Pages

Ads 468x60px

Wednesday, December 16, 2015

MUHIMBILI YAFUNGA CT-SCAN NYINGINE

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) inafunga mashine nyingine ya CT- Scan ambayo inategemewa kuanza kutoa huduma kesho mchana.

"Hivyo kufikia jumatatu ijayo Hospitali hiyo itakua na mashine mbili za CT-Scan ambazo zitakua zinafanya kazi hatua ambayo itaboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wagonjwa ambao wanatakiwa kupimwa kwa kutumia mashine hiyo," amesema Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Watoto na Wazee Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Watoto na Wazee Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo wakati alipotembelea mashine za CT-Scan na MRI katika hospitali hiyo.

Pamoja na mambo mengine Waziri huyo ameshauri ripoti za wagonjwa wanapimwa kwa kwa kutumia mashine hizo zitolewe haraka ili kuwapunguzia gharama za kukaa muda mrefu wagonjwa wanaotoka katika mikoa mingine.

Akizungumzia kuhusu mashine ya CT-Scan na MRI ambazo zimeharibika Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MHN Profesa Lawrence Mseru amesema juhudi za kutengeneza mashine hizo zinafanyika na kwamba kifaa cha CT- Scan kilichoharibika kitaingia leo usiku wakati Spea ya MRI imeshawasili na matengenezo yanaendelea.


Mashine ya CT-Scan hupima wastani wa wagonjwa 40 hadi 60 kwa saa 24 wakati MRI hupima wagonjwa 20 kwa siku.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates