Waziri
 Mkuu, Kassim Majliwa akikagua bandari ya Dar es salaam  Desemba 3, 2015
 ambako alikwenda kupata ukweli kuhusu makontena 2,431 yaliyopitia 
kwenye bandari hiyo bila kulipiwa kodi ya serikali.  
 Waziri
 Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mfumo wa kukagua makontena bandarini 
kwa kutumia scaner huku akipata maelzo kutoka kwa Ofisa wa forodha, 
January Shauri wakati alipotembelea bandari ya Dar es salaam Desemba 3, 
2015  kutaka kujua ukweli wa tuhuma za makontena 2431 yaliyopita 
bandarini hapo bila kulipiwa kodi ya serikali. 
 Waziri
 Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu utoaji bili za kulipia 
kodi za serikali kwa watumiaji wa bandari ya Dar es salaam kutoka kwa 
ofisa mwandamizi wa masuala ya fedha , Bw. Sartho Mbuya wakati 
alipotembelea bandari hiyo  Desemba 3, 2015 kutaka kujua ukweli wa 
tuhuma za makontena 2431 yaliyopita bandarini hapo bila kulipiwa kodi za
 serikali. 
 Waziri
 Mkuu, Kassim Majaliwa akimwonyesha Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es 
salaam, Bw. Abel Mhanga (kulia) orodha ya makontena 2,431 yaliyopitia 
kwenye banda ya Dar es salaam bila kulipiwa kodi wakati alipofanya ziara
 kwenye bandari hiyo Desemba ,3, 2015. 
 Waziri
 Mkuu,  Kassim Majliwa  akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika 
la Reli nchini TRL wakati alipotembelea stesheni ya Dar es salaam 
kukagua uendeshaji wa Shirika hilo Desemba 3, 2015. 
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akitembelea steheni ya reli ya Dar es salaam Desemba 3, 2015.
WAZIRI MKUU ATINGA TENA BANDARINI NA TRL
*Akuta makontena 2,431 yametoka bila kulipiwa ushuru
*Ataka majina yaletwe ofisini leo saa 11 jioni
*Atoa wiki wiki moja kwa mfumo wa malipo kubadilishwa
*Akagua mabehewa, awaweka kiporo TRL
WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa amefanya ziara nyingine ya kushtukiza bandarini na
 kukagua mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo na utozaji wa malipo baada 
ya kupewa taarifa kwamba kuna makontena 2,431 yametolewa bila kulipiwa 
ushuru.
Waziri
 Mkuu alisema kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa bandari ya kuanzia 
Machi hadi Septemba 2014, makontena hayo yalipita bila kulipiwa kodi 
kupitia bandari kavu nne (ICDs) ambazo ni JEFAG, DICD, PMM na AZAM.
Kwa
 mujibu wa taarifa hiyo, ni watumishi 10 tu ambao wamesimamishwa kazi 
kutokana na makosa hayo. “Mmeamua kuwasimamisha kazi watu wadogo na 
kuwaacha wakubwa wanaendelea na kazi. Hatuwezi kuendelea kuikosesha 
Serikali mapato namna hii,” alisema Waziri Mkuu.
Waziri
 Mkuu amemtaka Kaimu Meneja wa Bandari, Bw. Hebel Mhanga amletee ofisini
 majina ya watumishi wote waliohusika na ukwepaji kodi huo ifikapo leo 
saa 11 jioni. Pia amempa Meneja huyo wiki moja kuhakikisha kuwa mamlaka 
hiyo inabadilisha mfumo wa utozaji malipo kutoka kwenye billing system 
na badala yake kuweka mfumo wa malipo wa kielektroniki (e-payment).
Ametoa
 agizo hilo leo (Alhamisi, Desemba 3, 2015), wakati akikagua idara 
mbalimbali za mamlaka ya bandari na kuona ukaguzi wa mizigo 
unavyofanyika kwa kutumia scanners. Akiwa kwenye chumba cha scanner 
mojawapo, Waziri Mkuu alikuta manifest moja ikisema kontena limejaa 
diapers lakini picha ya kwenye kompyuta ya scanner ilionyesha kuwa ndani
 ya kontena hilo kuna vitu kama vifaa vya umeme.
Kwa
 mujibu wa Kaimu Meneja Bandari upande wa Mamlaka ya Mapato Tanzania 
(TRA), Bw. Ben Usaje ambaye pia ni msimamizi wa kitengo cha scanner, 
inapobainika taarifa kama hiyo inapaswa itumwe kwa wenye ICDs ili 
wafanye ukaguzi kwa kulifungua kontena ili kuhakikisha mali zilizomo 
ndizo zilizoandikishwa kwenye manifest.
Katika
 hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza 
kwenye ofisi za Shirika la Reli (TRL) na kukagua mabehewa yaliyokuwepo 
kisha akazungumza na baadhi ya wafanyakazi waliokuwepo kwenye stesheni 
hiyo ambako alibaini madudu kwenye malipo ya mishahara na makato ya 
michango ya wafanyakazi.
Akizungumza
 na Mkurugenzi Mkuu TRL, Mhandisi Elias Mshana, Waziri Mkuu alisema 
amefika kwenye shirika hilo ili kujifunza utendaji wao kazi lakini anazo
 taarifa za wao kupewa fedha na Serikali kiasi cha sh. bilioni 13.5/- 
ili waendeleze miundombinu ya reli lakini hawakufanya hivyo. “Nia ya 
kuwapa fedha hizo ilikuwa ni kuboresha miradi ili muweze kujiendesha 
kibiashara lakini nyie mkaamua kujilipa wenyewe,” alisema.
“Ninazo
 taarifa kuwa baada ya hapo, mlikopa sh. bilioni 3 kutoka benki ya TIB 
ili kuendesha miradi ya shirika lakini badala ya kufanya miradi, fedha 
hizo mkaamua nazo kujilipa mishahara. Sasa sijui mnarudishaje huo mkopo 
wakati hakuna mradi wowote uliofanyika,” alihoji bila kupata majibu.
Alipoulizwa
 wafanyakazi wana matatizo gani hapo TRL, Katibu wa TRAWU, Bw. Boaz 
Nyakeke alisema wanadai malimbikizo ya makato yao kwenye mifuko ya 
pensheni, malimbikizo ya makato kwenye SACCOS na malimbikizo ya kuanzia 
Julai – Novemba 2014.
Waziri
 Mkuu kwa upande wake alimtaka Mhandisi Mshana asimamie uboreshaji 
huduma za usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam ili hata mabasi 
ya mwendo kasi yatakapoanza wananchi waweze kuwa na uhuru wa kuchagua 
aina ya usafiri wautakao.
“Tunataka
 kujenga yadi kubwa nje ya mji ili watu wenye magari wawe wanayaacha 
huko na kutumia usafiri wa treni au DART kuja mjini kama njia mojawapo 
ya kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam,” alisema.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
ALHAMISI, DESEMBA 3, 2015.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment