Pages

Ads 468x60px

Wednesday, December 9, 2015

WANAFUNZI WA CHUO CHA KODI JIJINI DAR WATIMIZA WAJIBU

CHUO cha Kodi cha Mwenge jijini Dar es Salam wameitikia wito wa kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Joseph Magufuli kufanya usafi katika mazingira ya Chuo hicho.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Kodi, Edward Mwakimonga amewasihi wanafunzi pamoja na wananchi kwa ujumla kuwa usafi ni afya na ikiwezekana iwe ni kawaida kufanya usafi kila baada ya wiki mara moja ili kuweka mazingira safi.


Nae Waziri Mkuu wa serikali ya chuo cha Kodi, Jeremia Shushu amewashukuru wanafunzi pamoja na menejimenti ya chuo hicho kwa kukubali na kujitokeza kwa wingi kushirikiana kufanya usafi katika mazingira ya chuo chao.





Wanafunzi wa chuo cha Kodi wakishirikiana bega kwa bega kufanya usafi katika chuo chaoo leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni kusherekea sikukuu ya Uhuru Desemba 9.Wanafunzi wakizoa takataka.

0 comments:

Post a Comment

 
Blogger Templates