Pages

Ads 468x60px

Tuesday, November 10, 2015

KAMPUNI YA STAR MEDIA TANZANIA LIMITED YASHINDA TUZO YA UBORA YA WQC


 Makamu wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya utoaji huduma bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba kutoka kwa kampuni ya Business Initiative Directions (BID). Pamoja naye kulia ni Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang Liao.
 Makamu wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang Liao akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya utoaji huduma bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba kutoka kwa kampuni ya Business Initiative Directions (BID).
 
 
Kampuni ya Business Initiative Directions (BID) ya nchini Ufaransa imeitunuku kampuni ya StarTimes kutoka nchini tanzania tuzo ya World Quality Commitment (WQC) kwa utoaji huduma bora kwa wateja wake.
 
Sherehe za tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya 29 ziliyofanyika jijini Paris ambapo makampuni mbalimbali yalishinda yalishiriki.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kuonyesha tuzo hiyo Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania, Bw. Lanfang Liao amesema kuwa hiyo ni habari njema si tu kwa kampuni bali kwa taifa kwa ujumla kwa utoaji wa huduma bora kwa wateja wake.
 
“Tuzo hii imetolewa jijini Paris, Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba ambapo kampuni ya Business Initiative Directions (BID) ndio waandaaji wakuu wa tuzo hizi ambazo zimefanyika mara ya 29 kwa mwaka huu.” Alisema Bw. Liao

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates