Rais
 Dkt.John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya 
kuwasili katika makao makuu ya Wizara ya Fedha(HAZINA) kwa ziara ya 
kushtukiza leo mchana.Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt.Servacius 
Likwelile.Rais Magufuli alitembelea na kukagua ofisi zote wizarani hapo 
na kisha kuongea na viongozi waandamizi.
 Rais
 Dkt.John Pombe Magufuli akiwa na wafanyakazi wawili wa Wizara ya Fedha 
ambao ni walemavu Bwana Fundi Maruma na Frank Mkyama wakati Rais 
alipofanya ziara ya kushtukiza wizarani hapo leo.
Rais
 Dkt.John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi waandamizi wa Wizara ya
 Fedha wakati alipofanya ziara ya kushtukiza Wizarani hapo ambapo alitoa
 maagizo ya kuziba mianya ya wakwepa kodi.
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa 
Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amefanya ziara ya 
kushtukiza katika Ofisi za Wizara ya Fedha leo Ijumaa tarehe 6 Novemba, 
2015.
Katika ziara hiyo Mhe.Rais 
alipata fursa ya kutembelea baadhi ya Ofisi za Wizara na baadae  
kuzungumza na Viongozi wa Wizara ili kufahamu changamoto ambazo 
zinaikabili Wizara ya Fedha.Wakati akimkaribisha Mhe.Rais 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha        Dkt. Servacius Likwelile 
alimueleza kuwa Wizara ya Fedha inakabiliwa na changamoto kubwa 
inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani. 
 Miongoni mwa sababu ni 
misamaha ya kodi, wafanyabiashara wengi hasa wakubwa kukwepa kodi, 
makusanyo yasiyoridhisha ya maduhuli na kutokulipwa kwa kodi za majengo.
 Aidha Dkt. Likwelile alishauri ni bora kuwekwa mifumo mizuri, ikiwemo 
matumizi ya Tehama na EFDs.
“Pamoja na ziara yangu kuwa ni ya
 kustukiza nimefurahi sana kukuta Viongozi wote wapo ofisini na 
wanafanya kazi. Jambo hili limenipa faraja kubwa. Ziara yangu ya kuja 
hapa nimejifunza na kujua changamoto zipi zinazowakabili”. Alisema Mhe. 
Rais.
Nimesikia
 changomoto nyingi na 
ninaagiza kuwa muhakikishe walipa kodi wakubwa wanalipa kodi na 
kusimamia kikamilifu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili iweze 
kukusanya kodi kikamilifu na si kuwabana wafanya biashara wadogo 
wadogo.Mhe.Rais aliwataka Viongozi wa Wizara kufanya kazi kwa bidii ili 
kuvuka lengo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment