HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) inafunga mashine nyingine ya CT- Scan ambayo inategemewa kuanza kutoa huduma kesho mchana.
"Hivyo
 kufikia jumatatu ijayo Hospitali hiyo itakua na mashine mbili za 
CT-Scan ambazo zitakua zinafanya kazi hatua ambayo itaboresha zaidi 
utoaji wa huduma kwa wagonjwa ambao wanatakiwa kupimwa kwa kutumia 
mashine hiyo," amesema Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia , 
Watoto na Wazee Ummy Mwalimu.
Waziri
 wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Watoto na Wazee Ummy Mwalimu 
ameyasema hayo leo wakati alipotembelea mashine za CT-Scan na MRI katika
 hospitali hiyo.
Pamoja
 na mambo mengine Waziri huyo ameshauri ripoti za wagonjwa wanapimwa kwa
 kwa kutumia mashine hizo zitolewe haraka ili kuwapunguzia gharama za 
kukaa muda mrefu wagonjwa wanaotoka katika mikoa mingine.
Akizungumzia
 kuhusu mashine ya CT-Scan na MRI ambazo zimeharibika Kaimu Mkurugenzi 
Mtendaji wa MHN Profesa Lawrence Mseru amesema juhudi za kutengeneza 
mashine hizo zinafanyika na kwamba kifaa cha CT- Scan kilichoharibika 
kitaingia leo usiku wakati Spea ya MRI imeshawasili na matengenezo 
yanaendelea.
Mashine ya CT-Scan hupima wastani wa wagonjwa 40 hadi 60 kwa saa 24 wakati MRI hupima wagonjwa 20 kwa siku.
 
 
 
 
 
 

 
 
0 comments:
Post a Comment