwenye tovuti ya Airtel www.airteltanzania.com> 
aliongeza, Bayumi.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment