Pages

Ads 468x60px

Tuesday, November 10, 2015

RAIS MAGUFULI AMJULIA HALI DKT. HELLEN KIJO BISIMBA, AFANYA ZIARA YA GHAFLA MUHIMBILI



 Rais Dkt. John Pombe Magufuli, akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliolazwa kwenye hospitali ya taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya Novemba 9, 2015




Rais Dkt.John Pombe Magufuli akimjulia hali Mkurugenzi wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC) Dkt.Helen Kijo Bisimba aliyelazwa katika hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam leo Novemba 9, 2015. Dkt. Bisimba aliujeruhiwa katika ajali gari jijini Dar es Salaam, Novemba 8 2015. Rais pia alifanya ziara ya kushtukiza kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili, MNH, ili kujionea yeye mwenyewe jinsi wafanyakazi wanavyotekeleza majukumu yao katika kuhudumia Watanzania


Rais Dkt.john Pombe Magufuli akizungumza na kuwapa moyo wauguzi katika hospitali ya taifa Muhimbili wakati alipofanya ziara ya ghafa kujionea hali halisi.
 Rais Dkt.John Pombe Magufuli akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili wakati alipofanya ziara ya kushtukiza hospitalini hap oleo na kuwafariji wagonjwa.

 Rais akiagana na wauguzi na wafanyakazi wa hospitali ya taifa Muhimbili


Rais akipungia mkono, wagonjwa na wananchi wakati alipotembelea hospitali ya taifa Muhimbili

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates