Pages

Ads 468x60px

Tuesday, October 27, 2015

Baba Levo na Udiwani Kigoma, Idris kufungiwa Instagram.. Kingwendu kashinda ubunge



Kwenye list ya mastaa ambao wamejitosa kwenye Siasa 2015, Baba Levo nae yumo… Baba Levo ameshukuru sana kwa ushindi wake huku akisema kwamba japo kashinda na anakuwa Diwani Kigoma mjini kwa miaka mitano lakini muziki hatouacha na atajitahidi pia kusaidia vijana wenye vipaji Kigoma ili waweze kutambulika kwa sanaa wanazofanya.
Baba Levo
Baba Levo
Kingwendu nae aliingia kwenye Siasa japo Kura hazikutosha hivyo kashindwa kuibuka na ushindi, amesema kushindwa kwake kunafanya ajipange upya kwa ajili Siasa kwenye msimu mwingine wa Uchaguzi 2020 Tanzania.
kingwendu
Mchekeshaji Kingwendu.
Account ya Instagram ya staa wa Big Brother, Idris Sultan haiko hewani… kama ulishtuka kutokumuona upande huo basi taarifa ikufikie kwamba Wamiliki wa Mtandao wa Instagram wameifungia account yake kwa muda kwa sababu alikiuka kanuni za Mtandao huo.
Idris
Idris Sultan.
Idris amesema alifungiwa baada ya kupost kipande cha video kutoka kwenye movie ambacho yeye hakujua kwamba hiyo movie imefungiwa… Idris amesema yuko kwenye mipango ya kujadiliana na Wamiliki wa Mtandao huo ili wamfungulie.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates