Katibu
 Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile na Balozi wa Japani 
nchini Bw. Masaharu Yoshida wakibadilishana hati ya mkataba wa mkopo wa 
Shilingi Bilioni 210 kwa ajili ya mradi wa Umeme kati ya Tanzania na 
Kenya.
Katibu
 Mkuu Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile na Balozi wa Japani nchini
 Bw.Masaharu Yoshida wakisaini mkataba wa mkopo. Nyuma yao kushoto ni 
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eng. Omar Chambo, kulia ni 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Japani Seiji Kihara wakishuhudia tukio hilo 
katika ukumbi wa Wizara ya Fedha Jijini Dares Salaam.
Katibu
 Mkuu Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile akitoa ufafanuzi wa 
matumizi ya mkopo wa bilioni 210 baada ya kusaini mkataba wa mkopo huo 
katika ukumbi wa Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam.
SERIKALI
 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini mkataba na Serikali ya 
Japani kiasi cha shilingi Bilioni 210 kwa ajili ya maendeleo ya mradi wa
 njia ya kusafirishia umeme kati ya Tanzania na Kenya ambao utasaidia 
upatikanaji wa umeme wa kutosha.
Mkataba
 huo wa masharti nafuu ulisaininiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na 
Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile na Balozi 
wa Japani nchini Tanzania Bw. Masaharu Yoshida jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
 na waandishi wa habari baada ya kusaini mkataba huo Dkt. Likwelile 
alisema kuwa fedha hizo zitaelekezwa katika kusambaza nyaya za umeme 
zenye KV400, na urefu wa kilometa 414.5 kati ya Singida na Namanga 
kupitia Babati na Arusha.
Alisema
 kuwa kukamilika kwa mradi huo kutachochea maendeleo ya jamii na uchumi 
nchini kwa kuleta muungano wa kibiashara katika nchi za Afrika 
Mashariki.
Naye 
Balozi wa Japani nchini Tanzania Bw. Masaharu Yoshida alisema kuwa mkopo
 huo utafanikisha kusambaza nyanya za umeme zenye urefu wa takribani 
kilometa 508 kati ya Tanzania na Kenya ambapo Tanzania itasambaza 
kilometa 415 wakati Kenya itakuwa na kilometa 93.
Japani
 imekuwa ikisaidia Tanzania katika miradi ya umeme kwa muda mrefu, 
miradi ambayo tayari imekamilika ni pamoja na usambazaji umeme Zanzibar,
 mradi wa usambazaji nyaya za umeme mkoani Kilimanjaro na mradi wa 
kutengeneza nyaya mpya za umeme jijini Dar es Saalam.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment