Timu 
ya Taifa Tanzania ya Wanawake ya Mpira wa Miguu (Twiga Stars) 
inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Wanawake ya 
Malawi Novemba 7, 2015 jijini Dar es salaam.
Mchezo
 huo wa kirafiki ni sehmu ya kujipima kwa Twiga Stars inayonolewa na 
kocha Rogasian Kaijage, ambayo ilishiriki Fainali za Michezo ya Afrika 
(All Africa Games) mwezi Agosti – Septemba nchini Congo – Brazzavile.
Awali 
Twiga Stars ilikua icheze mchezo huo nchini Malawi Oktoba 24, kabla ya 
chama cha soka nchini humo (FAM) kuahirisha mchezo huo, na sasa mchezo 
huo utacheza nchini Tanzania Novemba 07, 2015.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment