Wananchi
 wa Mkoa wa Geita wameaswa kufuata kanuni za usafi wa mazingira ili 
kudhibiti maumbukizi ya ugonjwa wa kipindupindu,Hayo yamesemwa leo na 
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu 
mara baada ya kutembelea kambi ya kipindupindu iliyopo kwenye kituo cha 
afya cha Nyankumbu,mkoani hapa
Waziri
 Ummy akivaa vifaa maalum vya kujikinga na kipindupindu kabla ya kuingia
 kwenye kambi hiyo,kulia ni Mganga mfawidhi wa Kituo hicho Josephat 
Msafiri.(Picha Zote na Catherine Sungura WAMJW-GEITA)
 
Waziri Ummy akivua vifaa hivyo mara baada ya kutoka kuwasalimia wagonjwa
 wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi hiyo,wagonjwa waliopo hadi leo 
mchana ni wagonjwa wanne
  
 
 
Waziri huyo akiongea na mmoja wa wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi hiyo
  
 
 
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu 
akiwasalimia wagonjwa wa kipindupindu(hawapo pichani)kulia ni Mganga 
Mkuu wa Mkoa wa Geita Dkt.Joseph Kisala
  
 
 
Baadhi ya wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa kwenye kambi ya kituo cha afya cha Nyankumbu
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment