Waziri
 Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa (Kulia) 
akimkabidhi kombe Meneja masoko wa kampuni ya sukari ya Kilombero 
Ephraim Mafuru baada ya kuibuka washindi wa tatu wa Jumla katika tuzo za
 muajiri bora wa mwaka zilizo andaliwa na chama cha waajiri Tanzania 
(ATE). Hafla hiyo ilifanyika Dar-es-Salaam, mwishoni mwa wiki. 
Kampuni
 ya Kilombero Sugar Ltd imesema kuwa tuzo za Mwajiri Bora zinazotolewa 
na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), zinachangia kwa kiasi kikubwa 
kuleta hamasa kwa waajiri na kupelekea kutoa huduma nzuri kwa 
wafanyakazi. 
Akizungumzia
 tuzo hizo zinazotolewa kila mwaka, Meneja Rasilimali watu wa Kilombero 
Sugar Beda Marwa Chacha amesema kuwa shindano hilo linasaidia kwa kiasi 
kikubwa kuwafanya wajiri kutimiza majukumu yao ili kuweza kujinyakulia 
tuzo.
“Napenda
 kuwaomba waajiri wenzangu kushirikiana na ATE ili kuwawezesha kuboresha
 tuzo hizo. Tutambue kwamba sisi ndio muhimili mkubwa wa kuweza 
kuwafanya wao waendelee kuwepo,” alisema Beda ambaye kampuni yake 
imekuwa imefanikiwa kuwa mshindi wa tatu wa jumla.Amesema kuwa kadri 
wanavyoshiriki wanaendelea kujifunza mambo mengi kwa waajiri wenzao na 
hivyo kuendelea kufanya maboresho na kuwaasa ATE kuendelea kupanua wigo 
wa mashindano hayo.
Aliwaomba
 wanachama wenza kuhakikisha wanaendelea kutoa michango ili kukifanya 
chama kiendelee kuwepo  na kusaidia kuwapa changamoto waajiri.Alisema 
kuwa Kampuni ya Kilombero Sugar imefanikiwa kupata tuzo kwa utoaji 
huduma bora kwa  wafanyakazi wake, juhudi za kuzuia maambukizi ya virusi
 vya UKIMWI, utoaji huduma bora za maendeleo ya jamii na vilevile 
ushirikiano bora kwa wafanyazi pindi wawapo kazini.
Tuzo 
hizo zilitolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jijini Dar es Salaam 
mwishoni mwa wiki. Baada ya kukabidhiwa tuzo, Mkurugenzi wa Masoko wa 
Kampuni ya Sukari ya Kilombero Ephraim Mafuru alisema:  “Tumekuwa karibu
 kwenye kila kinyang’anyiro lakini katika sehemu hizi zote tumekuwa bora
 sana”.
Katika
 kampuni hiyo Serikali inamiliki asilimia 20 ya hisa zote, Kilombero 
Sugar inamiliki asilimia 55 ya hisa zote za Kampuni (hisa kubwa kuliko 
zote), asilimia 25 inamilikiwa na ED&F Man, kundi ambalo makazi yake
 yako jijini London. Kampuni ya Sukari Kilombero inatoa ajira za kudumu 
kwa wafanyakazi  zaidi ya 4000. 
Ikiwa 
kama moja ya makampuni yanayotoa huduma bora zaidi za kijamii, kampuni 
imejenga hospitali iliyogharimu kiasi cha shilingi milioni 700 ambayo 
hutoa huduma zake bure kabisa kwa wakazi wa eneo hilo.Vilevile kampuni 
hiyo imejenga shule ya sekondari ambayo inachukua wanafunzi kutoka pande
 zote za nchi, ujenzi wa mabweni, miradi ya maji pamoja na vyoo vya 
shule.
Moja 
ya vitu vinavyounda Kampuni ya Sukari ya Kilombero ni mashamba makubwa 
kwa ajili ya kilimo na viwanda cha sukari vya Msolwa na Ruembe vilivyopo
 karibu na Mto Ruaha Mkuu ambao umeunganishwa na daraja dogo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment