Makamu
wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto),
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya
utoaji huduma bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi
Oktoba kutoka kwa kampuni ya Business Initiative Directions (BID).
Pamoja naye kulia ni Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang
Liao.
Makamu wa Rais wa kampuni ya StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari.
Kaimu
Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes, Bw. Lanfang Liao akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tuzo ya utoaji huduma
bora waliyoipokea nchini Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba kutoka kwa
kampuni ya Business Initiative Directions (BID).
Kampuni
ya Business Initiative Directions (BID) ya nchini Ufaransa imeitunuku
kampuni ya StarTimes kutoka nchini tanzania tuzo ya World Quality
Commitment (WQC) kwa utoaji huduma bora kwa wateja wake.
Sherehe za tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya 29 ziliyofanyika jijini Paris ambapo makampuni mbalimbali yalishinda yalishiriki.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kuonyesha tuzo
hiyo Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania, Bw. Lanfang Liao
amesema kuwa hiyo ni habari njema si tu kwa kampuni bali kwa taifa kwa
ujumla kwa utoaji wa huduma bora kwa wateja wake.
“Tuzo
hii imetolewa jijini Paris, Ufaransa mwishoni mwa mwezi Oktoba ambapo
kampuni ya Business Initiative Directions (BID) ndio waandaaji wakuu wa
tuzo hizi ambazo zimefanyika mara ya 29 kwa mwaka huu.” Alisema Bw. Liao
0 comments:
Post a Comment