Mkuu wa Dawati la Jinsia katika Kituo cha Polisi Mkoa wa Kipolisi Chang'ombe, Thecla Kitajo.
Mkuu
wa Dawati la Jinsia katika Kituo cha Polisi Mkoa wa Kipolisi
Chang'ombe, Thecla Kitajo (kulia), akizungumza na waandishi wa habari
(hawapo pichani), Dar es Salaam leo mchana, ambao wanatembelea vituo vya
polisi na masoko ya Manispaa za Ilala na Temeke kujionea jinsi vitendo
hivyo vilivyo pungua baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa
mafunzo ya kupinga ukatili huo katika maeneo hayo. Kushoto ni Ofisa wa
Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo hicho, Meshack Mpwage.
Ofisa wa Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo hicho, Meshack Mpwage, akizungumza katika mkutano huo.
Ofisa
wa Jeshi la Polisi wa Kituo cha Chang'ombe, Digna Ngatena (kushoto),
akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mwanasheria wa Shirika la EfG,
Grace Mate)
Maofisa
wa Jeshi la Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo cha Polisi Chang'ombe.
Kutoka kushoto ni Albentina Aloyce, Nuni Munisy na Rose Lukanga.
Dotto Mwaibale
WAKATI
vitendo vya ubakaji na udhalilishaji kwa watu wakubwa vikipungua
matukio ya vitendo hivyo kwa watoto wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es
Salaam vimekuwa vikiongezeka kila siku.
Hayo
yalibainishwa na Mkuu wa Dawati la Jinsia wa Kituo cha Polisi Mkoa wa
Kipolisi Temeke Chang'ombe Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Thecla
Kitajo wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo
mchana, ambao wanafanya ziara katika masoko ya Manispaa ya Ilala na
Temeke na vituo vya polisi kujua vitendo vya ukatili wa kijinsia
ulivyopungua katika maeneo hayo baada ya Shirika la Equality for Growth
(EfG), kutoa mafunzo ya kupinga ukati huo.
0 comments:
Post a Comment