Mkuu wa Dawati la Jinsia katika Kituo cha Polisi Mkoa wa Kipolisi Chang'ombe, Thecla Kitajo.
 Mkuu
 wa Dawati la Jinsia katika Kituo cha Polisi Mkoa wa Kipolisi 
Chang'ombe, Thecla Kitajo (kulia), akizungumza na waandishi wa habari 
(hawapo pichani), Dar es Salaam leo mchana, ambao wanatembelea vituo vya
 polisi na masoko ya Manispaa za Ilala na Temeke kujionea jinsi vitendo 
hivyo vilivyo pungua baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa
 mafunzo ya kupinga ukatili huo katika maeneo hayo. Kushoto ni Ofisa wa 
Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo hicho, Meshack Mpwage.
 Ofisa wa Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo hicho, Meshack Mpwage, akizungumza katika mkutano huo.
 Ofisa
 wa Jeshi la Polisi wa Kituo cha Chang'ombe, Digna Ngatena (kushoto), 
akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mwanasheria wa Shirika la EfG, 
Grace Mate)
Maofisa
 wa Jeshi la Polisi wa Dawati la Jinsia wa Kituo cha Polisi Chang'ombe. 
Kutoka kushoto ni Albentina Aloyce, Nuni Munisy na Rose Lukanga.
Dotto Mwaibale
WAKATI
 vitendo vya ubakaji na udhalilishaji kwa watu wakubwa vikipungua 
matukio ya vitendo hivyo kwa watoto wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es 
Salaam vimekuwa vikiongezeka kila siku.
Hayo
 yalibainishwa na Mkuu wa Dawati la Jinsia wa Kituo cha Polisi Mkoa wa 
Kipolisi Temeke Chang'ombe Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Thecla 
Kitajo wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo 
mchana, ambao wanafanya ziara katika masoko ya Manispaa ya Ilala na 
Temeke na vituo vya polisi kujua vitendo vya ukatili wa kijinsia 
ulivyopungua katika maeneo hayo baada ya Shirika la Equality for Growth 
(EfG), kutoa mafunzo ya kupinga ukati huo.
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment