Mwenyekiti wa Kamati ya Soko la Samaki la Kimataifa la Feri, Ali Kibwana, akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko 
mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji
 wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for
 Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo. 
Kushoto ni Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.
Mwonekano wa sehemu ya soko la Samaki la Feri.
Na Dotto Mwaibale
ENEO
 la Lebanon katika Soko la Kimataifa la Samaki la Feri ambalo lipo 
jirani na Ikulu jijini Dar es Salaam limedaiwa kuwa ni hatari kwa 
wafanyabiashara wa soko hilo na kuwa linadhohofisha uchumi kutokana na 
kukithiri kwa watu wasio rasmi.
Hayo
 yamebainishwa na Mwezeshaji wa Sheria wa soko hilo, Asha Malenda wakati
 akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi 
wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani 
vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya 
Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili 
katika masoko hayo.
"Tunachangamoto
 kubwa sana katika soko letu la Feri tunayoipata kutoka eneo la Lebanon 
lenye mwingiliano wa watu wasio rasmi kutoka nje ya soko ambao ni kama 
wamejianzishia soko lao na wamekuwa na maamuzi yao lakini viongozi wa 
soko la Feri wanashindwa kuwachukulia hatua hali ambayo inatudhalilisha 
sisi wafanyabiashara hasa mama lishe na kuharibu uchumi wa soko letu" 
alisema Malenda.
Alisema
 wengi wa watu waliopo katika eneo hilo lisilo rasmi wamekuwa wakifanya 
biashara kiholela huku wakipika vyakula katika maeneo yanayoweza 
kuhatarisha afya ya mlaji wakati katika soko hilo kuna eneo maalumu la 
mama lishe na wengi wa watu hao wakienda kula eneo hilo rasmi wamekuwa 
hawalipi fedha na wakibanwa kulipa wanadiliki kutoa visu na silaha za 
jadi kuwatishia wanaodai.
"Eneo
 hilo la Lebanon ni hatari na kinachoshangaza linatizamana na Ikulu 
lakini hakuna hatua yoyote ya makusudi inayochukuliwa na viongozi wetu 
na linapopelekwa kwa viongozi wa kisiasa wanadai waachwe kwani ndio 
wapiga kura wao" alisema Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari 
Said.
Said
 alisema katika soko hilo kuna changoto nyingi za udhalilishaji wanawake
 kwa kushikwa katika maungo yao lakini kupitia EfG wamejitahidi 
kupunguza changamoto hizo kwani wasaidizi wa sheria waliopatiwa mafunzo 
na shirika hilo wanajitahidi kuupenyeza ujuzi waliopata kuifikishia 
jamii ambayo imeanza kuelewa kuhusu vitendo hivyo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment