CHUO
 cha Kodi cha Mwenge jijini Dar es Salam wameitikia wito wa kauli ya 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Joseph Magufuli 
kufanya usafi katika mazingira ya Chuo hicho.
Kaimu
 Mkuu wa Chuo cha Kodi, Edward Mwakimonga amewasihi wanafunzi pamoja na 
wananchi kwa ujumla kuwa usafi ni afya na ikiwezekana iwe ni kawaida 
kufanya usafi kila baada ya wiki mara moja ili kuweka mazingira safi.
Nae
 Waziri Mkuu wa serikali ya chuo cha Kodi, Jeremia Shushu amewashukuru 
wanafunzi pamoja na menejimenti ya chuo hicho kwa kukubali na kujitokeza
 kwa wingi kushirikiana kufanya usafi katika mazingira ya chuo chao.
 
 
 
 
 
 




 
 
0 comments:
Post a Comment