Makamu
 wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), 
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya
 utoaji huduma bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi 
Oktoba kutoka kwa kampuni ya Business Initiative Directions (BID). 
Pamoja naye kulia ni Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang
 Liao.
 Makamu wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari.
Kaimu
 Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang Liao akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya utoaji huduma 
bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba kutoka kwa 
kampuni ya Business Initiative Directions (BID).
Kampuni
 ya Business Initiative Directions (BID) ya nchini Ufaransa imeitunuku 
kampuni ya StarTimes kutoka nchini tanzania tuzo ya World Quality 
Commitment (WQC) kwa utoaji huduma bora kwa wateja wake.
Sherehe za tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya 29 ziliyofanyika jijini Paris ambapo makampuni mbalimbali yalishinda yalishiriki.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kuonyesha tuzo 
hiyo Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania, Bw. Lanfang Liao 
amesema kuwa hiyo ni habari njema si tu kwa kampuni bali kwa taifa kwa 
ujumla kwa utoaji wa huduma bora kwa wateja wake.
“Tuzo
 hii imetolewa jijini Paris, Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba ambapo 
kampuni ya Business Initiative Directions (BID) ndio waandaaji wakuu wa 
tuzo hizi ambazo zimefanyika mara ya 29 kwa mwaka huu.” Alisema Bw. Liao
 
 
 
 
 
 



 
 
0 comments:
Post a Comment