Pages

Ads 468x60px

Friday, December 4, 2015

BENKI YA DCB YATOA DAWA ZA MAJI KATIKA KUPAMBANA NA UGONJWA WA KIPINDUPINDU

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya DCB, Balozi Paul Rupia akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki sehemu ya katoni 58 za dawa za maji (Water Guard) kuajili ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu  leo katika  katika a Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, SaidMeck Sadiki akizungumza na watendaji wa Manispaa ya Kinondoni (hawapo pichani) juu ya kusimamia usafi wakati makadhibiano ya dawa za maji katoni 58 ilifanyika leo Katika viwanja vya Manispaa hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya DCB, Balozi Paul Rupia akimukabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki sehemu ya katoni 58 za dawa za maji (Water Guard) kuajili ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu  leo katika  katika a Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
MKUU wa Mkoa wa Dar es  Salaam,Said Meck Sadiki amewataka watendaji wa Manispaa ya Kinondoni kusimamia kikamilifu usafi katika kupambana na ugonjwa wa kipindupindu.
Meck Sadiki ameyasema hayo  wakati akikabidhiwa dawa za maji katoni 58 zenye thamani ya Sh. Milioni Tano (5) zilizotolewa na Baenki ya DCB ,amesema umefika wakati wa kutofumbia macho watu ambao hawatimizi wajibu wao katika suala la kufanya usafi.
Amesema watendaji wote ni lazima wawajibike katika kusimamia suala la usafi kwani kinondoni ndio ilikuwa ya kwanza kuwa na mgonjwa wa kipindupindu hivyo ni lazima kuwa ya kwanza ya kutokuwa na ugonjwa huo katika Manispaa ya Kinondoni.
Aidha amewataka watu kufuata ushauri wa watendaji  katika masualanya afya kutokana na kuwepo kwa magonjwa ya milipuko nambayo yanatokana na uchafu katika mitaa mbalimbali katika manispaa hiyo.Meck Sadiki amesema Benki ya DCB imetoa dawa ya maji kutokana na kutambua watu wanaogua wanamchango katika taifa pamoja na benki .
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya DCB, Balozi Paul Rupia amesema kuwa kutoa dawa hizo ni kutokana na kutambua wanaougua ni watu ambao wanazalisha hivyo wanawajibu kutoa msaada huo kadri ya uwezo wao.
Rupia amesema benki itaendelea kushirikiana na serikali katika masuala mbalimbali yanayohusu jamii kuweza kwenda sambasamba na serikali katika kutatua changamoto kwa namna moja au nyingine.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates