Mwenyekiti wa Kamati ya Soko la Samaki la Kimataifa la Feri, Ali Kibwana, akizungumza
na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko
mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji
wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for
Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo.
Kushoto ni Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.
Mwonekano wa sehemu ya soko la Samaki la Feri.
Na Dotto Mwaibale
ENEO
la Lebanon katika Soko la Kimataifa la Samaki la Feri ambalo lipo
jirani na Ikulu jijini Dar es Salaam limedaiwa kuwa ni hatari kwa
wafanyabiashara wa soko hilo na kuwa linadhohofisha uchumi kutokana na
kukithiri kwa watu wasio rasmi.
Hayo
yamebainishwa na Mwezeshaji wa Sheria wa soko hilo, Asha Malenda wakati
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi
wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani
vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya
Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili
katika masoko hayo.
"Tunachangamoto
kubwa sana katika soko letu la Feri tunayoipata kutoka eneo la Lebanon
lenye mwingiliano wa watu wasio rasmi kutoka nje ya soko ambao ni kama
wamejianzishia soko lao na wamekuwa na maamuzi yao lakini viongozi wa
soko la Feri wanashindwa kuwachukulia hatua hali ambayo inatudhalilisha
sisi wafanyabiashara hasa mama lishe na kuharibu uchumi wa soko letu"
alisema Malenda.
Alisema
wengi wa watu waliopo katika eneo hilo lisilo rasmi wamekuwa wakifanya
biashara kiholela huku wakipika vyakula katika maeneo yanayoweza
kuhatarisha afya ya mlaji wakati katika soko hilo kuna eneo maalumu la
mama lishe na wengi wa watu hao wakienda kula eneo hilo rasmi wamekuwa
hawalipi fedha na wakibanwa kulipa wanadiliki kutoa visu na silaha za
jadi kuwatishia wanaodai.
"Eneo
hilo la Lebanon ni hatari na kinachoshangaza linatizamana na Ikulu
lakini hakuna hatua yoyote ya makusudi inayochukuliwa na viongozi wetu
na linapopelekwa kwa viongozi wa kisiasa wanadai waachwe kwani ndio
wapiga kura wao" alisema Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari
Said.
Said
alisema katika soko hilo kuna changoto nyingi za udhalilishaji wanawake
kwa kushikwa katika maungo yao lakini kupitia EfG wamejitahidi
kupunguza changamoto hizo kwani wasaidizi wa sheria waliopatiwa mafunzo
na shirika hilo wanajitahidi kuupenyeza ujuzi waliopata kuifikishia
jamii ambayo imeanza kuelewa kuhusu vitendo hivyo.
0 comments:
Post a Comment